Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KISANDUKU CHA KUFUNDISHIA 15A

Dada Makahaba

Dada Makahaba

Mu Ezekieli sura ya 23, tunasoma kuhusu hukumu kali ya Mungu juu ya ukosefu wa uaminifu wa watu wake. Kuko mambo mingi yenye inafanana kati ya sura hii na sura ya 16. Kama vile sura ya 16, sura ya 23 pia inazungumuzia ukahaba wa mufano. Unabii unasema kama Yerusalemu njo dada mudogo na Samaria njo dada yake mukubwa. Sura zote mbili zinaonyesha namna ule dada mudogo alifuata mufano wa dada yake mukubwa kwa kufanya ukahaba; lakini kisha wakati fulani, alitenda uovu na uasherati kupita dada yake mukubwa. Mu sura ya 23, Yehova anaonyesha majina ya wale dada wawili: Ohola njo dada mukubwa, ni kusema, Samaria, muji mukubwa wa ufalme wa makabila kumi ya Israeli; Oholiba njo dada mudogo, ni kusema, Yerusalemu, muji mukubwa wa Yuda. *​—Eze. 23:1-4.

Zile sura mbili ziko na mambo ingine yenye inafanana. Pengine mambo makubwa zaidi yenye inafanana ni hii: Ku mwanzo, wale makahaba ni bibi za Yehova, lakini kisha, wanamusaliti. Tena, kuko ahadi yenye inatoa tumaini. Sura ya 23 inazungumuzia tumaini la ukombozi, lakini inaonyesha jambo fulani lenye kuzungumuziwa pia mu sura ya 16 wakati Yehova anasema: “Nitakomesha mwenendo wako muchafu na ukahaba wako.”​—Eze. 16:16, 20, 21, 37, 38, 41, 42; 23:4, 11, 22, 23, 27, 37.

Je, Wanafananisha Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo?

Zamani, vichapo vyetu vilikuwa vinasema kama wale dada wawili, Ohola na Oholiba, walikuwa wanafananisha Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo, zenye zinagawanyika mu sehemu mbili: Kanisa Katoliki na Kanisa la Kiprotestanti. Lakini, kisha tena kusali na kufanya utafiti mwingi, kumetokea maulizo fulani mazito. Je, kuko wakati Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo zilikuwaka bibi ya Yehova mu njia fulani? Je, kuko wakati zishakakuwa mu agano naye? Jibu ni hapana. Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo hazikukuwaka wakati Yesu alikuwa mupatanishi wa “agano jipya” na Israeli wa kiroho; tena, Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo haziyakuwaka sehemu ya ile taifa ya kiroho ya Wakristo watiwa-mafuta. (Yer. 31:31; Lu. 22:20) Zilitokeaka kisha kifo cha mitume. Mu karne ya 4 (301-400) K.K.Y. zilifikia kuwa tengenezo lenye kuasi-imani, lenye kupotoka, lenye kufanyizwa na “magugu,” ni kusema, Wakristo wa uongo wa unabii wa Yesu wa ngano na magugu.​—Mt. 13:24-30.

Tofauti ingine kubwa ni hii: Yehova alitoa tumaini yenye kuonyesha kama hali ya kukosa uaminifu ya Yerusalemu na Samaria ingebadilika. (Eze. 16:41, 42, 53-55) Je, Biblia inatoa tumaini ya vile kuhusu Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo? Hapana! Hazina tumaini sawasawa na dini zingine za Babiloni Mukubwa.

Kwa hiyo, Ohola na Oholiba hawafananishe Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo. Lakini, hali yao inatusaidia kuelewa muzuri zaidi jambo fulani la lazima: namna Yehova anajisikia kuhusu wale wenye wanavunjia heshima jina lake takatifu na kuzaraulisha kanuni zake za ibada safi. Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo ziko na hatia kubwa mu ile mambo sababu zinasema kama zinatumikia Mungu mwenye anazungumuziwa mu Biblia. Tena, zinasema kama Yesu, Mwana mupendwa wa Yehova, njo kiongozi wao. Lakini zinajipinga wakati zinafundisha kama Yesu ni sehemu ya Utatu na wakati zinakosa kutii amri yake yenye kuwa wazi ya kama haifae kuwa “sehemu ya ulimwengu.” (Yoh. 15:19) Kwa kuendelea kujiingiza mu ibada ya sanamu na mu mipango ya politike, Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo zimeonyesha waziwazi kama ziko sehemu ya “kahaba mukubwa.” (Ufu. 17:1) Bila kuenda kuume ao kushoto, hazitaponyoka uharibifu wenye unangojea dini zote za uongo!

^ fu. 3 Ile majina iko na maana fulani. Ohola maana yake “Hema Yake [ya Ibada]”​—ni wazi kama ile inahusiana na tabia ya Israeli ya kujitilia fasi zake mwenyewe za ibada kuliko kutumia hekalu la Yehova la Yerusalemu. Oholiba, kwa upande mwingine, maana yake “Hema Yangu [ya Ibada] Iko Ndani Yake.” Yerusalemu njo kwenye nyumba ya Yehova ilikuwa.