Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 09

Sala Inaweza Kukusaidia Umukaribie Mungu

Sala Inaweza Kukusaidia Umukaribie Mungu

Kuko wakati unawazaka kama uko na lazima ya mashauri ya kukusaidia? Kuko maulizo yenye unajiulizaka lakini hauyapataka majibu? Uko na lazima ya kitulizo? Unapenda kuwa na urafiki wa sana na Mungu? Sala inaweza kukusaidia. Lakini inaomba kusali namna gani? Mungu anasikilizaka sala zote? Unapaswa kufanya nini juu Mungu asikilize sala zako? Acha tuone.

1. Tunapaswa kusali kwa nani, na juu ya mambo gani?

Yesu alifundisha kama tunapaswa kusali kwa Baba yetu wa mbinguni tu. Yesu naye alikuwa anasali kwa Yehova. Alisema hivi: “Munapaswa kusali hivi: ‘Baba yetu mwenye kuwa mbinguni . . .’” (Matayo 6:9) Wakati tunasali kwa Yehova, tunakuwa na urafiki wa sana pamoja naye.

Tunaweza kusali juu ya kila kitu yenye tunapenda. Lakini, juu Mungu asikie sala yetu, tunapaswa kusali kupatana na mapenzi yake. “Hata kama tunaomba nini kulingana na mapenzi [ya Mungu], yeye anatusikia.” (1 Yohana 5:14) Yesu alionyesha mambo fulani yenye tunaweza kuambia Mungu wakati tunasali. (Soma Matayo 6:9-13.) Tunaweza kuambia Mungu mambo yenye iko inatuhangaisha. Lakini, tusisahau kumushukuru juu ya mambo yenye alishatufanyia. Na tusikose kumuomba asaidie wengine.

2. Tunapaswa kusali namna gani?

Biblia inatuambia tumwange mioyo yetu mbele ya Mungu. (Zaburi 62:8) Njo maana, wakati tunasali, tunapaswa kusema mambo yenye inatoka mu moyo. Tunaweza kusali kwa sauti ao kimya-kimya. Tunaweza kusali na tunasimama, tunaikala, tunapiga magoti, ao mu hali ingine yenye inaonyesha heshima. Tena, tunaweza kusali wakati yoyote na fasi yoyote.

3. Namna gani Mungu anajibiaka sala zetu?

Anafanyaka vile mu njia mbalimbali. Kwa mufano, Yehova ametupatia Neno yake, Biblia. Wakati tunasoma Biblia, tunapata majibu ya maulizo yenye tunajiulizaka. Kusoma Neno ya Mungu kunaweza “[kumufanya] mwenye hana uzoefu akuwe na hekima.” (Zaburi 19:7; soma Yakobo 1:5.) Mungu anaweza kutusaidia tutulie wakati tuko na magumu. Na anaweza kuchochea watumishi wake watusaidie wakati tuko na lazima ya musaada.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone mambo yenye tunaweza kufanya juu Mungu asikilize sala zetu, na namna sala inaweza kutusaidia.

4. Kuko mambo yenye Mungu anapenda tufanye juu asikilize sala zetu

Inaomba tufanye nini juu Mungu asikilize sala zetu? Muangalie VIDEO.

Yehova anapenda tukuwe tunasali kwake. Musome Zaburi 65:2, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Unawaza “Musikiaji wa sala” anapenda ukuwe unasali kwake? Juu ya nini unasema vile?

Kama tunapenda Mungu asikilize sala zetu, tunapaswa kutii sheria zake. Musome Mika 3:4 na 1 Petro 3:12, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Tunapaswa kufanya nini juu Yehova asikilize sala zetu?

Wakati wa vita, watu wa vikundi mbili vyenye kupigana wanaweza kumuomba Mungu awasaidie wapate ushindi. Unawaza Mungu anaweza kabisa kujibia zile sala?

5. Wakati tunasali, tunapaswa kusema mambo yenye inatoka mu moyo

Watu fulani wamefundishwa sala zenye wanapaswa kurudilia-rudilia kila wakati. Lakini, ni vile njo Mungu anapenda tukuwe tunasali kwake? Musome Matayo 6:7, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Wakati unasali, namna gani unaweza kuepuka kusema “mambo yaleyale tena na tena”?

Kila siku, fikiria jambo fulani ya muzuri yenye Mungu amekufanyia, na kisha umushukuru. Ufanye vile kila siku kwa juma moja. Kama unafanya vile, wakati juma itafika ku mwisho, utakuwa ulishasali juu ya mambo saba tofauti-tofauti. Ile itakusaidia usirudilie mambo ileile.

Baba muzuri anapendaka watoto wake wakuwe wanamuambia mambo yenye kutoka mu moyo. Yehova naye anapenda tukuwe tunamuambia mambo yenye kutoka mu moyo

6. Sala ni zawadi yenye Mungu ametupatia

Namna gani sala inaweza kutusaidia, zaidi sana wakati tuko na magumu? Muangalie VIDEO.

Biblia inatuambia kama sala inaweza kutusaidia tutulie. Musome Wafilipi 4:6, 7, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Hata kama sala haimalizake magumu yetu, inatusaidiaka namna gani?

  • Unaweza kupenda kusali juu ya mambo gani?

Unajua?

Neno “amina” maana yake “ikuwe vile” ao “hakika.” Biblia inaonyesha kama tangu zamani, watu wanasemaka “amina” ku mwisho wa sala. ​—1 Mambo ya Nyakati 16:36.

7. Usikuwe unakosa kusali

Wakati fulani tunaweza kuwa na mambo mingi sana ya kufanya mupaka tunasahau kusali. Ni nini inaonyesha kama Yesu aliona sala kuwa jambo ya maana sana? Musome Matayo 14:23 na Marko 1:35, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Yesu alifanya nini juu asikose kusali?

  • Wakati gani njo unaweza kuwa unasali?

WATU FULANI WANASEMAKA: “Kusali ni kupoteza wakati juu hakuna mwenye anasikilizaka.”

  • Mutu akikuambia vile, utamujibia namna gani?

KWA KIFUPI

Sala za kutoka mu moyo zinafanyaka tukuwe na urafiki wa sana pamoja na Yehova, zinatusaidia tutulie, na tukuwe na nguvu ya kumufurahisha Yehova.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Tunapaswa kusali kwa nani?

  • Tunapaswa kusali namna gani?

  • Taya faida fulani za kusali.

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona majibu ya maulizo yenye watu wanazoea kuuliza juu ya sala.

“Mambo 7 Yenye Unapaswa Kujua Juu ya Sala” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 10, 2010)

Ona juu ya nini ni jambo ya maana kusali na namna unaweza kufanya sala zako zikuwe muzuri zaidi.

“Sababu Gani Napaswa Kusali?” (Inapatikana ku Enternete)

Ona mwenye Biblia inasema kama tunapaswa kusali kwake.

“Je, Ninapaswa Kusali kwa Watakatifu?” (Inapatikana ku Enternete)

Mu hii video ya muziki, ona ikiwa kuko wakati wenye tunapaswa kusali ao kama kuko fasi kwenye tunapaswa kuwa juu tusali.

Sali Saa Yote (1:22)