Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 17

Kusema Mambo ya Kueleweka

Kusema Mambo ya Kueleweka

1 Wakorinto 14:9

JAMBO LA KUFANYA: Saidia wasikilizaji wako waelewe maana ya habari yako.

NAMNA YA KUFANYA VILE:

  • Jifunze habari yako muzuri kabisa. Elewa habari muzuri juu uweze kuifasiria mu njia ya mwepesi na mu maneno yako.

  • Tumia misemwa ya mufupi-mufupi na ya mwepesi. Hata kama haiko mubaya kutumia misemwa ya murefu-murefu, sema mambo ya maana kwa kutumia misemwa ya mufupi-mufupi.

  • Fasiria maneno yenye haijulikane sana. Usitumie sana maneno yenye wasikilizaji wako hawajue. Kama ni lazima utumie neno lenye halijulikane sana, ao kuzungumuzia mutu fulani mu Biblia mwenye hajulikane sana, ao kipimo ao desturi fulani ya zamani, leta mafasirio.