Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 08

Unaweza Kuwa Rafiki ya Yehova

Unaweza Kuwa Rafiki ya Yehova

Yehova anapenda umujue muzuri. Juu ya nini? Juu anatumaini kama ukijua muzuri sifa zake, namna anatendeaka watu, na maisha yenye anapenda ukuwe nayo, utapenda sana kuwa rafiki yake. Inawezekana kabisa ukuwe rafiki ya Yehova? (Soma Zaburi 25:14.) Unaweza kufanya nini juu ukuwe rafiki yake? Biblia inajibia ile maulizo na inaonyesha kama Yehova njo rafiki muzuri sana.

1. Yehova anakuomba ufanye nini?

‘Umukaribie Mungu, naye atakukaribia.’ (Yakobo 4:8) Maana yake nini? Maana yake Yehova anakuomba ukuwe rafiki yake. Watu fulani wanawazaka kama ni nguvu kuwa rafiki ya Mungu juu hawamuonake. Lakini mu Biblia, Yehova anatuambia sifa zake juu tuweze kumukaribia. Wakati tunasoma mambo yenye anatuambia mu Biblia, urafiki wetu na Yehova unakomala hata kama hatuyamuonaka.

2. Juu ya nini Yehova njo Rafiki muzuri sana?

Hakuna mutu mwenye anakupenda sana sawa vile Yehova. Anapenda ukuwe na furaha. Tena, anapenda ukuwe unazungumuza naye wakati uko na lazima ya musaada. Unaweza ‘kumutupia mahangaiko yako yote, kwa sababu yeye anakuhangaikia.’ (1 Petro 5:7) Kila siku, Yehova iko tayari kusaidia, kutuliza, na kusikiliza marafiki wake.​—Soma Zaburi 94:18, 19.

3. Yehova anapenda tufanye nini juu tukuwe marafiki wake?

Yehova anapendaka watu wote, “lakini anafanya urafiki wa karibu pamoja na watu wanyoofu [ao, wenye kufanya mambo ya muzuri].” (Mezali 3:32) Juu mutu akuwe rafiki ya Yehova, Yehova anapenda ajikaze kufanya mambo ya muzuri na kuepuka mambo ya mubaya. Watu fulani wanawazaka kama hawataweza kufanya mambo yote yenye Yehova anawaomba na kama hawataweza kuepuka mambo ya mubaya. Lakini, Yehova anatuelewaka. Anakubali kila mutu mwenye anamupenda kabisa na mwenye anajikaza sana kumufurahisha.​—Zaburi 147:11; Matendo 10:34, 35.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone mambo yenye unaweza kufanya juu ukuwe rafiki ya Yehova, na tuone juu ya nini Yehova njo Rafiki muzuri sana.

4. Abrahamu alikuwa rafiki ya Yehova

Mu Biblia muko habari ya Abrahamu (mwenye aliitwa pia Abramu). Ile habari inatusaidia kujua mambo yenye tunaweza kufanya juu tukuwe marafiki wa Mungu. Musome habari ya Abrahamu mu Mwanzo 12:1-4. Kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Yehova alimuomba Abrahamu afanye nini?

  • Yehova aliambia Abrahamu kuwa atamufanyia mambo gani?

  • Abrahamu alifanya nini wakati Yehova alimuambia atoke mu inchi yake?

5. Yehova anapenda mutu afanye nini juu akuwe rafiki yake?

Kuko mambo yenye tunapendaka marafiki wetu wafanye.

  • Unapendaka marafiki wako wakufanyie nini?

Musome 1 Yohana 5:3, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Yehova anapenda mutu afanye nini juu akuwe rafiki yake?

Juu tumutii Yehova, pengine itaomba tubadilishe tabia yetu. Musome Isaya 48:17, 18, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini Yehova anaomba mutu mwenye anapenda kuwa rafiki yake atii amri zake?

Rafiki muzuri anatuambiaka mambo yenye inaweza kutusaidia tuepuke hatari na yenye inaweza kutuletea faida. Yehova naye anafanyiaka vile marafiki wake

6. Mambo yenye Yehova anafanyiaka marafiki wake

Yehova anasaidiaka marafiki wake wakati wa magumu. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Vile tumeona mu video, namna gani Yehova alisaidia ule mwanamuke asiendelee kujisikia mubaya?

Musome Isaya 41:10, 13, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Yehova anasema kama atafanyia marafiki wake nini?

  • Unawaza kama Yehova anaweza kuwa Rafiki muzuri? Juu ya nini unawaza vile?

Rafiki muzuri anakusaidiaka wakati uko na lazima ya musaada. Yehova naye atakusaidia

7. Juu tukuwe marafiki wa Yehova, tunapaswa kuzungumuza naye

Kama marafiki wanazoea kuzungumuza, urafiki wao unakuwaka nguvu. Musome Zaburi 86:6, 11, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Namna gani tunaweza kuzungumuza na Yehova?

  • Yehova anazungumuzaka na siye namna gani?

Siye tunazungumuzaka na Yehova kupitia sala; naye anazungumuzaka na siye kupitia Biblia

WATU FULANI WANASEMAKA: “Haiwezekane kuwa rafiki ya Mungu.”

  • Unaweza kutumia andiko gani juu ya kuonyesha kama inawezekana kuwa rafiki ya Mungu?

KWA KIFUPI

Yehova anapenda kuwa Rafiki yako, na atakusaidia juu na weye ukuwe rafiki yake.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Yehova anafanyiaka marafiki wake nini?

  • Juu ya nini Yehova anaambiaka marafiki wake watii amri zake?

  • Unawaza kama Yehova anaombaka marafiki wake wafanye mambo yenye hawataweza? Juu ya nini unasema vile?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona juu ya nini mwanamuke fulani anaona kama kuwa rafiki ya Yehova kuliokoa maisha yake.

“Sikupenda Kufa!” (Munara wa Mulinzi Na. 1 2017)

Sikia namna vijana wanaeleza mawazo yao juu ya Yehova.

Kuwa Rafiki ya Mungu Maana Yake Nini? (1:46)