Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 18

Kufundisha Kabisa Wasikilizaji Wako

Kufundisha Kabisa Wasikilizaji Wako

1 Wakorinto 9:19-23

JAMBO LA KUFANYA: Saidia wasikilizaji wafikiri juu ya habari, juu waone kama wamejifunza kitu fulani cha lazima.

NAMNA YA KUFANYA VILE:

  • Fikiria mambo yenye wasikilizaji wako wanajuaka. Kuliko tu kurudilia-rudilia mambo yenye walishakasikia, uwasaidie wafikirie ile habari mu njia ingine.

  • Tafuta habari mu vichapo na uwaze sana. Wakati inawezekana, tumia habari zenye hazijulikane sana ao mambo yenye ilitokea sasa hivi juu ya kuzungumuzia mawazo ya maana. Waza sana juu ya habari yako na uone kama inapatana mambo yenye unapenda kutaja.

  • Onyesha namna habari yako inaweza kusaidia. Eleza namna mawazo ya Maandiko inaweza kusaidia wasikilizaji wako mu maisha yao ya kila siku. Zungumuzia hali fulani, mielekeo fulani, na matendo fulani yenye inahusu wasikilizaji wako.