Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 18

Namna ya Kutambua Wakristo wa Kweli

Namna ya Kutambua Wakristo wa Kweli

Watu wengi sana wanajiita kuwa Wakristo. Lakini wote hawaamini mambo ileile na hawatii sheria zilezile. Sasa, namna gani unaweza kutambua Wakristo wa kweli?

1. Mukristo njo nani?

Wakristo ni wanafunzi ao wafuasi wa Yesu Kristo. (Soma Matendo 11:26.) Namna gani wanaonyesha kama wao ni wanafunzi wa Yesu? Yesu alisema hivi: “Kama munakaa katika neno langu, ninyi kwa kweli ni wanafunzi wangu.” (Yohana 8:31) Ni kusema, Wakristo wa kweli wanapaswa kutii mafundisho ya Yesu. Mambo yenye Yesu alikuwaka nafundisha ilikuwaka inatoka mu Biblia. Wakristo wa kweli nao wanafundishaka mambo yenye inatoka mu Biblia.​—Soma Luka 24:27.

2. Namna gani Wakristo wa kweli wanaonyeshaka upendo?

Yesu aliambia wanafunzi wake hivi: “Mupendane kama vile niliwapenda ninyi.” (Yohana 15:12) Yesu alikuwa nafanya nini juu ya kuonyesha kama anapenda wanafunzi wake? Alikuwa napitisha wakati pamoja nao, alikuwa nawatia moyo, na alikuwa nawasaidia. Na hata alikubali kufa kwa ajili yao. (1 Yohana 3:16) Vilevile, Wakristo wa kweli hawafundishake tu kama inaomba kupendana. Lakini wanaonyeshaka kwa maneno na matendo yao kama wanapendana.

3. Wakristo wa kweli wako wanafanya kazi gani?

Yesu alipatia wanafunzi wake kazi. ‘Aliwatuma kuhubiri Ufalme wa Mungu.’ (Luka 9:2) Wakristo wa kwanza-kwanza hawakukuwa tu nahubiri fasi za ibada. Lakini walikuwa pia nahubiri fasi zingine kwenye wangeweza kupata watu, na mu manyumba ya watu. (Soma Matendo 5:42; 17:17.) Na leo Wakristo wa kweli wanahubiriaka fasi yote kwenye wanaweza kupata watu. Wanapenda watu. Njo maana wanafurahi kutumia wakati wao na nguvu yao juu ya kuhubiria watu habari yenye iko mu Biblia, yenye inaweza kuwapatia tumaini na kuwatuliza.​—Marko 12:31.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone mambo yenye inaweza kutusaidia kujua wanani njo Wakristo wa kweli na wanani njo hawako Wakristo wa kweli.

4. Wanajikaza kuelewa mafundisho ya Biblia

Wakristo wa kwanza-kwanza walikuwa wanaheshimia Neno ya Mungu

Watu fulani wenye kujiita kuwa Wakristo hawaone kama ni jambo ya maana kujikaza kuelewa mafundisho ya Biblia. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Makanisa fulani yenye inasema kuwa inafuata Kristo imefanya nini juu ya kuzuia watu kujifunza mafundisho ya Yesu?

Yesu alifundisha watu kweli ya Neno ya Mungu. Musome Yohana 18:37, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Yesu alisema kama Wakristo wenye kuwa “upande wa ile kweli” wanafanya nini?

5. Wanahubiria watu kweli ya Biblia

Wakristo wa kwanza-kwanza walikuwa wanahubiria watu

Mbele Yesu apande mbinguni, alipatia wanafunzi wake kazi yenye ingali inaendelea mupaka leo. Musome Matayo 28:19, 20 na Matendo 1:8, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Kazi ya kuhubiri ingefanywa mupaka wakati gani na mupaka wapi?

6. Mambo yenye wanahubiriaka njo yenye wanafanyaka

Nini njo ilifanya mwanaume mwenye kuitwa Tom aamini kabisa kama amepata kweli? Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, nini njo ilifanya Tom aachane kabisa na mambo ya dini?

  • Nini njo ilifanya aamini kama amepata dini ya kweli?

Matendo ya mutu njo inaonyeshaka kama iko mwanafunzi wa kweli wa Yesu, hapana tu maneno. Musome Matayo 7:21, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Nini njo Yesu anaangaliaka sana, maneno ao matendo yetu?

7. Wanapendana

Wakristo wa kwanza-kwanza walikuwa wanapendana

Unajua kama kuko Wakristo wenye walikuwa tayari kufa juu ya Wakristo wenzao? Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, nini njo ilifanya Ndugu Lloyd akuwe tayari kufa kwa ajili ya Ndugu Johansson?

  • Unawaza kama mambo yenye alifanya inaonyesha kama ni Mukristo wa kweli?

Musome Yohana 13:34, 35, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Wanafunzi wa Yesu (Wakristo wa kweli) wanapaswa kutendea namna gani watu wa taifa ao kabila ingine?

  • Wanapaswa kufanya vile namna gani wakati wa vita?

WATU FULANI WANASEMAKA: “Mungu anakubali dini zote.”

  • Unaweza kutumia andiko gani juu ya kusaidia mutu ajue namna ya kutambua Wakristo wa kweli?

KWA KIFUPI

Wakristo wa kweli wanafuata mafundisho ya Biblia, wanaonyesha wengine upendo, na wanafundisha wengine kweli za Biblia.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Wakristo wa kweli wanatoshaka wapi mambo yenye wanafundishaka?

  • Wakristo wa kweli wanaonyeshaka sifa gani?

  • Wakristo wa kweli wanafanyaka kazi gani?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ujifunze mambo mingi zaidi juu ya kikundi ya watu wenye wanajikaza kufuata mafundisho na mufano wa Yesu Kristo.

Mashahidi wa Yehova Ni Watu wa Namna Gani? (1:13)

Ona nini njo ilisaidiaka mwanamuke mwenye alikuwa mutawa mu kanisa Katoliki apate “familia ya duniani pote ya ndugu na dada.”

“Walitumia Biblia ili Kujibu Kila Ulizo!” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 4, 2014)

Ona namna Wakristo wa kweli wanaonyeshaka upendo waabudu wenzao wenye kuwa na lazima ya musaada.

Tunasaidiaka Ndugu Zetu Wakati wa Misiba​—Sehemu (3:57)

Ona mambo yenye kufanana kati ya Wakristo wa leo na Wakristo wa kwanza-kwanza. Yesu alisema kama ile mambo njo ingetambulisha wanafunzi wake.

“Ni Sifa Gani Njo Zinatambulisha Wakristo wa Kweli?” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 3, 2012)