Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 13

Dini za Uongo Zinafanya Watu Wasimupende Mungu

Dini za Uongo Zinafanya Watu Wasimupende Mungu

Mungu ni upendo. Lakini dini za mingi zenye zinasema kama zinamuabudu, zimefanya mambo mingi ya mubaya sana. Juu ya nini? Juu zile dini ni za uongo. Zinafanya watu wasimupende Mungu. Zinafanya vile namna gani? Mungu anazionaka namna gani? Na atazifanya nini?

1. Namna gani mafundisho ya dini za uongo imefanya watu wasimupende Mungu?

Dini za uongo ‘zimebadilisha kweli ya Mungu kwa ajili ya uongo.’ (Waroma 1:25) Kwa mufano, dini za mingi hazifundishake watu jina ya Mungu. Lakini, Biblia inasema kama tunapaswa kutumikisha jina ya Mungu. (Waroma 10:13, 14) Wakati mambo ya mubaya inatokea, viongozi fulani wa dini wanasemaka kama ni mapenzi ya Mungu. Lakini, ile ni uongo. Haiko Mungu njo analetaka mambo ya mubaya. (Soma Yakobo 1:13.) Inahuzunisha kuona kama mafundisho ya dini za uongo, imefanya watu wasimupende Mungu.

2. Namna gani matendo ya dini za uongo imefanya watu wasimupende Mungu?

Yehova anatendeaka watu kwa upendo. Lakini dini za uongo hazionyeshake watu upendo. Biblia inasema kama zambi za dini za uongo zimerundamana mupaka mbinguni. (Ufunuo 18:5) Kwa miaka mingi, dini zimejiingiza mu mambo ya politike, mu mambo ya vita, na zimeuisha watu wengi sana. Viongozi fulani wa dini wanapendaka sana maisha ya raha. Njo maana wanaombaka watu wa mu makanisa yao makuta. Ile matendo yote inaonyesha kama hawamujue Mungu na hawastahili kufundisha watu mambo ya Mungu.​—Soma 1 Yohana 4:8.

3. Mungu anaona namna gani dini za uongo?

Mambo yenye dini za uongo inafanyaka, inakukasirishaka? Kama ni vile, halafu Yehova? Hata kama Yehova anapendaka watu, anakasirikia sana viongozi wa dini za uongo juu wanamuzaraulisha, na wanatendea watu mubaya. Anasema kama dini zote za uongo zitaharibiwa na ‘hazitapatikana tena hata kidogo.’ (Ufunuo 18:21) Siku yenye Mungu ataziharibu iko karibu sana.​—Ufunuo 18:8.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuchunguze zaidi namna Mungu anaona dini za uongo. Tuone mambo ingine yenye zile dini zimefanya, na juu ya nini ile mambo haipaswe kukufanya uache kujifunza juu ya Yehova.

4. Haiko dini zote njo Mungu anakubali

Watu wengi wanaamini kama dini ziko sawa vile barabara za mingi na zote zinapeleka watu kwa Mungu. Ile ni kweli? Musome Matayo 7:13, 14, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Biblia inasema nini juu ya barabara yenye inaongoza kwenye uzima?

Mungalie VIDEO, kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Biblia inasema kama Mungu anakubali dini zote?

5. Dini za uongo hazina upendo

Matendo ya mubaya ya dini za uongo imefanya watu wasimupende Mungu. Kwa mufano, zimejiingiza mu mambo ya vita. Juu ya kuona mufano moja, muangalie VIDEO. Kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Makanisa mingi ilifanya nini wakati ya Vita ya Pili ya Ulimwengu?

  • Unaona namna gani mambo yenye walifanya?

Musome Yohana 13:34, 35 na 17:16. Kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Unawaza Yehova anajisikiaka namna gani wakati dini zinajiingiza mu mambo ya vita?

  • Dini za uongo zimefanya mambo ya mingi sana ya mubaya. Umejionea mambo gani yenye inaonyesha kama dini za uongo hazina upendo?

Dini za uongo hazina upendo

6. Mungu anapenda kusaidia watu watoke mu dini za uongo

Musome Ufunuo 18:4, a na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Mungu anapenda kusaidia watu wenye dini za uongo zimedanganya. Kujua vile kunakufanya ujisikie namna gani?

7. Usiache kujifunza juu ya Yehova

Unapaswa kukatala kujifunza juu ya Mungu juu tu ya mafundisho ya dini za uongo na mambo ya mubaya yenye zinafanyaka? Wazia hii mufano: Mutoto anakatala kutii baba yake, anatoka kwao, na anaanza kufanya mambo ya mubaya sana. Baba hafurahie mambo yenye mutoto wake iko nafanya. Juu ya nini haiko muzuri kusema kama ni kosa ya baba?

  • Sababu gani haiko muzuri kusema kama Yehova njo mwenye kosa na kuacha kujifunza juu yake, juu tu ya matendo ya dini za uongo?

WATU FULANI WANASEMAKA: “Dini zote ziko sawa, hakuna yenye inafundishaka watu mambo ya mubaya.”

  • Na weye unawazaka vile?

  • Hata kama dini za mingi zinasemaka kama zinafundishaka mambo ya muzuri, juu ya nini haiko dini zote njo Mungu anakubali?

KWA KIFUPI

Mafundisho na matendo ya dini za uongo, imefanya watu wasimupende Mungu. Mungu ataharibu dini za uongo.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Unaona namna gani mafundisho ya dini za uongo na mambo ya mubaya yenye zinafanyaka?

  • Yehova anaona namna gani dini za uongo?

  • Mungu atafanya nini dini za uongo?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona ni katika njia gani mbili dini za mingi zinamuchukiza Mungu.

“Dini Zote Ziko Sawa? Zote Zinapelekaka kwa Mungu?” (Inapatikana ku Enternete)

Juu ya nini Yehova anapenda tumuabudu pamoja na watu wengine?

“Ni Lazima Kabisa Kuwa mu Dini Fulani?” (Inapatikana ku Enternete)

Padri fulani alikuwa na mashaka juu ya dini yake, lakini hakuacha kutafuta kweli juu ya Mungu.

“Sababu Iliyofanya Padri Aache Kanisa Lake” (Amuka!, Mwezi wa 2, 2015)

Dini zimefundisha mambo ya uongo juu ya Mungu. Ile imefanya watu wawaze kama Mungu hatuhangaikiake na hana huruma. Ona mifano tatu.

“Mafundisho ya Uongo Ambayo Yanafanya Watu Wasimupende Mungu” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 11, 2013)

a Ili kujua juu ya nini kitabu ya Ufunuo inafananisha dini za uongo na mwanamuke mwenye kuitwa Babiloni Mukubwa, ona Mafasirio Ingine ya 1.