Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 29

Wafu Wako mu Hali Gani?

Wafu Wako mu Hali Gani?

Ulishakafiwa? Mu ile wakati ya huzuni sana, unaweza kujiuliza: ‘Wakati mutu anakufa, anakuwaka mu hali gani? Kuko siku tutamuonaka tena?’ Mu hii somo na mu somo ya kufuata, tutaona namna Biblia inajibia ile maulizo. Majibu yenye Biblia inatoa, inaweza kututia moyo.

1. Wakati mutu anakufa, anakuwaka mu hali gani?

Yesu alisemaka kama kifo iko sawa vile usingizi. Mutu mwenye analala sana, hajuake mambo yenye iko napitikana pembeni yake. Kifo nayo ni vile. Mutu mwenye alishakufa, hasikiake maumivu. Hata kama alikuwa napenda sana watu wa familia yake na marafiki wake, hawezi kuwakumbuka. Biblia inasema hivi: “Wafu hawajue kitu chochote.”​—Soma Muhubiri 9:5.

2. Kujua kweli juu ya hali ya wafu kunatuletea faida gani?

Watu wengi wanaogopaka kifo, na wanaogopaka hata wafu. Lakini, mambo yenye Biblia inasema juu ya kifo inaweza kukutuliza. Yesu alisema hivi: “Kweli itawaweka ninyi huru.” (Yohana 8:32) Dini za mingi zinafundishaka kama mutu anakuwaka na nafsi ao roho yenye inaendeleaka kuishi kisha mwili kufa. Lakini Biblia haifundishe vile. Hakuna mutu mwenye anatesekaka kisha kufa. Tena, wafu hawajue kitu. Njo maana, hawawezi kututendea mubaya. Kwa hiyo, hatupaswe kuabudu wafu ao kuwafanyia mambo fulani juu ya kuwaza kama, ikiwa hatuwafanyie vile, watakasirika. Na hatupaswe kuwaombea.

Watu fulani wanasemaka kama wanaweza kuzungumuza na wafu. Lakini ile haiwezekane. Sawa vile tumejifunza, wafu “hawajue kitu chochote.” Mutu mwenye anawaza kama iko nazungumuza na mutu mwenye alishakufa, inawezekana iko njo nazungumuza na pepo wachafu, juu pepo wachafu wanajifanya kuwa sawa vile watu wenye walishakufa. Njo maana, kujua kweli juu ya hali ya wafu kunaweza kutulinda juu pepo wachafu wasitudanganye. Yehova anatushauria tusipime kuzungumuza na wafu juu anajua kama wakati tunafanya vile, tuko njo nazungumuza na pepo wachafu. Na wale pepo wachafu wanaweza kututendea mubaya.​—Soma Kumbukumbu la Torati 18:10-​12.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone mambo ingine yenye Biblia inafundisha juu ya hali ya wafu na tuone mambo yenye inahakikisha kama Mungu mwenye upendo hawezi kutesa watu wenye walishakufa.

3. Kweli juu ya hali ya wafu

Mu dunia yote watu wanaamini mambo mbalimbali juu ya hali ya wafu. Lakini haiko ile mambo yote njo ya kweli.

  • Fasi kwenye unaishi watu wanasemaka wafu wako mu hali gani?

Juu ya kuona mambo yenye Biblia inafundisha, muangalie VIDEO.

Musome Muhubiri 3:20, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Vile ile andiko inaonyesha, mutu mwenye alishakufa iko mu hali gani?

  • Mutu anakuwaka na sehemu fulani yenye inaendeleaka kuishi kisha mwili kufa?

Biblia inazungumuzia kifo ya Lazaro, rafiki ya Yesu wa sana. Musome Yohana 11:11-​14. Wakati munasoma ile andiko, angalia mambo yenye Yesu alisema juu ya hali yenye Lazaro alikuwa ndani. Kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Yesu alionyesha kama kifo iko sawa nini?

  • Ile inatufundisha nini juu ya hali ya wafu?

  • Unaona namna gani mafasirio yenye Biblia inatoa juu ya hali ya wafu?

4. Kujua kweli juu ya hali ya wafu kunatuletea faida

Kujua kweli juu ya hali ya wafu kunatusaidia tusikuwe tunaogopa wafu. Musome Muhubiri 9:10, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Wafu wanaweza kututendea mubaya?

Tena, kujua kweli ya Biblia kunatusaidia tusiamini mafundisho yenye kusema kama tunapaswa kuabudu wafu ao kuwafanyia mambo fulani juu wasikasirike. Musome Isaya 8:19 na Ufunuo 4:11, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Unawaza Yehova anajisikiaka namna gani wakati mutu anaabudu ao anatafuta musaada wa mutu mwenye alishakufa?

Kujua kweli juu ya hali ya wafu kunatusaidia tuachane na desturi zenye hazimufurahishe Yehova

5. Kujua kweli juu ya hali ya wafu kunatutuliza

Watu wengi wamefundishwa kama, ikiwa wanakufa, watateseka juu ya mambo ya mubaya yenye walifanyaka zamani. Lakini, inatuliza sana kujua kama hakuna mutu mwenye anatesekaka kisha kufa, hata mutu mwenye alikuwa nafanya mambo ya mubaya sana. Musome Waroma 6:7, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Biblia inasema kama mutu mwenye anakufa, analipia zambi zake zote. Kama ni vile, unawaza mutu mwenye alishakufa iko nateseka juu ya makosa yake ya zamani?

Wakati tunaendelea kumujua Yehova muzuri zaidi, tunafikia kuona kama hawezi hata kidogo kutesa wafu. Musome Kumbukumbu la Torati 32:4 na 1 Yohana 4:8, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Unawaza Mungu mwenye iko na sifa zenye hii maandiko inazungumuzia anaweza kabisa kutesa watu wenye walishakufa?

  • Kujua kweli juu ya hali ya wafu kunatuliza? Juu ya nini?

WATU FULANI WANASEMAKA: “Ninaogopaka mambo yenye itanifikia siku nitakufa.”

  • Kama mutu anasema vile, unaweza kumupatia andiko gani ya kumutuliza?

KWA KIFUPI

Wakati mutu anakufa, maisha yake inaishia pale. Wafu hawatesekake na hawawezi kututendea mubaya.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Wafu wako mu hali gani?

  • Kujua kweli juu ya hali ya wafu kunatuletea faida gani?

  • Juu ya nini kujua kweli juu ya hali ya wafu kunatutuliza?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona namna Biblia inafasiria neno “nafsi.”

“Nafsi Ni Nini?” (Inapatikana ku Enternete)

Ona ikiwa Mungu anatesaka watu wabaya mu moto wa mateso.

Kuko Moto wa Mateso? (3:07)

Ona namna kujifunza kweli juu ya hali ya wafu kulituliza mwanaume fulani.

“Nilifurahia Majibu ya Biblia Yenye Kuwa Wazi, na Yenye Kueleweka” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 2, 2015)