Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 22

Unaweza Kufanya Nini Juu Uhubirie Wengine Habari Njema?

Unaweza Kufanya Nini Juu Uhubirie Wengine Habari Njema?

Wakati unaendelea kujifunza mafundisho ya kweli ya Biblia, unaweza kujiambia hivi: ‘Ni muzuri kama kila mutu anajua hii mambo!’ Ni vile kabisa, kila mutu iko na lazima ya kujua ile mambo! Lakini, unaweza kuogopa kuiambia wengine. Tuzungumuzie mambo yenye inaweza kukusaidia usiogope kuhubiria wengine na namna kazi ya kuhubiri inaweza kukuletea furaha.

1. Unaweza kufanya nini juu uambie wengine mambo yenye umejifunza?

Wanafunzi wa Yesu walisema hivi: “Hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo yenye tumeona na kusikia.” (Matendo 4:20) Walifurahia mambo yenye walijifunza. Njo maana walipenda sana kuiambia wengine. Na weye unafurahia mambo yenye uko najifunza? Kama ni vile, ujikaze sana kuiambia watu wa familia yako na marafiki wako, na ufanye vile kwa heshima.​—Soma Wakolosai 4:6.

Unaweza kufanya hivi

  • Saa uko naongea na watu wa familia, anzisha mazungumuzo juu ya habari fulani ya Biblia kwa kusema: “Hii juma nilijifunza jambo fulani ya muzuri.”

  • Saa uko naongea na rafiki mwenye iko mugonjwa ao mwenye iko na mahangaiko, musomee andiko fulani yenye itamutia moyo.

  • Kama wafanyakazi wenzako wanakuuliza juma ilipita namna gani, uwaambie jambo fulani yenye ulijifunza wakati wa funzo ao ku mukutano.

  • Onyesha marafiki wako site ya jw.org.

  • Uombe wengine wajiunge na weye wakati wa funzo, ao uwaonyeshe namna ya kuomba funzo ya Biblia ku jw.org.

2. Juu ya nini ni muzuri ufikirie kuanza kuhubiri na kutaniko?

Wanafunzi wa Yesu hawakuhubiria tu watu wa familia yao na marafiki wao. Yesu ‘aliwatuma wawili-wawili wamutangulie katika kila muji’ juu ya kuhubiri. (Luka 10:1) Ile kazi, ilisaidia watu wengi wasikie habari njema. Tena, wanafunzi walipata furaha wakati walikuwa nahubiri pamoja. (Luka 10:17) Na weye unaweza kufikiria kuanza kuhubiri na kutaniko?

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone mambo yenye inaweza kukusaidia usiogope kuhubiri na namna kazi ya kuhubiri inaweza kukuletea furaha.

3. Yehova atakusaidia

Watu fulani wanapendaka kuhubiri, lakini wanaweza kujiuliza: Wengine wataniona namna gani? Watanisikiliza?

  • Na weye unaogopaka kuambia wengine mambo yenye uko najifunza? Juu ya nini?

Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Nini njo ilisaidia wale vijana waache kuogopa?

Musome Isaya 41:10, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini unapaswa kusali kama unaogopa kuhubiri?

Unajua?

Mashahidi wengi wa Yehova walikuwaka nawaza kama hawatawezaka kuhubiria wengine habari njema. Kwa mufano, Sergey alikuwa najiona kuwa mutu wa bure, na alikuwa na magumu ya kuzungumuza na wengine. Kisha, akaanza kujifunza Biblia. Anasema hivi: “Hata kama nilikuwa naogopa, nilianza kuambia wengine mambo yenye nilikuwa najifunza. Nilishangala kuona kama, kuhubiria wengine kulinisaidia niache kuogopa. Na tena, kulifanya imani yangu ikuwe nguvu.”

4. Ukuwe na heshima

Mbele ya kuhubiria mutu, ufikirie mambo yenye utasema na namna utaisema. Musome 2 Timoteo 2:24 na 1 Petro 3:15, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Hii maandiko, inaweza kukusaidia namna gani wakati uko naambia wengine mambo yenye ulijifunza mu Biblia?

  • Kama watu fulani wa familia yako na marafiki wako hawaitike mambo yenye uko nawaambia, unaweza kufanya nini? Haupaswe kufanya nini?

  • Juu ya nini ni muzuri ukuwe natumia maulizo kuliko kuwakaza waamini mambo yenye weye unaamini?

5. Kuhubiria wengine habari njema kunaletaka furaha

Yehova alipatia Yesu kazi ya kuhubiri habari njema. Yesu aliona ile kazi namna gani? Musome Yohana 4:34, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Kukula chakula ya muzuri, kunatusaidiaka tukuwe na afya ya muzuri na kunatuleteaka furaha. Yesu alisema kama kufanya mapenzi ya Mungu, kwa mufano kuhubiri habari njema, iko sawa vile kukula chakula. Juu ya nini alisema vile?

  • Unawaza kuhubiri habari njema kunaweza kuletea mutu furaha?

Mawazo fulani ya kukusaidia

  • Ku mukutano wa katikati ya juma, tafuta njia zenye na weye unaweza kutumia juu ya kuanzisha mazungumuzo.

  • Ujiandikishe juu na weye ukuwe napitisha vipindi. Ile itakusaidia usikuwe naogopa kuhubiria wengine.

  • Tumia sehemu “Watu Fulani Wanasemaka” ao “Kama Mutu Anauliza” zenye ziko mu hii kitabu, juu uone unaweza kusema nini kama watu wanakuuliza ulizo fulani ao wako na mawazo fulani.

KAMA MUTU ANAULIZA: “Juu ya nini hauonekanake tena?”

  • Namna gani unaweza kutumia ile nafasi juu ya kumuambia mambo fulani yenye umejifunza mu Biblia?

KWA KIFUPI

Kuhubiria wengine habari njema kunaletaka furaha na haiko nguvu kuanza kuhubiri sawa vile pengine unawaza.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Juu ya nini ni muzuri tuhubirie wengine habari njema?

  • Namna gani unaweza kufanya vile kwa heshima?

  • Unaweza kufanya nini juu uache kuogopa kuhubiri?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona njia ine zenye unaweza kutumia juu ya kuhubiria wengine habari njema kwa kutumia karte ya jw.org.

Namna ya Kutolea Mutu Karte ya JW.ORG (1:43)

Ona sifa ine zenye zinaweza kukusaidia uhubirie wengine habari njema.

“Uko Tayari Kuwa Muvuvi wa Watu?” (Munara wa Mulinzi, Mwezi wa 9, 2020)

Ona namna habari fulani ya Biblia inaweza kutusaidia tusiogope kuhubiri habari njema, hata kama tungali watoto.

Yehova Atakusaidia Ukuwe na Ujasiri (11:59)

Ona namna unaweza kuhubiria watu wa familia wenye hawayajifunza juu ya Yehova.

“Namna ya Kugusa Mioyo ya Watu wa Jamaa Wasio Mashahidi” (Munara wa Mulinzi, 15 Mwezi wa 3, 2014)