Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 18A

Yehova Aonya Kuhusu Vita Vikubwa Vinavyokaribia

Yehova Aonya Kuhusu Vita Vikubwa Vinavyokaribia

Biblia ina unabii mwingi unaotoa onyo kuhusu vita vya mwisho, Yehova atakapowaangamiza wale wanaompinga yeye na watu wake. Orodha ifuatayo ina baadhi ya unabii huo. Ona ulinganifu kati ya maonyo hayo, na pia ona kwamba Yehova amehakikisha wanadamu wote wanapata nafasi ya kusikia na kuchukua hatua.

KATIKA ISRAELI LA KALE

EZEKIELI: “‘Nitauita upanga umshambulie [Gogu] kwenye milima yangu yote,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”—Eze. 38:18-23.

YEREMIA: “[Yehova] atawahukumu wanadamu wote. Naye atawaangamiza waovu kwa upanga.”—Yer. 25:31-33.

DANIELI: “Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao . . . utazipondaponda na kuzikomesha falme hizi zote.”—Dan. 2:44.

KARNE YA KWANZA W.K.

YESU: “Kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijawahi kutokea tangu mwanzo wa ulimwengu.”—Mt. 24:21, 22.

PAULO: “Yesu . . . pamoja na malaika wake wenye nguvu . . . [wataleta] kisasi juu ya wale wasiomjua Mungu.”—2 The. 1:6-9.

PETRO: “Siku ya Yehova itakuja kama mwizi, . . . na dunia na kazi zilizo ndani yake zitafunuliwa.”—2 Pet. 3:10.

YOHANA: “Kinywani mwake [Yesu] upanga mrefu mkali unachomoza, upanga ambao atatumia kuyapiga mataifa.” —Ufu. 19:11-18.

NYAKATI ZETU

Biblia ndicho kitabu kilichotafsiriwa na kusambazwa zaidi katika historia yote

WATUMISHI WA YEHOVA WA SIKU HIZI . . .

  • Wanasambaza mabilioni ya machapisho yanayozungumzia Biblia katika mamia ya lugha

  • Wanatumia mamia ya mamilioni ya saa kila mwaka wakihubiri