Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 5

Kusoma Bila Makosa

Kusoma Bila Makosa

1 Timoteo 4:13

JAMBO LA KUFANYA: Soma mambo kwa sauti vile inaandikwa mu kichapo.

NAMNA YA KUFANYA VILE:

  • Jitayarishe muzuri. Wazia sababu yenye ilifanya ile habari iandikwe. Ufanye mazoezi ya kusoma makundi ya maneno, hapana tu neno moja-moja. Ukuwe muangalifu juu usiongeze maneno, ao kuruka maneno, ao kutia neno fulani lenye haliko. Heshimia alama za vituo, sawa vile nukta (.), mukato (,), alama ya kuuliza (?).

  • Sema kila neno muzuri. Kama haujue namna ya kusema neno fulani, iangalie mu diksionere, sikiliza usomaji wenye ulirekodiwa wa kichapo, ao omba musomaji muzuri akusaidie.

  • Sema maneno ya kusikilika. Sema maneno muzuri, simamisha kichwa na ufungue kinywa muzuri. Jikaze kusema kila silabe.