SOMO YA 4
Kutanguliza Maandiko Muzuri
NAMNA YA KUFANYA VILE:
-
Ujue kwanza juu ya nini unasoma andiko. Tanguliza andiko mu namna yenye inasaidia wasikilizaji wako waone jambo la maana lenye unataka kuwaonyesha mu ile andiko.
-
Onyesha kama mambo yenye unasema inatoka mu Biblia. Wakati uko unasema na watu wenye wanaamini Mungu, uwapeleke mu Biblia, Neno la Mungu. Kwa kufanya vile unaonyesha kama mu Biblia njo muko hekima ya muzuri zaidi.
-
Fanya wasikilizaji wako wakuwe na hamu ya kusoma andiko. Uliza ulizo lenye andiko litajibia, taja magumu fulani yenye andiko litasaidia kuimaliza, ao onyesha kanuni yenye habari fulani ya Biblia itawasaidia kuelewa.