Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 3

Kutumia Maulizo

Kutumia Maulizo

Matayo 16:13-16

JAMBO LA KUFANYA: Uliza maulizo kwa busara juu ya kufanya watu wakuwe na hamu ya kukusikiliza na waendelee kuwa na ile hamu, juu ya kufikiri na wasikilizaji wako, na juu ya kukazia mambo makubwa.

NAMNA YA KUFANYA VILE:

  • Fanya wasikilizaji wakuwe na hamu ya kukusikiliza na waendelee kuwa nayo. Uliza maulizo yenye itafanya wasikilizaji wafikiri kuhusu habari yenye uko unazungumuzia na wakuwe na hamu ya kujua.

  • Fikiri nao kuhusu habari yako. Saidia wasikilizaji wako waone namna wazo fulani linapatana na akili kwa kuuliza maulizo yenye itawasaidia wafikie kuamua mambo muzuri.

  • Kazia mambo makubwa. Juu ya kutanguliza wazo la maana, tumia ulizo lenye kufanya mutu akuwe na hamu ya kujua. Tumia maulizo ya kujikumbusha kisha kuzungumuzia jambo la maana ao wakati unamalizia habari yako.