Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 6

Kufasiria Waziwazi Sababu ya Kutumia Andiko

Kufasiria Waziwazi Sababu ya Kutumia Andiko

Yohana 10:33-36

JAMBO LA KUFANYA: Usisome tu andiko na kuenda mara moja ku jambo lingine. Hakikisha kama wasikilizaji wako wanaona waziwazi namna andiko lenye unasoma linapatana na wazo lenye unataka kuwafundisha.

NAMNA YA KUFANYA VILE:

  • Onyesha maneno ya maana. Kisha kusoma andiko, onyesha maneno yenye inapatana moja kwa moja na jambo kubwa lenye unataka kuwafundisha. Unaweza kufanya vile kwa kurudilia ile maneno ao kwa kuuliza maulizo yenye itasaidia wasikilizaji wako waone maneno ya maana.

  • Kazia jambo lenye unataka wakumbuke. Kama ulitanguliza andiko kwa kuonyesha sababu yenye inafanya muisome, eleza namna gani maneno ya maana ya ile andiko inapatana na ile sababu.

  • Toa mafasirio ya mwepesi. Epuka kutoa maelezo juu ya mambo yenye haina uhusiano na jambo kubwa lenye unataka kufundisha. Kisha kufikiria mambo yenye tayari wasikilizaji wako wanajua kuhusu habari yako, amua ni maelezo ngapi itakuwa ya lazima juu wasikilizaji wako waelewe wazo lenye unataka kuwafundisha.