Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 32

Ufalme wa Mungu Umeanza Kutawala!

Ufalme wa Mungu Umeanza Kutawala!

Ufalme wa Mungu ulianza kutawala mbinguni mwaka wa 1914. Pia, siku za mwisho za utawala wa wanadamu zilianza mwaka huo. Tunajuaje? Tutachunguza mambo ambayo Biblia ilitabiri, hali zinazoendelea ulimwenguni leo, na jinsi ambavyo watu wamekuwa wakitenda tangu mwaka wa 1914.

1. Biblia ilitabiri nini?

Kitabu cha Biblia cha Danieli kinaonyesha kwamba Ufalme wa Mungu ungeanza kutawala mwishoni mwa kipindi kinachoitwa “nyakati saba.” (Danieli 4:16, 17) Karne nyingi baadaye, Yesu alisema kipindi hicho kinaitwa “nyakati zilizowekwa za mataifa,” na alifundisha kwamba bado kilikuwa kinaendelea. (Luka 21:24) Kama tutakavyoona, zile nyakati saba ziliisha mwaka wa 1914.

2. Tangu mwaka wa 1914, hali zimekuwaje na watu wamekuwa wakitendaje?

Wanafunzi wa Yesu walimwuliza hivi: “Ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mfumo wa mambo?” (Mathayo 24:3) Yesu aliwajibu kwa kutabiri mambo mengi ambayo yangetokea wakati ambapo angeanza kutawala mbinguni akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu. Baadhi ya mambo aliyotaja ni vita, upungufu wa chakula, na matetemeko ya ardhi. (Soma Mathayo 24:7.) Pia, Biblia ilitabiri kwamba tabia za watu katika “siku za mwisho” zingefanya hali ziwe “ngumu kushughulika nazo.” (2 Timotheo 3:1-5) Hali na tabia hizo zimeonekana waziwazi hasa tangu mwaka wa 1914.

3. Kwa nini hali zimekuwa mbaya sana tangu Ufalme wa Mungu ulipoanza kutawala?

Muda mfupi baada ya kuwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu, Yesu alipigana vita mbinguni dhidi ya Shetani na roho waovu. Shetani alishindwa katika vita hivyo. Biblia inasema: “[alitupwa] chini duniani, na malaika zake wakatupwa chini pamoja naye.” (Ufunuo 12:9, 10, 12) Shetani ana hasira kali kwa sababu anajua kwamba ataangamizwa. Kwa hiyo, anasababisha maumivu na kuteseka ulimwenguni pote. Ndiyo sababu hali ni mbaya sana ulimwenguni! Ufalme wa Mungu utaondoa matatizo hayo yote.

CHIMBA ZAIDI

Chunguza kwa nini tunaamini kwamba Ufalme wa Mungu ulianza kutawala mwaka wa 1914 na jinsi hilo linavyotuhusu.

4. Mfuatano wa matukio katika Biblia unaongoza kwenye mwaka wa 1914

Mungu alifanya Mfalme Nebukadneza wa jiji la kale la Babiloni aote ndoto ya kinabii. Ndoto hiyo na ufafanuzi wa Danieli unahusu utawala wa Nebukadneza na Ufalme wa Mungu.​—Soma Danieli 4:17. a

Soma Danieli 4:20-26, kisha utumie chati kujibu maswali yanayofuata:

Jinsi Ile Ndoto ya Mti Inavyohusiana na Ufalme wa Mungu

UNABII (Danieli 4:20-36)

Utawala

(A) Mti mkubwa sana

Utawala wakatizwa

(B) “Ukateni na kuuangusha mti” na acheni “nyakati saba zipite”

Utawala warudishwa

(C) “Utarudishiwa tena ufalme wako”

Katika utimizo wa kwanza wa unabii huu . . .

  • (D) Mti ulimwakilisha nani?​—Ona mstari wa 22.

  • (E) Utawala wake ulikatizwa jinsi gani?​—Soma Danieli 4:29-33.

  • (F) Ni nini kilichompata Nebukadneza baada ya “nyakati saba” kwisha?​—Soma Danieli 4:34-36.

UTIMIZO WA KWANZA

Utawala

(D) Nebukadneza, Mfalme wa Babiloni

Utawala wakatizwa

(E) Baada ya mwaka wa 606 K.W.K., Nebukadneza arukwa na akili na anashindwa kutawala kwa miaka saba

Utawala warudishwa

(F) Nebukadneza arudiwa na fahamu na anaanza kutawala tena

Katika utimizo wa pili wa unabii huu . . .

  • (G) Mti huo uliwakilisha nani?​—Soma 1 Mambo ya Nyakati 29:23.

  • (H) Utawala wao ulikatizwaje? Tunajuaje kwamba bado utawala wao ulikuwa umekatizwa Yesu alipokuwa duniani?​—Soma Luka 21:24.

  • (I) Utawala huo ulirudishwa lini na wapi?

UTIMIZO WA PILI

Utawala

(G) Wafalme Waisraeli ambao waliwakilisha utawala wa Mungu

Utawala wakatizwa

(H) Yerusalemu laharibiwa na kukatiza utawala wa wafalme Waisraeli kwa miaka 2,520

Utawala warudishwa

(I) Yesu aanza kutawala mbinguni akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu

Zile nyakati saba zina urefu gani?

Baadhi ya mistari ya Biblia hueleweka kwa kuchunguza mistari mingine ya Biblia. Kwa mfano, kitabu cha Biblia cha Ufunuo kinasema kwamba nyakati tatu na nusu ni sawa na siku 1,260. (Ufunuo 12:6, 14) Nyakati saba ni mara mbili ya nyakati tatu na nusu, yaani, siku 2,520. Nyakati nyingine, Biblia hutumia siku moja kuwakilisha mwaka mmoja. (Ezekieli 4:6) Ndivyo ilivyo kuhusu zile nyakati saba zinazotajwa katika kitabu cha Danieli, zinawakilisha miaka 2,520.

5. Ulimwengu umebadilika tangu mwaka wa 1914

Yesu alitabiri kuhusu hali ambazo zingekuwa ulimwenguni wakati ambapo angeanza kutawala. Soma Luka 21:9-11, kisha mzungumzie swali hili:

  • Umesikia au kujionea nini kati ya mambo hayo yaliyotabiriwa?

Mtume Paulo alifafanua jinsi ambavyo watu wangetenda wakati wa siku za mwisho za utawala wa wanadamu. Soma 2 Timotheo 3:1-5, kisha mzungumzie swali hili:

  • Umejionea watu wakiwa na tabia gani kati ya tabia hizo?

6. Utawala wa Ufalme wa Mungu unapaswa kutuchochea kutenda

Soma Mathayo 24:3, 14, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Ni kazi gani muhimu inayoonyesha kwamba Ufalme wa Mungu unatawala?

  • Unawezaje kushiriki kufanya kazi hiyo?

Sasa Ufalme wa Mungu unatawala, na hivi karibuni utaitawala dunia yote. Soma Waebrania 10:24, 25, kisha mzungumzie swali hili:

  • Kila mmoja wetu anapaswa kufanya nini ‘kadiri tunavyoona siku ile ikikaribia’?

Unapojifunza jambo linaloweza kuwasaidia au kuwaokoa wengine, unapaswa kufanya nini?

HUENDA MTU AKAULIZA: “Kwa nini Mashahidi wa Yehova wanasema mwaka wa 1914 ni muhimu sana?”

  • Wewe ungesemaje?

MUHTASARI

Unabii wa Biblia, mfuatano wa matukio, na hali zilizo ulimwenguni zinathibitisha kwamba sasa Ufalme wa Mungu unatawala. Tunaonyesha kwamba tunaamini hilo kwa kuhubiri kuhusu Ufalme na kuhudhuria mikutano ya kutaniko.

Ungejibuje?

  • Ni nini kilichotokea baada ya nyakati saba zilizotabiriwa katika kitabu cha Biblia cha Danieli?

  • Ni nini kinachokuthibitishia kwamba Ufalme wa Mungu ulianza kutawala mwaka wa 1914?

  • Unaweza kuonyeshaje kwamba unaamini Ufalme wa Mungu unatawala?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Chunguza mambo ambayo wanahistoria na watu wengine husema kuhusu mabadiliko ulimwenguni tangu mwaka wa 1914.

“Maadili Yalipoporomoka Ghafula” (Amkeni!, Aprili 2007)

Soma uone jinsi unabii ulio katika Mathayo 24:14 ulivyobadili maisha ya mwanamume fulani.

“Nilipenda Mchezo wa Besiboli Kuliko Kitu Kingine Chochote!” (Mnara wa Mlinzi, Na. 3 2017)

Ni nini kinachoonyesha kwamba nyakati saba zinazotajwa katika Danieli sura ya 4 ziliisha mwaka wa 1914?

“Ufalme wa Mungu Ulianza Kutawala Lini? (Sehemu ya 2)” (Mnara wa Mlinzi, Novemba 1, 2014)

a Ona  makala mbili za mwisho kwenye sehemu ya Chunguza Zaidi katika somo hili.