Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 24

Biblia Inafundisha Nini Juu ya Malaika?

Biblia Inafundisha Nini Juu ya Malaika?

Yehova anapenda tujue familia yake ya mbinguni. Mu ile familia muko malaika. Biblia inawaita “wana wa Mungu.” (Yobu 38:7) Biblia inasema nini juu ya malaika? Wanatendeaka watu namna gani? Wote wako mu familia ya Mungu?

1. Malaika ni nani?

Yehova aliumba malaika mbele aumbe dunia. Hatuwezi kuwaona sawa vile tu hatuwezi kuona Yehova, juu wao pia wako na mwili wa roho. (Waebrania 1:14) Mbinguni kuko mamilioni ya malaika na kila malaika iko na namna yake ya kuwa. (Ufunuo 5:11) Malaika ‘wanashika neno [la Yehova], kwa kutii sauti yake.’ (Zaburi 103:20) Yehova alikuwaka natuma malaika waende kuambia watumishi wake habari fulani, wawasaidie, na kuwaokoa. Leo, malaika wanasaidiaka Wakristo kupata watu wenye wanapenda kumujua Mungu.

2. Shetani na pepo wake wachafu ni nani?

Malaika fulani waliacha kumutii Yehova. Malaika wa kwanza mwenye alifanya vile ‘anaitwa Ibilisi na Shetani, mwenye anapotosha dunia yote.’ (Ufunuo 12:9) Shetani alipenda kutawala wengine. Njo maana, alichochea Adamu na Eva wasimutii Mungu. Na kisha alichochea malaika wengine wasimutii Mungu. Biblia inaita wale malaika wabaya kuwa pepo wachafu. Yehova aliwafukuza mbinguni na kuwatupa ku dunia, na atawaharibu.​—Soma Ufunuo 12:9, 12.

3. Shetani na pepo wachafu wanafanyaka nini juu ya kudanganya watu?

Shetani na pepo wachafu wanatumia uchawi juu ya kudanganya watu. Uchawi ni kuzungumuza na pepo wachafu. Kwa mufano, watu fulani wanatafutaka habari kwa watu wenye kujifunza nyota, wenye kutabiri matukio, wafumu, na wachawi. Wengine wanatafutaka matunzo yenye iko ndani mambo ya uchawi. Tena, Shetani na pepo wachafu wanafanyaka watu waamini kama inawezekana kuzungumuza na wafu. Lakini, Yehova anatuonya hivi: “Musiendee watu wenye kupashana habari na pepo wachafu, na musitafute shauri kwa watu wenye kutabiri matukio.” (Mambo ya Walawi 19:31) Yehova anatuambia vile juu ya kutulinda. Hapendi Shetani na pepo wake wachafu watudanganye. Ni maadui wake, na wanapenda kutufanya mubaya.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone mambo ya muzuri yenye malaika wanafanyaka, hatari ya kuzungumuza na pepo wachafu, na mambo yenye tunaweza kufanya juu Shetani na pepo wake wachafu wasitudanganye.

4. Malaika wanasaidiaka watu wajifunze juu ya Yehova

Malaika hawaendake kutembelea watu juu ya kuwahubiria. Lakini, wanaweza kusaidia watumishi wa Mungu wapate watu wenye wanapenda kujifunza juu ya Mungu. Musome Ufunuo 14:6, 7, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Juu ya nini tuko na lazima ya musaada wa malaika mu kazi ya kuhubiri?

  • Malaika wanaweza kukusaidia upate watu wenye wanapenda kujifunza Biblia. Kujua vile kunakutia moyo? Juu ya nini?

5. Epuka kuzungumuza na pepo wachafu

Shetani na pepo wake wachafu ni maadui wa Yehova. Na ni maadui wetu pia. Musome Luka 9:38-42, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Namna gani pepo wachafu wanatendeaka watu?

Hatupendi kukaribisha pepo wachafu mu maisha yetu. Musome Kumbukumbu la Torati 18:10-12, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Pepo wachafu wanafanyaka nini juu ya kutafuta kutudanganya na kuzungumuza na siye? Kwenye unaishi unaonaka tabia gani za kuzungumuza na pepo wachafu?

  • Yehova anatuomba tuepuke mambo ya uchawi. Unawaza iko na sababu ya muzuri ya kufanya vile? Juu ya nini unasema vile?

Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie hii maulizo.

  • Unawaza kitu yenye Palesa alikuwa navalisha mutoto wake juu ya kumulinda ilikuwa mubaya? Juu ya nini unasema vile?

  • Palesa alipaswa kufanya nini juu pepo wachafu wasimutendee mubaya?

Wakristo wa kweli wanapingaka pepo wachafu. Musome Matendo 19:19 na 1 Wakorinto 10:21, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini inaomba kuharibu kabisa kila kitu yenye iko na uhusiano na mambo ya uchawi?

6. Upinge kabisa Shetani na pepo wake wachafu

Shetani njo anaongoza pepo wachafu. Lakini, Mikaeli, Malaika Mukubwa, ni kusema Yesu, njo anaongoza malaika waaminifu. Unawaza Mikaeli iko na nguvu sana? Musome Ufunuo 12:7-9, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Nani njo iko na nguvu sana, Mikaeli na malaika wake, ao Shetani na pepo wake wachafu?

  • Unawaza wanafunzi wa Yesu wako na sababu ya kuogopa Shetani na pepo wake wachafu?

Unaweza kupinga kabisa Shetani na pepo wake wachafu. Musome Yakobo 4:7, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Unaweza kufanya nini juu Shetani na pepo wake wachafu wasikudanganye?

WATU FULANI WANASEMAKA: “Haiko mubaya kuangalia filme za mambo ya uchawi. Ni kujifurahisha tu.”

  • Juu ya nini ile mawazo haiko ya muzuri?

KWA KIFUPI

Malaika waaminifu wanatusaidiaka. Shetani na pepo wake wachafu ni maadui wa Yehova, na wanatumia mambo ya uchawi juu ya kudanganya watu.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Malaika wa Yehova wanafanyaka nini juu ya kusaidia watu wajifunze juu yake?

  • Shetani na pepo wake wachafu ni nani?

  • Juu ya nini unapenda kuepuka kabisa mambo ya uchawi?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona mambo yenye inaonyesha kama Yesu njo Mikaeli, Malaika Mukubwa.

“Mikaeli, Malaika Mukubwa, Ni Nani?” (Inapatikana ku Enternete)

Ona mambo yenye inaonyesha kama Shetani iko kabisa.

“Je, Shetani Iko Kabisa?” (Inapatikana ku Enternete)

Ona namna mwanamuke fulani aliachanaka na mambo ya uchawi.

“Alipata Kusudi mu Maisha” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 7, 1993)

Ona namna Shetani anatumikishaka mambo ya uchawi juu ya kudanganya watu.

“Ukweli Juu ya Mambo ya Uchawi na Ulozi” (Barabara Yenye Inaongoza Kwenye Uzima wa Milele, sehemu ya 5)