Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KISANDUKU CHA KUFUNDISHIA 16A

Je, Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo Zinafananisha Yerusalemu ya Zamani?

Je, Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo Zinafananisha Yerusalemu ya Zamani?

Zamani, vichapo vyetu vilisema kama Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo zinafananisha Yerusalemu yenye kuasi ya zamani. Hali zenye zilikuwa mu Yerusalemu yenye ilikosa uaminifu​—sawa vile ibada ya sanamu na upotovu mwingi—​zinafanana kabisa na mambo yenye iko inafanyika leo mu Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo. Lakini, vichapo vya hivi karibuni, kutia ndani kitabu hiki chenye uko unasoma, havifasirie tena unabii kwa kutumia vifananishi na vifananishwa wakati Biblia haitoe musingi wenye uko wazi wa kufanya vile. Je, kuko sababu ya Kimaandiko ya kuonyesha kama Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo zinafananisha Yerusalemu ya zamani? Hakuna.

Fikiria mambo hii: Wakati fulani, Yerusalemu ilikuwa fasi ya maana sana ya ibada safi; kisha, wakaaji wake waligeuka na kuwa waasi-imani. Lakini, Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo haziyafanyaka ibada safi. Kuanzia tu wakati zilianza mu karne ya ine (301-400) K.K.Y., Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo zinafundishaka tu mafundisho ya uongo.

Zaidi ya ile, kisha Wababiloni kuharibu Yerusalemu, Yehova alikubali tena ile muji na ikakuwa tena fasi ya maana ya ibada ya kweli. Lakini hakuna siku Mungu amekubali Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo, na saa zitaharibiwa wakati wa taabu kubwa, hazitatokeaka tena.

Kulingana na ile yote, tunaweza kusema nini? Wakati tunachunguza maunabii ya Biblia yenye ilitimia juu ya Yerusalemu yenye ilikosa uaminifu, tunaweza kuona kama, ‘Hii ao ile inafanana na mambo yenye tuko tunaona leo mu Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo.’ Lakini hakuna musingi wowote wa Kimaandiko wa kufanya tuseme kama Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo zinafananisha Yerusalemu ya zamani.