Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 21

Habari Njema Iko Nahubiriwa Namna Gani?

Habari Njema Iko Nahubiriwa Namna Gani?

Yehova atatumia Ufalme wake juu ya kumaliza magumu yetu yote. Siku yenye atafanya vile, inakaribia sana. Yesu alipenda wanafunzi wake waambie watu wengine ile habari! (Matayo 28:19, 20) Mashahidi wa Yehova wanafanyaka nini juu ya kutii ile amri ya Yesu?

1. Namna gani andiko ya Matayo 24:14 iko natimia leo?

Yesu alisemaka hivi: “Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote.” (Matayo 24:14) Mashahidi wa Yehova wanaonaka kazi ya kuhubiri kuwa ya maana sana na wanafurahiaka kuifanya. Tuko nahubiri habari njema mu dunia yote na mu luga zaidi ya 1 000! Kuhubiri mu dunia yote na mu luga za mingi vile, inaomba bidii na kupanga mambo muzuri. Na hatuwezi kuifanya bila musaada wa Yehova.

2. Tunafanyaka nini juu tuweze kuhubiria watu?

Tunahubiriaka fasi yote kwenye tunaweza kupata watu. Wakristo wa kwanza-kwanza walikuwaka nahubiri “nyumba kwa nyumba,” na siye tunafanyaka vile. (Matendo 5:42) Ile inatusaidiaka tuhubirie watu wengi sana kila mwaka. Tena, tunahubiriaka fasi kwenye kunakuwaka watu wengi, sawa vile mu masoko, mu barabara, na fasi za kuchungia magari. Tunafanyaka vile juu haiko kila wakati njo watu wanakuwaka kwao. Kila wakati tunatafutaka namna ya kuambia wengine juu ya Yehova na mambo yenye anapanga kutufanyia.

3. Nani njo anapaswa kufanya kazi ya kuhubiri habari njema?

Wakristo wote wa kweli wanapaswa kuhubiria wengine habari njema. Na tunakamataka ile kazi na mikono mbili. Tunajikazaka sana kuhubiri juu tunajua kama ile habari njema inaweza kuokoa watu. (Soma 1 Timoteo 4:16.) Hatulipiwake. Biblia inasema hivi: “Mulipokea bure, mutoe bure.” (Matayo 10:7, 8) Haiko kila mutu njo anatusikilizaka. Lakini tunaendeleaka tu kuhubiri. Juu ya nini? Juu tunapenda kumutii Yehova na kumufurahisha.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone namna siye Mashahidi wa Yehova tunajikazaka kuhubiri mu dunia yote, na namna Yehova iko natusaidia.

4. Tunajikazaka kuhubiria watu wote

Mashahidi wa Yehova wanajikazaka sana kuhubiria watu habari njema fasi yote. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Mashahidi wa Yehova wanafanyaka mambo mingi sana juu wahubirie wengine. Kati ya ile mambo, ya wapi njo inakushangazaka sana?

Musome Matayo 22:39 na Waroma 10:13-15, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Kazi yetu inaonyesha namna gani kama tunapenda majirani wetu?

  • Yehova anaona namna gani wale wenye wako nahubiria wengine habari njema?​—Ona mustari wa 15.

5. Tuko nafanya kazi pamoja na Mungu

Mambo mingi yenye tulishajionea inaonyesha kama Yehova iko naongoza kazi yetu. Kwa mufano, mu inchi ya Nouvelle-Zélande, ndugu mwenye kuitwa Paul, alikutanaka na mwanamuke fulani wakati alikuwa nahubiri nyumba kwa nyumba mu saa za kisha muchana. Asubui ya ile siku, ule mwanamuke alisali kwa kutumia jina ya Mungu, Yehova. Mu ile sala, aliomba Yehova amutumie mutu wa kumutembelea. Paul anasema hivi: “Kisha saa tatu, nilifika ku mulango yake.”

Musome 1 Wakorinto 3:9, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Namna gani mambo sawa ile yenye ilifanyika mu Nouvelle-Zélande inaonyesha kama Yehova iko naongoza kazi ya kuhubiri?

Musome Matendo 1:8, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini tuko na lazima ya musaada wa Yehova juu tuweze kufanya kazi ya kuhubiri?

Unajua?

Kila juma, ku mukutano wetu wa katikati ya juma, tunajifunzaka namna ya kuhubiri. Kama ulishakafika ku ile mukutano, uliona namna gani mafundisho yenye tunapataka?

6. Tunatii amri ya Mungu ya kuhubiri

Wakati ya mitume, kuko watu wenye walikuwa nakataza wanafunzi wa Yesu kuhubiri. Lakini, wanafunzi walitetea haki yao ya kuhubiri kwa “kuifanya ikubaliwe kisheria.” (Wafilipi 1:7) Na leo Mashahidi wa Yehova wanafanyaka vile. a

Musome Matendo 5:27-42, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

KAMA MUTU ANAULIZA: “Juu ya nini Mashahidi wa Yehova wanahubiriaka nyumba kwa nyumba?”

  • Utamujibia nini?

KWA KIFUPI

Yesu aliambia wanafunzi wake wahubiri habari njema mu mataifa yote. Yehova iko nasaidia watu wake kufanya ile kazi.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Nini njo inaonyesha kama habari njema iko nahubiriwa mu dunia yote?

  • Juu ya nini kazi yetu ya kuhubiri inaonyesha kama tunapenda watu?

  • Unawaza kazi ya kuhubiri inaweza kutuletea furaha? Juu ya nini unasema vile?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona namna Mashahidi wa Yehova wanahubiriaka watu mu miji mikubwa-mikubwa.

Kuhubiri Fasi za Watu Wengi mu Muji Mukubwa wa Paris (5:11)

Mashahidi wa Yehova wamefanya nini juu ya kuhubiria wakimbizi?

Kusaidia Wakimbizi Wamujue Yehova (5:59)

Ujisikilie vile mutu fulani anaeleza namna kutumia maisha yake yote mu kazi ya kuhubiri, kulimuletea furaha.

Nilifanya Muzuri Kuchagula Hii Kazi (6:29)

Ona ushindi mbalimbali wa maana wenye tulipata ku tribinali, wenye ulisaidia kazi yetu ya kuhubiri habari njema iendelee.

“Wahubiri wa Ufalme Wanajitetea Kwenye Tribinali” (Ufalme wa Mungu Unatawala!, sura ya 13)

a Mungu njo anatutuma tuhubiri habari njema. Njo maana siye Mashahidi wa Yehova, hatuna lazima ya ruhusa ya wakubwa wa serikali juu tuhubiri.