Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Matangazo

Matangazo

KAZI YA KUJITOLEA Kama unataka kujitolea ili kusaidia kufanya kazi kwenye mukusanyiko, tafazali ujulishe ndugu wenye kusimamia Biro ya Wafanyakazi Wenye Kujitolea.

MATUNZO YA KWANZA Tafazali, ukumbuke kwamba biro hii inatoa MATUNZO YA HARAKA TU.

MICHANGO Tumetumia feza mingi ili tupate mahali pazuri pa kufanyia mukusanyiko wetu, vyombo vya muzuri vya sauti na video, na kufanya mambo ingine ili tufurahie mukusanyiko wetu na kutusaidia tumukaribie Yehova zaidi. Michango yenu ya kujipendea inasaidia kulipia mambo hayo yote na kutegemeza kazi yenye kufanywa mu dunia yote. Visanduku vya michango vyenye kuonekana wazi vinapatikana nafasi mbalimbali mahali hapa. Michango yenu yote inaonwa kuwa ya maana sana. Baraza Lenye Kuongoza linawashukuru kwa michango yenye munatoa kwa moyo wote ili kutegemeza faida za Ufalme.

UBATIZO Ikiwa hakuna mabadiliko yoyote, viti vya mbele ya jukwaa vitatayarishwa kwa ajili ya wale wenye watabatizwa. Wale wenye watabatizwa wanapaswa kukaa hapo Siku ya Posho asubui mbele hotuba ya ubatizo ianze. Kila mumoja wao anapaswa kuwa na nguo ya kujipanguza nayo maji na nguo zenye kustahili za kubatizwa nazo.

VITI Tafazali, ufikirie wengine. Kumbuka kama unaweza kuchunga tu viti kwa ajili ya watu wa familia yako, watu wenye umekuja nao katika motokari moja, watu wenye unakaa nao katika nyumba moja, ao watu wenye unajifunza nao Biblia kwa sasa. Tafazali, usitie vitu ku viti vyenye hauchungiane.

VITU VYENYE VILIOKOTWA Kama unaokota kitu fulani na haujue mwenye nacho, tafazali ukipeleke ku Biro ya Vitu Vyenye Viliokotwa. Kama umepoteza kitu fulani, enda ku biro hiyo ili uone kama kimeokotwa. Mutoto mwenye amepotea wazazi wake, anapaswa kupelekwa ku biro hiyo. Lakini, ili kujiepusha na wasiwasi yenye inatokana na kupoteza mutoto, tafazali muchunge watoto wenu na mukae pamoja nao.

WAKARIBISHAJI Ndugu wenye kukaribisha watu wako tayari kukusaidia. Tafazali, uwasikilize na ufuate maagizo yao kuhusu mahali pa kuweka motokari, mahali pa kuingilia na kutokea, ao maagizo kuhusu kuchungia wengine viti, na mambo ingine.

MUKUTANO WA PEKEE

MASOMO KWA AJILI YA WAENEZA-INJILI WA UFALME Mapainia wenye kuwa na miaka 23 mupaka 65 wenye wanafurahia kupanua utumishi wao, wanaalikwa kuhuzuria mukutano wa wale wenye wanataka kufuata Masomo kwa Ajili ya Waeneza-Injili wa Ufalme Siku ya Yenga kisha midi. Saa na mahali kwenye mukutano huo utafanywa vitatangazwa.

Umetayarishwa na Baraza Lenye Kuongoza la Mashahidi wa Yehova