Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 30

Watu wa Familia na Marafiki Wako Wenye Walishakufa Wanaweza Kuishi Tena!

Watu wa Familia na Marafiki Wako Wenye Walishakufa Wanaweza Kuishi Tena!

Kifo inaletaka huzuni sana. Njo maana Biblia inasema kama kifo ni adui. (1 Wakorinto 15:26) Mu Somo ya 27, ulijifunza kama Yehova atatosha kifo. Lakini, mambo itakuwa namna gani juu ya watu wenye walishakufa? Mu hii somo, utajifunza jambo ingine ya muzuri yenye Yehova atafanya: Atafufua watu wengi sana wenye walishakufa juu waishi milele. Ile ni kweli kabisa? Wakati watu watafufuliwa, wataishi mbinguni ao ku dunia?

1. Yehova anapenda kufanyia nini watu wenye walishakufa?

Yehova anapenda sana kufufua watu wenye walishakufa. Yobu, mwanaume mwenye imani, alikuwa hakika kama Mungu hatamusahau wakati atakufa. Aliambia Mungu hivi: “Utaita, na mimi nitakujibu [na niko mu Kaburi].”​—Soma Yobu 14:13-​15.

2. Nini njo inaonyesha kama wafu wanaweza kufufuliwa?

Wakati Yesu alikuwa ku dunia, Mungu alimupatia nguvu ya kufufua wafu. Alifufua mutoto mwanamuke wa miaka 12 na mutoto mwanaume wa mujane. (Marko 5:41, 42; Luka 7:12-​15) Kisha, Lazaro, rafiki ya Yesu, alikufa. Hata kama Lazaro alikuwa alishafanya siku ine mu kaburi, Yesu alimufufua. Yesu alisali kwa Mungu, kisha akasema hivi: “Lazaro, kuja huku inje!” Na “mutu huyo mwenye alikuwa amekufa akatoka inje” na iko muzima! (Yohana 11:43, 44) Wazia namna watu wa familia ya Lazaro na marafiki wake walifurahi sana!

3. Kuko tumaini gani juu ya marafiki na watu wa familia yetu wenye walishakufa?

Biblia inasema hivi: “Kutakuwa ufufuo.” (Matendo 24:15) Wale wenye Yesu alifufuaka hawakukuwaka walishaenda mbinguni. (Yohana 3:13) Walifurahi vile Yesu aliwafufua juu waishi tena ku dunia. Vilevile, Yesu atafufua watu wengi sana juu waishi milele mu dunia paradiso. Alisema kama “wale wote wenye kuwa katika makaburi ya ukumbusho” watafufuliwa. Hata wale wenye inaweza kuonekana kama wamesahauliwa, Mungu angali anawakumbuka na atawafufua.​—Yohana 5:28, 29.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone namna Biblia inaonyesha kama wafu wanaweza kufufuliwa na kama watafufuliwa. Na tuone namna kujua kama wafu watafufuliwa kunaweza kukutuliza na kukupatia tumaini.

4. Yesu alionyesha kama anaweza kufufua wafu

Tuone mambo yenye Yesu alifanyiaka rafiki yake Lazaro. Musome Yohana 11:14, 38-​44, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Nini njo inaonyesha kama Lazaro alikuwa alishakufa kabisa?​—Ona mustari wa 39.

  • Kama Lazaro alikuwaka alishaenda mbinguni, unawaza Yesu angemufufuaka hapa ku dunia?

Muangalie VIDEO.

5. Watu wengi watafufuliwa!

Musome Zaburi 37:29, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Watu wengi sana wenye watafufuliwa wataishi wapi?

Yesu atafufua watu wengine wengi wenye hawakumutumikiaka Yehova. Musome Matendo 24:15, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Utapenda kuona nani wakati wa ufufuo?

Waza kidogo: Ni mwepesi kwa Yesu kufufua mutu sawa vile tu baba anaweza kulamusha mutoto wake mwenye analala

6. Kujua kama wafu watafufuliwa kunaweza kukutuliza na kukupatia tumaini

Habari ya Biblia yenye inaonyesha namna mutoto mwanamuke wa Yairo alifufuliwaka, imetuliza na kutia moyo watu wengi wenye wamefiwa. Musome ile habari ya kweli kabisa mu Luka 8:40-​42, 49-​56.

Mbele Yesu afufue mutoto wa Yairo, aliambiaka hivi baba yake: “Usiogope, ukuwe tu na imani.” (Ona mustari wa 50.) Namna gani tumaini ya ufufuo inaweza kukusaidia . . .

  • wakati unafiwa?

  • wakati maisha yako iko mu hatari?

Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Namna gani tumaini ya ufufuo imetuliza na kutia moyo wazazi wa Phelicity?

WATU FULANI WANASEMAKA: “Siwazie kabisa kama wafu watafufuliwaka.”

  • Na weye unawaza nini?

  • Unaweza kutumia andiko gani juu ya kuonyesha mutu kama kutakuwa ufufuo?

KWA KIFUPI

Biblia inasema kama watu wengi sana wenye walishakufa watafufuliwa. Yehova anapenda waishi tena, na amepatia Yesu nguvu ya kuwafufua.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Nini njo inaonyesha kabisa kama Yehova na Yesu wanapenda kabisa kufufua wafu?

  • Watu wengi sana wenye watafufuliwa wataishi wapi, mbinguni ao ku dunia? Juu ya nini unasema vile?

  • Nini njo inakuhakikishia kama marafiki na watu wa familia yako wenye walishakufa wanaweza kuishi tena?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona mambo fulani yenye inaweza kukusaidia wakati unafiwa.

“Musaada kwa Wale Wenye Wamefiwa na Mupendwa Wao” (Amuka! Na. 3 2018)

Biblia inaweza kabisa kusaidia mutu mwenye amefiwa?

Mambo Yenye Unaweza Kufanya Wakati Unafiwa (5:06)

Namna gani unaweza kusaidia watoto wakati rafiki ao mutu wa familia yao anakufa?

Zabihu ya Ukombozi (2:07)

Kuko wale wenye watafufuliwa juu waende mbinguni? Nani njo hawatafufuliwa?

“Ufufuo Ni Nini?” (Inapatikana ku Enternete)