SOMO LA 3
Kutumia Maswali
Mathayo 16:13-16
MUHTASARI: Uliza maswali kwa busara ili kuchochea na kudumisha upendezi, kujadiliana na wasikilizaji wako, na kukazia mambo muhimu.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
-
Chochea na kudumisha upendezi. Uliza maswali yasiyohitaji majibu ambayo yatachochea udadisi wa msikilizaji wako na kumfanya afikiri.
-
Zungumzia habari kwa mfuatano mzuri. Wasaidie wasikilizaji wako wafuate mawazo kwa mpangilio fulani kwa kuuliza mfululizo wa maswali yanayowasaidia kufikia mkataa unaofaa.
-
Kazia mambo muhimu. Uliza swali lenye kuchochea ili kutokeza wazo kuu. Tumia maswali ya pitio baada ya kuzungumzia jambo muhimu au unapomalizia mazungumzo yako.