Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 4

Kutoa Utangulizi Mzuri wa Maandiko

Kutoa Utangulizi Mzuri wa Maandiko

Mathayo 22:41-45

MUHTASARI: Tayarisha akili za wasikilizaji wako kabla ya kusoma andiko.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Fikiria lengo lako la kusoma andiko. Toa utangulizi wa kila andiko kwa njia itakayowafanya wasikilizaji wako wakazie fikira jambo kuu katika mstari unaosoma.

  • Tumia Biblia kuwa mamlaka yako. Unapozungumza na watu wanaomwamini Mungu, wasaidie waikazie fikira Biblia kuwa Neno la Mungu. Unapofanya hivyo utawaonyesha kwamba unawafundisha mawazo ya Mungu.

  • Chochea upendezi wa wasikilizaji wako. Uliza swali ambalo litajibiwa katika andiko, taja tatizo ambalo litatatuliwa na andiko, au taja kanuni ambayo itafafanuliwa na simulizi la Biblia.