Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KISANDUKU CHA KUFUNDISHIA 21A

“Muchango Wenye Mutatia Pembeni”

“Muchango Wenye Mutatia Pembeni”

EZEKIELI 48:8

Tufuate Ezekieli wakati anakaza uangalifu wake juu ya sehemu ya inchi yenye Yehova anatia pembeni. Ile sehemu iko na maeneo tano. Maeneo gani? Na ile maeneo iko na kazi gani?

A. “Muchango”

Ni eneo la guvernema na linaitwa pia “eneo la usimamizi.”

EZE. 48:8

B. “Muchango Muzima”

Unatiwa pembeni kwa ajili ya makuhani, Walawi, na muji. Tena, watu wa makabila yote 12 wanaingia mu ile eneo juu ya kumuabudu Yehova na kutegemeza mupango wa usimamizi.

EZE. 48:20

C. “Eneo la Mukubwa”

“Sehemu hiyo ya udongo itakuwa mali yake katika Israeli.” “Itakuwa ya mukubwa.”

EZE. 45:7, 8; 48:21, 22

D. “Muchango Mutakatifu”

Eneo hii inaitwa pia “sehemu takatifu.” Sehemu ya juu ni “kwa ajili ya Walawi.” Ni “kitu kitakatifu.” Sehemu ya katikati ni “muchango mutakatifu kwa ajili ya makuhani.” Ni “mahali kwa ajili ya nyumba zao na mahali patakatifu kwa ajili ya patakatifu,” ao hekalu.

EZE. 45:1-5; 48:9-14

E. “Eneo Lenye Linabakia”

‘Litakuwa la nyumba yote ya Israeli’ na “litakuwa la matumizi ya kawaida ya muji, kwa ajili ya makao na eneo la malisho.”

EZE. 45:6; 48:15-19