Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 04

Mungu Ni Nani?

Mungu Ni Nani?

Tangu zamani, wanadamu wameabudu miungu mingi. Lakini, Biblia inazungumuzia Mungu mumoja tu mwenye “ni mukubwa kuliko miungu mingine yote.” (2 Mambo ya Nyakati 2:5) Ule Mungu ni nani? Nini njo inafanya akuwe mukubwa kuliko miungu ingine yote yenye watu wanaabudu? Mu hii somo, tutajifunza mambo yenye ule Mungu anapenda tujue juu yake.

1. Jina ya Mungu ni nani, na nini njo inaonyesha kama anapenda tujue jina yake?

Mu Biblia, Mungu anatuambia jina yake. Anasema hivi: “Mimi ni Yehova. Hilo ndilo jina langu.” (Soma Isaya 42:5, 8.) Inaonekana kama jina ya Kiebrania yenye inatafsiriwa “Yehova” inamaanisha “Yeye Anafanya Kuwa.” Yehova anapenda tujue jina yake. (Kutoka 3:15) Nini njo inaonyesha vile? Alifanya jina yake iandikwe mu Biblia zaidi ya mara 7 000! a Jina Yehova ni ya “Mungu wa kweli juu mbinguni na chini duniani.”​—Kumbukumbu la Torati 4:39.

2. Biblia inatuambia mambo gani juu ya Yehova?

Biblia inasema kama wanadamu wako wanaabudu miungu mingi. Lakini, Yehova tu njo Mungu wa kweli. Juu ya nini? Kuko sababu za mingi. Yehova iko na mamlaka yote, na yeye tu njo “Mwenye Kuwa Juu Zaidi, juu ya dunia yote.” (Soma Zaburi 83:18.) Yeye njo “Mweza-Yote,” maana yake yeye njo iko na nguvu ya kufanya kila kitu yenye anapenda. Yeye njo ‘aliumba vitu vyote;’ aliumba ulimwengu na kila kitu yenye iko ku dunia. (Ufunuo 4:8, 11) Tena, Yehova tu njo hana mwanzo, na hatakuwaka na mwisho.​—Zaburi 90:2.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone tofauti kati ya majina ya cheo ya Mungu na jina yake ya pekee. Kisha tuone namna alitujulisha jina yake na juu ya nini alifanya vile.

3. Mungu iko na majina mingi ya cheo, lakini iko na jina moja tu ya pekee

Juu ya kuona tofauti kati ya jina ya cheo ya mutu na jina yake ya pekee, muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Kuko tofauti gani kati ya jina ya cheo, sawa vile “Bwana,” na jina ya pekee?

Biblia inasema kama watu wanaabudu miungu mingi na mabwana wengi. Musome Zaburi 136:1-3, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Nani njo “Mungu wa miungu” na “Bwana wa mabwana”?

4. Yehova anapenda ujue jina yake na uitumikishe

Nini inaonyesha kama Yehova anapenda ujue jina yake? Mungalie VIDEO, na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Unawaza Yehova anapenda watu wajue jina yake? Juu ya nini unasema vile?

Yehova anapenda watu watumikishe jina yake. Musome Waroma 10:13, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Juu ya nini ni muzuri kutumikisha jina ya Mungu, Yehova?

  • Unajisikiaka namna gani wakati mutu anakumbuka jina yako na kukuita mu jina yako?

  • Unawaza Yehova anajisikiaka namna gani wakati unatumikisha jina yake?

5. Yehova anapenda ukuwe rafiki yake

Mwanamuke mumoja wa mu inchi ya Cambodge, mwenye kuitwa Soten, alisema kama kujua jina ya Mungu kulimusaidia ‘ajisikie muzuri zaidi.’ Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, kujua jina ya Mungu kulimusaidia Soten namna gani?

Mbele ukuwe rafiki ya mutu fulani, unatafutaka kwanza kujua jina yake. Musome Yakobo 4:8a, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Yehova anakuomba ufanye nini?

  • Namna gani kujua jina ya Mungu na kuitumikisha kunaweza kukusaidia umukaribie zaidi, ni kusema ukuwe rafiki yake?

WATU FULANI WANASEMAKA: “Kuko Mungu mumoja tu, lakini iko na majina mingi.”

  • Unaamini kama Yehova njo jina ya Mungu?

  • Nini njo inakuonyesha kama Mungu anapenda tutumikishe jina yake?

KWA KIFUPI

Kuko Mungu mumoja tu wa kweli, na jina yake ni Yehova. Anapenda tujue jina yake na tuitumikishe juu tukuwe marafiki wake.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Nini njo inafanya Yehova akuwe tofauti na miungu ingine yote yenye watu wanaabudu?

  • Juu ya nini tunapaswa kutumikisha jina ya Mungu?

  • Nini njo inaonyesha kama Yehova anapenda ukuwe rafiki yake?

Pima kufanya hivi:

HABARI ZINGINE

Ona sababu tano zenye zinatuhakikishia kama Mungu anakuwaka.

“Mungu Anakuwaka?” (Inapatikana ku Enternete)

Ona juu ya nini kuamini kama Mungu hana mwanzo haiko kukosa akili.

“Ni Nani Aliyemuumba Mungu?” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 8, 2014)

Ona juu ya nini tunapaswa kutumikisha jina ya Mungu, hata kama hatujue kabisa-kabisa namna watu walikuwa wanaisema zamani.

“Yehova Ni Nani?” (Inapatikana ku Enternete)

Tunaweza kuita Mungu vile tunapenda? Ona juu ya nini tunaweza kusema kama iko na jina moja tu ya pekee.

“Mungu Iko na Majina Ngapi?” (Inapatikana ku Enternete)

a Juu ya kupata habari zaidi juu ya maana ya jina ya Mungu na juu ya nini haipatikane mu tafsiri fulani za Biblia, ona Nyongeza A4 mu Biblia​—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya.