Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 15

Kuzungumza kwa Usadikisho

Kuzungumza kwa Usadikisho

1 Wathesalonike 1:5

MUHTASARI: Onyesha kwa uthabiti kwamba unaamini yale unayosema ni kweli na ni muhimu.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Tayarisha kikamili. Jifunze habari hiyo mpaka uelewe mambo makuu kikamili na jinsi Maandiko yanavyothibitisha mambo hayo kuwa ya kweli. Jaribu kueleza mawazo makuu ya habari yako kwa maneno machache rahisi. Kazia fikira jinsi habari hiyo itakavyowasaidia wasikilizaji wako. Sali upate roho takatifu.

  • Tumia maneno yanayoonyesha usadikisho. Badala ya kurudia maneno yaliyo kwenye chapisho, tumia maneno yako mwenyewe. Chagua maneno yanayoonyesha kwamba una uhakika na mambo unayosema.

  • Zungumza kwa mkazo na unyoofu. Zungumza kwa sauti inayofaa. Ikiwa desturi za kwenu zinaruhusu, watazame wasikilizaji.