SOMO LA 20
Umalizio Wenye Matokeo
Mhubiri 12:13, 14
MUHTASARI: Katika maneno yako ya kumalizia, wachochee wasikilizaji wakubali na kutumia mambo waliyojifunza.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
-
Husianisha umalizio na habari yote kwa ujumla. Taja tena au utumie maneno mengine kurudia mambo makuu na mada kuu ya habari yako.
-
Wachochee wasikilizaji. Waonyeshe wasikilizaji wanachohitaji kufanya, na uwape sababu za msingi za kufanya hivyo. Zungumza kwa njia inayoonyesha unasadiki jambo unalosema na kwamba ni muhimu.
-
Umalizio uwe rahisi na mfupi. Usianze kutaja mambo makuu mapya. Ukitumia maneno machache iwezekanavyo, wachochee kwa mara ya mwisho wachukue hatua.