Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 13A

Mahekalu Tofauti, Masomo Tofauti

Mahekalu Tofauti, Masomo Tofauti

Hekalu Ambalo Ezekieli Aliona:

  • Ezekieli aliwafafanulia wahamishwa Wayahudi huko Babiloni kulihusu

  • Lina madhabahu ambapo dhabihu nyingi zinatolewa

  • Linakazia viwango vya Yehova vya uadilifu kuhusu ibada

  • Linakazia fikira zetu kwenye kurudishwa kwa ibada safi kulikoanza mwaka wa 1919

Hekalu Kubwa la Kiroho:

  • Paulo alilifafanua alipokuwa akiwaandikia Wakristo Waebrania

  • Lina madhabahu ambapo dhabihu moja inatolewa, “mara moja kwa wakati wote” (Ebr. 10:10)

  • Linafafanua uhalisi wa mpango wa kiroho ambao ulikaziwa zamani kupitia hema la ibada na mahekalu halisi—Mpango wa Yehova wa ibada safi kwa msingi wa dhabihu ya fidia ya Kristo

  • Linakazia fikira zetu kwenye kazi ambayo Kristo alifanya akiwa Kuhani Mkuu Zaidi kuanzia mwaka wa 29 hadi 33 W.K.