Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 19

Mashahidi wa Yehova Njo Wakristo wa Kweli?

Mashahidi wa Yehova Njo Wakristo wa Kweli?

Tunaamini kama siye Mashahidi wa Yehova njo Wakristo wa kweli. Juu ya nini? Ona kwenye tunatoshaka mambo yenye tunaamini, jina yenye inafanya tukuwe tofauti na wengine, na namna tunapendana.

1. Mashahidi wa Yehova wanatoshaka wapi mafundisho yao?

Yesu alisema hivi: “Neno [la Mungu] ni kweli.” (Yohana 17:17) Sawa vile Yesu, Mashahidi wa Yehova wanatoshaka mafundisho yao yote mu Neno ya Mungu. Fikiria historia yetu: Mu mwaka wa 1870 hivi, kikundi ya watu wenye walikuwa na nia ya muzuri walianza kuchunguza Biblia juu wajue Biblia inafundisha nini kabisa. Waliamini tu mambo yenye inatoka mu Biblia, hata wakati ilipingana na mambo yenye makanisa ilikuwa inafundisha. Kisha wakaanza kuhubiria wengine mambo yenye walikuwa wanavumbula mu Biblia. a

2. Juu ya nini tunajiita kuwa Mashahidi wa Yehova?

Yehova anaita waabudu wake kuwa mashahidi wake juu wanaambiaka wengine kweli juu yake. (Waebrania 11:4–12:1) Kwa mufano, zamani Mungu aliambiaka hivi watu wake: “Muko mashahidi wangu.” (Soma Isaya 43:10.) Biblia inamuita Yesu kuwa “Shahidi Muaminifu.” (Ufunuo 1:5) Njo maana, mu mwaka wa 1931, tulikamata jina Mashahidi wa Yehova. Tunapendaka sana ile jina.

3. Namna gani Mashahidi wa Yehova wanaonyeshaka wengine upendo sawa vile Yesu?

Yesu alikuwa napenda sana wanafunzi wake na alikuwa anawaona sawa vile watu wa familia yake. (Soma Marko 3:35.) Vilevile Mashahidi wa Yehova wako na umoja. Wanafanyiza familia moja mu dunia yote. Njo maana, tunaitanaka ndugu na dada. (Filemoni 1, 2) Tena, tunatii hii amri: “Mupende ushirika muzima wa ndugu.” (1 Petro 2:17) Mashahidi wa Yehova wanaonyeshaka ule upendo mu njia za mingi. Kwa mufano, wanasaidiaka ndugu na dada zao mu dunia yote wakati wa magumu.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tujifunze zaidi historia ya Mashahidi wa Yehova, na tuone mambo ingine yenye kuonyesha kama siye njo Wakristo wa kweli.

Wakristo wa kweli wanatoshaka mambo yenye wanaamini mu Biblia na wanailezeaka wengine

4. Mambo yote yenye tunaamini inatoka mu Biblia

Yehova alisemaka kama tutaendelea kuelewa muzuri zaidi mafundisho ya Biblia. Musome Danieli 12:4 na maelezo ya chini, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Wakati watu wa Mungu wangeendelea kuchunguza Biblia, nini njo ingeendelea kuwa mingi?

Ona namna Charles Russell na wanafunzi wengine wa Biblia, walikuwa wanajifunza Neno ya Mungu. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, Charles Russell na wanafunzi wengine wa Biblia, walikuwa najifunza Biblia namna gani?

Unajua?

Wakati fulani, tumerekebisha mambo yenye tunaamini. Juu ya nini? Sawa vile tunaonaka muzuri zaidi kadiri mwangaza wa jua unaendelea kuongezeka, Mungu anasaidiaka watumishi wake waelewe Biblia pole kwa pole. (Soma Mezali 4:18.) Biblia haibadilikake. Lakini, kadiri tunaelewa muzuri zaidi mambo yenye inafundisha, tunarekebishaka mambo yenye tunaamini.

5. Jina yetu inatufaa

Juu ya nini tulikamata jina Mashahidi wa Yehova? Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Juu ya nini jina Mashahidi wa Yehova inatufaa?

Juu ya nini Yehova amechagua watu juu wakuwe Mashahidi wake? Juu wasaidie watu kujua kama yeye njo Mungu wa kweli, kwa sababu watu wameambiwa mambo mingi ya uongo juu yake. Tuone mambo mbili.

Dini fulani zimefundisha watu kama Mungu anapenda tutumie sanamu mu ibada. Lakini, Musome Mambo ya Walawi 26:1, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Biblia inasema nini hapa? Yehova iko na mawazo gani juu ya sanamu?

Viongozi fulani wa dini wamefundisha watu kama Yesu ni Mungu. Lakini, Musome Yohana 20:17, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Biblia inasema nini hapa? Mungu na Yesu ni mutu mumoja?

  • Kujua kama Yehova ametuma Mashahidi wake juu wasaidie watu kujua kweli juu yake na juu ya Mwana wake, kunafanya ujisikie namna gani?

6. Tunapendana

Biblia inasema kama Wakristo wako sawa vile sehemu za mwili. Musome 1 Wakorinto 12:25, 26, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Wakristo wa kweli wanapaswa kufanya nini wakati Wakristo wenzao wako nateseka?

  • Umejionea nini yenye inaonyesha kama Mashahidi wa Yehova wanapendanaka?

Wakati Mashahidi wa Yehova wa fasi fulani wako nateseka, wenzao wa mu dunia yote, wanatendaka haraka juu ya kuwasaidia. Juu ya kuona mufano, muangalie VIDEO. Kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Mashahidi wa Yehova walikamata mipango gani juu ya kusaidia Wakristo wenzao? Na ile inaonyesha nini?

Wakristo wa kweli wanaonyeshaka upendo wale wenye kuwa na lazima ya musaada

WATU FULANI WANASEMAKA: “Dini ya Mashahidi wa Yehova ni ya hapa juzi-juzi tu.”

  • Ni tangu wakati gani njo Yehova anaitaka watumishi wake kuwa mashahidi?

KWA KIFUPI

Mashahidi wa Yehova njo Wakristo wa kweli. Tuko familia moja mu dunia yote. Mambo yenye tunaamini inatoka mu Biblia, na tunaambiaka wengine kweli juu ya Yehova.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Juu ya nini tulikamata jina Mashahidi wa Yehova?

  • Tunatendeanaka namna gani?

  • Unawaza Mashahidi wa Yehova njo Wakristo wa kweli?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona mufano moja wenye kuonyesha namna Mashahidi wanafunua waziwazi mafundisho ya uongo.

Watu wa Mungu Wanatukuza Jina Yake (7:08)

Ona majibu ya maulizo yenye pengine unajiulizaka juu ya Mashahidi wa Yehova.

“Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana juu ya Mashahidi wa Yehova” (Inapatikana ku Enternete)

Stephen alikuwa anachukia watu wa rangi ingine ya ngozi na alikuwa nawatendea mubaya. Ona mambo yenye ilifanya abadilike.

“Maisha Yangu Yaliendelea Kuwa Mabaya Sana” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 7, 2015)

a Kuanzia mwaka wa 1879, Mashahidi wa Yehova wamechapisha gazeti Munara wa Mulinzi. Ile gazeti inafasiriaka mafundisho ya kweli ya Biblia.