SOMO LA 5
Kusoma kwa Usahihi
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
-
Tayarisha vizuri. Elewa kusudi la kuandikwa kwa simulizi hilo. Jizoeze kusoma mafungu ya maneno, si neno mojamoja. Epuka kuongeza, kurukaruka, au kubadilisha maneno. Zingatia alama za vituo.
-
Tamka kila neno kwa usahihi. Ikiwa hujui jinsi neno linavyotamkwa, liangalie katika kamusi, sikiliza rekodi ya chapisho lililosomwa, au uombe msaada kutoka kwa msomaji mzuri.
-
Zungumza waziwazi. Tamka maneno waziwazi, inua kichwa chako na ufumbue kabisa kinywa unapoongea. Jitahidi kutamka kila silabi.