Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 27

Kifo ya Yesu Inaweza Kutuokoa Namna Gani?

Kifo ya Yesu Inaweza Kutuokoa Namna Gani?

Tunafanyaka zambi, tunatesekaka, na tunakufaka juu wazazi wetu wa kwanza, Adamu na Eva, hawakumutii Mungu. a Lakini, kuko tumaini. Yehova amefanya jambo fulani juu ya kutukomboa kutoka mu laana ya zambi na kifo: alituma Mwana wake Yesu Kristo akufe kwa ajili yetu. Biblia inafundisha kama, wakati Yesu alikufa, alitoa bei ya ukombozi. Bei ya ukombozi, ni bei yenye inalipiwaka juu ya kukomboa mutu. Bei yenye Yesu alilipaka ni uzima wake mukamilifu wenye alikuwa nao hapa ku dunia. (Soma Matayo 20:28.) Juu Yesu alikuwa mukamilifu na alikuwa namutii Mungu, angeweza kuishi milele hapa ku dunia. Lakini alikubali kutukufia juu tupate tena mambo yote yenye Adamu na Eva walipotezaka. Tena, ile ilionyesha kama yeye na Yehova, wanatupenda sana. Hii somo itatusaidia tukuwe wenye shukrani sana juu Yesu alitukufiaka.

1. Kifo ya Yesu inaweza kutuletea faida gani leo?

Juu hatukamilike, tunafanyaka mambo ya mingi yenye haimufurahishe Yehova. Lakini, kama tunatubu kabisa zambi zetu, tunaomba Yehova, mu jina ya Yesu, atusamehe, na tunajikaza kabisa juu tusirudilie tena ile makosa, tunaweza kuwa na urafiki wa sana na Mungu. (1 Yohana 2:1) Biblia inasema hivi: “Kristo alikufa mara moja kwa wakati wote kwa ajili ya zambi, mutu mwenye haki kwa ajili ya watu wenye hawako wenye haki, ili awaongoze ninyi kwa Mungu.”​—1 Petro 3:18.

2. Kifo ya Yesu itatuletea faida gani mu siku zenye ziko nakuya?

Yehova alituma Yesu ku dunia juu atoe uzima wake mukamilifu “ili kila mutu mwenye anamuamini asiharibiwe lakini apate uzima wa milele.” (Yohana 3:16) Juu Yesu alitoa uzima wake, Yehova ataweza kumaliza mambo yote ya mubaya yenye zambi ya Adamu imetuletea. Na siku yenye atafanya vile iko karibu sana. Kama tunaonyesha kuwa tunaamini zabihu ya Yesu, na siye tunaweza kuishi milele mu dunia paradiso!​—Isaya 65:21-​23.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuchunguze zaidi juu ya nini Yesu alikubali kufa, na faida yenye kifo yake inatuletea.

3. Kifo ya Yesu inatukomboa kutoka mu zambi na kifo

Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Adamu alipoteza nini wakati alikosa kumutii Mungu?

Musome Waroma 5:12, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Zambi ya Adamu imeleta magumu gani mu maisha yako?

Musome Yohana 3:16, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini Yehova alimutuma Mwana wake hapa ku dunia?

  1. Adamu alikuwa mutu mukamilifu lakini hakumutii Mungu, na ile imeletea wanadamu wote zambi na kifo

  2. Yesu alikuwa mutu mukamilifu na alimutii Mungu, na ile itasaidia wanadamu wakuwe wakamilifu na waishi milele

4. Kifo ya Yesu inaletea watu wote faida

Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Namna gani kifo ya mutu mumoja ingeweza kuletea watu wote faida?

Musome 1 Timoteo 2:5, 6, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Adamu alikuwa mutu mukamilifu, lakini yeye njo aliletea wanadamu wote zambi na kifo. Yesu naye alikuwa mwanadamu mukamilifu. Juu ya nini uzima wenye Yesu alitoa ni “bei ya ukombozi yenye kulingana”?

5. Bei ya ukombozi ni zawadi yenye Yehova amekupatia

Kila rafiki ya Yehova haonake bei ya ukombozi kuwa tu zawadi yenye Yehova alitoa kwa ajili ya watu wote. Lakini anaionaka sawa vile zawadi yenye Yehova amemupatia yeye kabisa. Kwa mufano, musome Wagalatia 2:20, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Paulo alisema nini yenye ilionyesha kama aliona bei ya ukombozi kuwa zawadi yake yenye Yehova alimupatia?

Wakati Adamu alifanya zambi, alijiletea yeye na watoto wake wote hukumu ya kifo. Lakini, Yehova alituma Mwana wake akufe juu uweze kuishi milele.

Wakati munasoma maandiko yenye kufuata, wazia namna Yehova alijisikia wakati aliona Mwana wake iko nateseka. Musome Yohana 19:1-7, 16-​18, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Wakati unafikiria mambo yenye Yehova na Yesu walikufanyia, unajisikia namna gani?

KAMA MUTU ANAULIZA: “Inawezekana kabisa kifo ya mutu mumoja ikomboe watu wote?”

  • Utamujibia nini?

KWA KIFUPI

Juu Yesu alitukufia, Yehova anaweza kutusamehe zambi zetu, na tunaweza kuishi milele.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Juu ya nini Yesu alikufa?

  • Juu ya nini uzima wenye Yesu alitoa ni bei ya ukombozi yenye kulingana?

  • Kifo ya Yesu inaweza kukuletea faida gani?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona juu ya nini uzima mukamilifu wenye Yesu alitoa unaitwa bei ya ukombozi.

“Namna Gani Kifo ya Yesu Ni Zabihu ya Ukombozi kwa Ajili ya Watu Wengi?” (Inapatikana ku Enternete)

Ona mambo yenye tunapaswa kufanya juu tuokolewe.

“Yesu Anatuokoa Namna Gani?” (Inapatikana ku Enternete)

Ona namna kujifunza juu ya zabihu ya Kristo kulisaidia mwanaume fulani kubadilisha namna yake ya kuwa.

“Siko Tena Mutumwa wa Jeuri” (Inapatikana ku Eternete)

a Zambi haiko tu kufanya jambo fulani ya mubaya. Lakini tena, zambi ni hali ya kutokamilika yenye tuliriti.