Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 16

Yesu Alifanya Nini Wakati Alikuwa ku Dunia?

Yesu Alifanya Nini Wakati Alikuwa ku Dunia?

Watu wengi wanaonaka Yesu sawa vile mutoto mwenye anatoka tu kuzaliwa, nabii mwenye hekima, ao mutu mwenye alitesekaka sana mbele akufe. Lakini, unawaza kuchunguza maisha ya Yesu ku dunia kunaweza kukusaidia umujue muzuri? Mu hii somo, tutaona mambo ya maana sana yenye Yesu alifanyaka na namna inaweza kutusaidia.

1. Kazi ya maana sana ya Yesu ilikuwa kufanya nini?

Kazi ya maana sana ya Yesu ilikuwa ’kutangaza habari njema ya Ufalme wa Mungu.’ (Soma Luka 4:43.) Alihubiri habari njema yenye ilionyesha kama Mungu atasimamisha Ufalme ao serikali yenye itamaliza magumu yote ya wanadamu. a Yesu alihubiri kwa bidii sana ile habari njema kwa miaka tatu na nusu.​—Matayo 9:35.

2. Juu ya nini Yesu alifanya miujiza?

Biblia inazungumuzia “matendo yenye nguvu na maajabu na alama zenye Mungu alifanya kupitia [Yesu].” (Matendo 2:22) Mungu alipatia Yesu nguvu ya kutuliza upepo mukali, kukulisha watu wengi sana, kuponyesha wagonjwa, na hata kufufua wafu. (Matayo 8:23-27; 14:15-21; Marko 6:56; Luka 7:11-17) Miujiza ya Yesu ilionyesha wazi kama Mungu njo alimutuma. Tena, ilionyesha kama Yehova iko na nguvu ya kumaliza magumu yetu yote.

3. Maisha ya Yesu inaweza kutufundisha nini?

Yesu alimutii Yehova mu mambo yote. Alifanya mambo yote yenye Baba yake alimuomba. (Soma Yohana 8:29.) Alifanya vile maisha yake yote hapa ku dunia hata kama watu wengi walitafuta kumuzuia asimutii Mungu. Maisha yake ilionyesha kama inawezekana wanadamu wamutii Mungu hata kama wanapata magumu ya nguvu sana. Yesu alituachia mufano juu tufuate hatua zake kwa ukaribu.​—1 Petro 2:21.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone namna Yesu alihubiria watu habari njema na kufanya miujiza.

4. Yesu alihubiria watu habari njema

Yesu alikuwa naenda fasi za mbali, mu barabara zenye ziliyala vumbi, juu ya kuhubiria watu wengi sana habari njema. Musome Luka 8:1, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Yesu alikuwa nahubiria tu watu wenye walikuwa nakuya kumusikiliza?

  • Yesu alifanya nini juu apate watu wa kuhubiria?

Mungu alikuwaka alishasema kama Masiya atahubiria watu habari njema. Musome Isaya 61:1, 2, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Yesu alitimiza unabii gani?

  • Unawaza leo watu wako na lazima ya kusikia habari njema?

5. Yesu alifundisha watu mambo ya maana

Zaidi ya kuhubiria watu habari njema juu ya Ufalme wa Mungu, Yesu alifundisha watu mambo ya maana yenye inaweza kuwasaidia. Tuone mambo fulani yenye alifundisha watu mu mahubiri yake ya ku mulima. Musome Matayo 6:14, 34 na 7:12, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Ni mashauri gani yenye iko mu hii andiko yenye Yesu alifundisha watu?

  • Unawaza hii mashauri inaweza kutusaidia leo?

6. Yesu alifanya miujiza

Yehova alipatia Yesu nguvu ya kufanya miujiza ya mingi. Juu ya kuona muujiza fulani wenye alifanyaka, musome Marko 5:25-34 ao muangalie VIDEO. Kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, ule mwanamuke alikuwa hakika na jambo gani?

  • Nini njo inafanya ufurahie sana ile muujiza?

Musome Yohana 5:36, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Miujiza ya Yesu ‘ilitoa ushahidi,’ ao ilionyesha nini juu yake?

Unajua?

Habari za mingi juu ya maisha ya Yesu zinapatikana mu vitabu ine vya Biblia vyenye vinaitwa Injili. Vile vitabu ni Matayo, Marko, Luka, na Yohana. Kila muandikaji wa Injili anaandika habari fulani zenye mwingine hakuandika. Wakati tunasoma Injili zote ine, tunaelewa muzuri kabisa maisha ya Yesu.

  • MATAYO

    njo aliandikaka Injili ya kwanza. Inazungumuzia sana mafundisho ya Yesu, zaidi sana mambo yenye Yesu alifundishaka juu ya Ufalme wa Mungu.

  • MARKO

    njo aliandikaka Injili ya mufupi zaidi. Inayala mambo ya mingi ya kugusa moyo.

  • LUKA

    anazungumuzia zaidi sana sala na namna Yesu alikuwa anatendea wanamuke.

  • YOHANA

    anatuambia mambo mingi yenye Yesu alikuwa anazungumuzia pamoja na marafiki wake wa sana na watu wengine. Ile inatusaidia kuelewa Yesu ni mutu wa namna gani.

WATU FULANI WANASEMAKA: “Yesu alikuwaka tu mutu muzuri, hakuna kitu ingine.”

  • Na weye unawaza nini?

KWA KIFUPI

Yesu alihubiri juu ya Ufalme wa Mungu, alifanya miujiza, na alimutii Yehova mu mambo yote.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Ni kazi gani ya maana yenye Yesu alikuwa anafanya ku dunia?

  • Miujiza ya Yesu inaonyesha nini?

  • Yesu alifundisha mambo gani ya maana?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona juu ya nini tunaweza kuamini kama miujiza ya Yesu ilifanyikaka kabisa.

“Miujiza ya Yesu Inaweza Kukufundisha Nini?” (Munara wa Mulinzi, 15 Mwezi wa 7, 2004)

Ona namna mwanaume fulani alibadilisha maisha yake wakati alijifunza namna Yesu alikuwa anahangaikia watu wengine.

“Nilikuwa Mwenye Kujifikiria Sana Katika Maisha” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 10, 2014)

Ona mambo ya maana yenye Yesu alifanya. Imepangwa kulingana na vile ilifuatana.

“Matukio Makubwa ya Maisha ya Yesu Katika Dunia” (BibliaTafsiri ya Ulimwengu Mupya, Nyongeza A7)

a Mu somo ya 31-33 tutaona mambo mingi zaidi juu ya Ufalme wa Mungu.