Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 18

Kuwaelimisha Wasikilizaji

Kuwaelimisha Wasikilizaji

1 Wakorintho 9:19-23

MUHTASARI: Wachochee wasikilizaji wako wafikiri, wabaki wakihisi kwamba wamejifunza jambo muhimu.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Zingatia kile ambacho wasikilizaji tayari wanajua. Badala ya kurudia mambo ambayo wanajua, wasaidie waione habari hiyo kwa njia mpya.

  • Fanya utafiti na utafakari. Ikiwezekana, tia ndani habari zisizojulikana sana au matukio ya karibuni kufafanua mawazo makuu. Fikiria kwa kina kuhusu habari utakayotoa na uhusiano kati ya habari hiyo na mambo hakika unayotaka kutaja.

  • Onyesha umuhimu wa ujumbe wako. Eleza jinsi habari za Kimaandiko zinavyoweza kuwasaidia wasikilizaji katika maisha yao ya kila siku. Zungumzia hali hususa, mitazamo, na matendo yanayofaana na wasikilizaji wako.