Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 21A

“Mchango Mtakaoweka Kando”

“Mchango Mtakaoweka Kando”

Ezekieli 48:8

Acheni tujiunge na Ezekieli anapochunguza kwa undani eneo ambalo Yehova aliliweka kando. Lina sehemu tano. Ni sehemu gani hizo? Na zinatimiza kusudi gani?

A. “Mchango”

Ni eneo kwa ajili ya utawala na linaitwa “eneo la usimamizi.”

EZE. 48:8

B. “Mchango Mzima”

Ni sehemu iliyowekwa kando kwa ajili ya makuhani, Walawi, na jiji. Pia, watu kutoka makabila yote 12 wanaingia kwenye sehemu hii ili kumwabudu Yehova na kuunga mkono mpango wa usimamizi.

EZE. 48:20

C. “Eneo la Kiongozi”

“Ardhi hii itakuwa mali yake katika Israeli.” “Itakuwa mali ya kiongozi.”

EZE. 45:7, 8; 48:21, 22

D. “Mchango Mtakatifu”

Eneo hili linafafanuliwa pia kuwa “sehemu takatifu.” Sehemu ya juu ni kwa ajili ya “Walawi.” Ni “kitu kitakatifu.” Sehemu ya katikati ni “mchango mtakatifu kwa ajili ya makuhani.” Ni “mahali kwa ajili ya nyumba zao, na mahali patakatifu kwa ajili ya patakatifu,” au hekalu.

EZE. 45:1-5; 48:9-14

“Eneo Linalobaki”

Litakuwa la “watu wote wa nyumba ya Israeli” na “litakuwa la matumizi ya kawaida ya jiji, kwa ajili ya makao na malisho.”

EZE. 45:6; 48:15-19