Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Barua Kutoka ku Baraza Lenye Kuongoza

Barua Kutoka ku Baraza Lenye Kuongoza

“Mungepaswa kuwa walimu.” (Ebr. 5:12) Waza kidogo! Yehova​—Mwalimu muzuri zaidi mu ulimwengu wote​—anatualika sisi tufundishe wengine juu yake! Kila mugao wa kufundisha kweli juu ya Yehova​—ikuwe mu familia, mu kutaniko, ao mu mahubiri​—ni pendeleo la maana sana na ni daraka nzito. Tunaweza kufanya nini juu tuweze?

Jibu linapatikana mu maneno yenye mutume Paulo aliandikiaka Timoteo: “Endelea kufanya bidii katika kusoma mbele ya watu, kutia moyo, na kufundisha.” Paulo aliongezea hivi: “Kwa kufanya vile utajiokoa wewe mwenyewe na utaokoa pia wale wenye wanakusikiliza.” (1 Ti. 4:13, 16) Uko na ujumbe wa kutangaza wenye unaweza kuokoa uzima. Kwa hiyo, inaomba ujikaze kuwa musomaji na mufundishaji muzuri. Broshua hii imetayarishwa juu ikusaidie ufikie ile kusudi. Ona sehemu fulani za broshua hii.

Andiko lenye liko ku kila ukurasa linaonyesha kanuni ya Biblia yenye inapatana na somo ya kujifunza ao namna ya kutumia somo yenye iko inazungumuziwa

Yehova ni “Mufundishaji Mukubwa.” (Isa. 30:20) Broshua hii itakusaidia ukuwe musomaji na mufundishaji muzuri, lakini, usisahau hata kidogo kwamba ujumbe wetu unatoka kwa Yehova na yeye njo anavutaka watu. (Yoh. 6:44) Kwa hiyo, ukuwe unamuomba kila mara akupatie roho takatifu. Ukuwe unatumia sana Neno la Mungu. Saidia watu wakaze akili yao juu ya Yehova, hapana juu yako. Ujikaze kusaidia wasikilizaji wako wamupende sana mu mioyo yao.

Umealikwa kufundisha ujumbe wa maana sana kupita ujumbe wote wenye wanadamu wamekwisha kupewa. Tuko hakika kama utaweza kama unaendelea kutegemea “nguvu zenye Mungu anatoa.”​—1 Pe. 4:11.

Walimu wenzako,

Baraza Lenye Kuongoza la Mashahidi wa Yehova