Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 19

Kujikaza Kugusa Moyo

Kujikaza Kugusa Moyo

Mezali 3:1

JAMBO LA KUFANYA: Saidia wasikilizaji wako waone faida ya mambo yenye wamejifunza na watende kulingana nayo.

NAMNA YA KUFANYA VILE:

  • Saidia wasikilizaji wako wajichunguze. Tumia maulizo yenye haiombe wasikilizaji wajibie kwa sauti juu ya kuwasaidia wachunguze mawazo yao wenyewe.

  • Saidia wasikilizaji wakuwe na nia ya muzuri. Tia moyo wasikilizaji wako wachunguze juu ya nini wanafanyaka matendo ya muzuri. Uwasaidie wakuwe wanafanya mambo juu ya kuchochewa na nia ya muzuri, maana yake kupenda Yehova, kupenda wanadamu wenzao, na kupenda mafundisho ya Biblia. Fikiri na wasikilizaji wako; usiwaambie-ambie tu mambo yenye wanapaswa kufanya ao kuwachambua-chambua. Kuliko kuwapatisha haya ao kuwafanya wajisikie kuwa na kosa, uwaache wakiwa wametiwa moyo ku mwisho ya hotuba yako, wakiwa wamechochewa kufanya ile wanaweza.

  • Saidia wasikilizaji wako wakaze akili yao juu ya Yehova. Onyesha namna mafundisho ya Biblia, kanuni za Biblia, na amri za Biblia zinaonyesha sifa za Mungu na namna anatupenda. Saidia wasikilizaji wako wakuwe wanafikiria kwanza namna Yehova anaona mambo na wakuwe na tamaa ya kumufurahisha.