Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 26

Juu ya Nini Kuko Mateso na Mambo Mingi ya Mubaya?

Juu ya Nini Kuko Mateso na Mambo Mingi ya Mubaya?

Wakati jambo fulani ya mubaya inatokea, tunajiulizaka juu ya nini ile jambo ilitokea. Tunafurahi sana juu Biblia inatuonyesha waziwazi juu ya nini mambo ya mubaya inatokeaka!

1. Namna gani Shetani alileta mambo ya mubaya ku dunia?

Shetani Ibilisi alikatala kumutii Mungu. Njo maana alichochea wanadamu wa kwanza, Adamu na Eva, wasimutii Mungu. Alifanya vile wakati alimudanganya Eva. (Mwanzo 3:1-5) Alifanya Eva awaze kama Yehova iko namuficha mambo fulani ya muzuri. Alionyesha kama wanadamu wanaweza kuwa na furaha sana kama hawamutii Mungu. Shetani alisema uongo wa kwanza wakati aliambia Eva kama hatakufa. Njo maana, Biblia inaita Shetani kuwa “muongo na baba ya uongo.”​—Yohana 8:44.

2. Adamu na Eva walifanya nini?

Yehova alipatia Adamu na Eva mambo mingi ya muzuri sana. Aliwaambia wanaweza kula matunda ya kila muti mu bustani ya Edeni. Aliwakataza matunda ya muti moya tu. (Mwanzo 2:15-​17) Lakini waliamua kula matunda ya ile muti yenye Yehova aliwakataza. Eva ‘alianza kukamata matunda ya muti huo na kuyakula.’ Na kisha, Adamu naye “akaanza kuyakula.” (Mwanzo 3:6) Wote wawili hawakumutii Mungu. Juu Adamu na Eva walikuwa wakamilifu, ilikuwa mwepesi kwao kufanya mambo ya muzuri. Lakini wakati waliamua kukosa kumutii Mungu, walifanya zambi na kupinga utawala wa Mungu. Ile iliwaletea mateso mingi sana.​—Mwanzo 3:16-​19.

3. Zambi ya Adamu na Eva ilituletea magumu gani?

Kisha Adamu na Eva kufanya zambi, hawakukuwa tena wakamilifu. Njo maana, watoto wao wote hawako wakamilifu. Biblia inasema hivi: “Kupitia mutu mumoja zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi, na ni vile kifo kilienea kwa watu wote.”​—Waroma 5:12.

Kuko mambo mingi yenye inafanyaka tuteseke. Wakati fulani, tunatesekaka juu tuliamua mambo mubaya. Wakati ingine, tunatesekaka juu wengine waliamua mambo mubaya. Na wakati ingine, tunatesekaka juu tuko fasi ya mubaya, saa ya mubaya.​—Soma Muhubiri 9:11.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone juu ya nini haiko Mungu njo anatuleteaka mateso na mambo ya mubaya sana yenye iko natupata leo, na tuone namna anajisikiaka wakati tuko nateseka.

4. Mwenye anatuleteaka mateso

Watu wengi wanaamini kama Mungu njo anatawala dunia. Unawaza ile ni kweli? Muangalie VIDEO.

Musome Yakobo 1:13 na 1 Yohana 5:19, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Mungu njo anatuleteaka mateso na mambo ya mubaya?

5. Utawala wa Shetani umeleta magumu mingi sana

Musome Mwanzo 3:1-6, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Shetani alisema uongo gani?​—Ona mustari wa 4 na 5.

  • Namna gani Shetani alionyesha kama Yehova iko naficha wanadamu mambo fulani ya muzuri?

  • Shetani alisema nini ili kuonyesha kama wanadamu hawana lazima ya Yehova juu wakuwe na furaha?

Musome Muhubiri 8:9, kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu haiko Yehova njo iko natawala dunia, matokeo imekuwa nini?

  1. Adamu na Eva walikuwa wakamilifu na walikuwa naishi mu paradiso. Lakini, walimusikiliza Shetani na wakakatala kumutii Yehova

  2. Kisha Adamu na Eva kukosa kumutii Mungu, mu dunia muliyala zambi, mateso, na kifo

  3. Yehova atamaliza zambi, mateso, na kifo. Kisha wanadamu watakuwa tena wakamilifu na wataishi mu paradiso

6. Yehova anajisikiaka mubaya wakati tunateseka

Unawaza Yehova anaonaka mateso yetu? Ona mambo yenye Mufalme Daudi na mutume Petro waliandika. Musome Zaburi 31:7 na 1 Petro 5:7, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Kujua kama Yehova anaonaka mateso yetu na kama anatuhangaikiaka kunafanya ujisikie namna gani?

7. Mungu atamaliza mateso yote ya wanadamu

Musome Isaya 65:17 na Ufunuo 21:3, 4, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini inafurahisha kujua kama Yehova atatosha mambo yote ya mubaya yenye inatesa wanadamu?

Unajua?

Wakati Shetani alisema uongo wa kwanza, alimusingizia Yehova. Ni kusema, alifanya watu wawaze mambo ya mubaya juu ya Yehova. Alifanya wawaze kama Yehova ni Mutawala mwenye hana upendo na haki. Wakati Yehova atamaliza mateso yote ya wanadamu, atatakasa jina yake. Ni kusema, atafanya watu wasikuwe tena na ile mawazo juu yake. Ataonyesha kama namna yake ya kutawala njo ya muzuri zaidi. Kutakaswa kwa jina ya Yehova njo jambo ya maana sana kupita mambo yote.​—Matayo 6:9, 10.

WATU FULANI WANASEMAKA: “Mungu anatuleteaka mateso juu ya kutujaribu.”

  • Unaweza kuwajibia namna gani?

KWA KIFUPI

Shetani Ibilisi na Adamu na Eva njo waliletaka mambo ya mubaya mu dunia. Yehova anasikiaka mubaya sana wakati tuko nateseka, na atamaliza mateso.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Shetani aliambia Eva uongo gani?

  • Juu Adamu na Eva hawakumutii Mungu, ile imetuletea magumu gani?

  • Nini njo inaonyesha kama Yehova anasikiaka mubaya wakati tunateseka?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona namna Biblia inafasiria zambi.

“Zambi Ni Nini?” (Inapatikana ku Enternete)

Ujifunze zaidi juu ya mashitaka yenye Shetani alitokezaka mu bustani ya Edeni.

“Sababu Gani Mungu Anaacha Watu Wateseke?” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 1, 2014)

Ona mambo yenye mwanaume fulani alijifunza juu ya mateso yenye alikuwa naona.

Siko Tena Peke Yangu (5:09)