Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 3

Kutumia Maswali

Kutumia Maswali

Mathayo 16:13-16

MUHTASARI: Uliza maswali kwa busara ili kuchochea na kudumisha upendezi, kujadiliana na wasikilizaji wako, na kukazia mambo muhimu.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Chochea na kudumisha upendezi. Uliza maswali yasiyohitaji majibu ambayo yatachochea udadisi wa msikilizaji wako na kumfanya afikiri.

  • Zungumzia habari kwa mfuatano mzuri. Wasaidie wasikilizaji wako wafuate mawazo kwa mpangilio fulani kwa kuuliza mfululizo wa maswali yanayowasaidia kufikia mkataa unaofaa.

  • Kazia mambo muhimu. Uliza swali lenye kuchochea ili kutokeza wazo kuu. Tumia maswali ya pitio baada ya kuzungumzia jambo muhimu au unapomalizia mazungumzo yako.