Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 32

Ufalme wa Mungu Uko Natawala!

Ufalme wa Mungu Uko Natawala!

Ufalme wa Mungu ulianza kutawala mbinguni mu mwaka wa 1914. Na ni mu ile mwaka njo siku za mwisho za utawala wa wanadamu zilianza. Nini njo inatusaidia kujua vile? Tuchunguze unabii fulani wa Biblia, hali zenye ziko mu dunia tangu mwaka wa 1914, na tabia zenye watu wengi wako nazo tangu ile mwaka.

1. Unabii wa Biblia unaonyesha nini?

Kitabu ya Danieli ilionyesha kama Ufalme wa Mungu ungeanza kutawala ku mwisho wa kipindi yenye Biblia inaita “nyakati saba.” (Danieli 4:16, 17) Miaka mingi kisha pale, Yesu aliita ile kipindi “nyakati zenye ziliwekwa za mataifa,” na alifundisha kama ile kipindi ilikuwa haiyamalizika. (Luka 21:24) Sawa vile tutaona, zile nyakati saba zilimalizika mu mwaka wa 1914.

2. Tangu mwaka wa 1914, hali za dunia zimekuwa namna gani, na watu wamekuwa na tabia gani?

Wanafunzi wa Yesu walimuuliza hivi: “Ni nini itakuwa alama ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mupangilio wa mambo?” (Matayo 24:3) Wakati Yesu aliwajibia, aliwaambia mambo yenye ingetokea wakati angeanza kutawala mbinguni. Alisema kama mu dunia mutakuwa mambo sawa vile vita, njala, na matetemeko ya inchi. (Soma Matayo 24:7.) Tena Biblia ilisema kama tabia zenye watu wangekuwa nazo mu “siku za mwisho” zingefanya maisha ikuwe nguvu kuvumilia. (2 Timoteo 3:1-5) Ile mambo yote iko naonekana sana tangu mwaka wa 1914.

3. Juu ya nini mambo imeharibika sana ku dunia tangu Ufalme wa Mungu uanze kutawala?

Kisha tu Yesu kuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu, alipigana vita na Shetani na pepo wake wachafu kule mbinguni. Alimushinda Shetani. Biblia inasema kama Shetani ‘alitupwa chini katika dunia, na malaika wake wakatupwa chini pamoja naye.’ (Ufunuo 12:9, 10, 12) Shetani iko na kasirani sana juu anajua kama ataharibiwa. Njo maana iko naletea wanadamu mateso mu dunia yote. Ile inatusaidia kuelewa juu ya nini mambo imekuwa mubaya sana ku dunia! Lakini, Ufalme wa Mungu utamaliza mambo yote ya mubaya.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone nini njo inatusaidia kujua kama Ufalme wa Mungu ulianza kutawala mu mwaka wa 1914, na tuone kujua vile kunatuchochea kufanya nini.

4. Unabii wa Biblia unaonyesha kama Ufalme wa Mungu ulianza kutawala mu mwaka wa 1914

Mungu alifanya Nebukadneza, mufalme wa Babiloni ya zamani, alote ndoto yenye ilionyesha mambo yenye ingetokea. Wakati tunasoma ile ndoto na namna Danieli aliifasiria, tunaona wazi kama inazungumuzia utawala wa Nebukadneza na inazungumuzia pia Ufalme wa Mungu.​—Musome Danieli 4:17. a

Musome Danieli 4:20-​26, na kisha mutumie muchoro juu ya kujibia maulizo yenye kufuata:

Uhusiano Kati ya Ndoto ya Nebukadneza na Ufalme wa Mungu

UNABII (Danieli 4:20-36)

Utawala

(A) Muti mukubwa

Utawala unakatizwa

(B) “Mukate muti huu” mupaka “nyakati saba zipite juu yake”

Utawala unarudishwa

(C) “Ufalme wako, utakuwa wako tena”

Mu utimizo wa kwanza wa huu unabii . . .

  • (D) Muti ilifananisha nani? ​—Ona mustari wa 22.

  • (E) Utawala wa Nebukadneza ulikatizwa wakati gani?​—Musome Danieli 4:29-33.

  • (F) Ni mambo gani ilimufikia Nebukadneza ku mwisho wa “nyakati saba”?​—Musome Danieli 4:34-36.

UTIMIZO WA KWANZA

Utawala

(D) Nebukadneza, mufalme wa Babiloni

Utawala unakatizwa

(E) Kisha mwaka wa 606 M.K.Y., Nebukadneza anapoteza akili na haweze tena kutawala kwa miaka saba

Utawala unarudishwa

(F) Akili ya Nebukadneza inamurudilia na anaanza tena kutawala

Mu utimizo wa pili wa huu unabii . . .

  • (G) Muti ilifananisha nani?​—Musome 1 Mambo ya Nyakati 29:23.

  • (H) Utawala wao ulikatizwa wakati gani? Nini njo inatusaidia kujua kama utawala wao ulikuwa ungali unakatizwa wakati Yesu alikuwa ku dunia?​—Musome Luka 21:24.

  • (I) Ule utawala ulirudishwa wakati gani na wapi?

UTIMIZO WA PILI

Utawala

(G) Wafalme Waisraeli wenye waliwakilisha utawala wa Mungu

Utawala unakatizwa

(H) Yerusalemu inaharibiwa, na kwa miaka 2 520 hakuna mufalme yeyote mu Israeli mwenye anatawala

Utawala unarudishwa

(I) Yesu anakuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu, na anaanza kutawala kule mbinguni

Nyakati saba ziko na urefu gani?

Sehemu fulani za Biblia zinatusaidiaka kuelewa sehemu zingine. Kwa mufano, kitabu ya Ufunuo inasema kama nyakati tatu na nusu ni siku 1260. (Ufunuo 12:6, 14) Ni kusema, nyakati saba ni siku 1260 mara mbili ao siku 2520. Wakati fulani, Biblia inatumiaka neno “siku” juu ya kumaanisha mwaka. (Ezekieli 4:6) Ni vile pia kuhusu nyakati saba zenye kitabu ya Danieli inazungumuzia, ziko na urefu wa miaka 2520.

5. Dunia imebadilika tangu mwaka wa 1914

Yesu alionyesha mambo yenye ingetokea mu dunia wakati angeanza kutawala. Musome Luka 21:9-​11, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Kati ya ile mambo, kuko yenye ulishajionea ao kusikia?

Mutume Paulo alionyesha tabia zenye watu wengi wangekuwa nazo mu siku za mwisho za utawala wa wanadamu. Musome 2 Timoteo 3:1-5, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Kati ya zile tabia, kuko yenye unaona watu wako nayo leo?

6. Kujua kama Ufalme wa Mungu uko natawala kunapaswa kutuchochea kufanya jambo fulani

Musome Matayo 24:3, 14, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Ni kazi gani ya maana yenye inaonyesha kama Ufalme wa Mungu uko natawala?

  • Unaweza kufanya nini juu ya kusaidia ku ile kazi?

Ufalme wa Mungu uko natawala, na siku yenye utaanza kutawala dunia yote iko karibu. Musome Waebrania 10:24, 25, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Kadiri “tunaona siku ile kuwa inakaribia,” tunapaswa kufanya nini?

Kama unajua jambo fulani yenye inaweza kusaidia na kuokoa wengine, utafanya nini?

KAMA MUTU ANAULIZA: “Juu ya nini Mashahidi wa Yehova wanazungumuziaka sana mwaka wa 1914?”

  • Utamujibia nini?

KWA KIFUPI

Unabii wa Biblia, na hali zenye ziko mu dunia, zinaonyesha kama Ufalme wa Mungu uko natawala. Tunaonyesha kama tunaamini vile, wakati tunajikaza kuhubiria watu na kufika ku mikutano.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Nini njo ilitokeaka ku mwisho wa nyakati saba zenye kitabu ya Danieli inazungumuzia?

  • Juu ya nini unaamini kama Ufalme wa Mungu ulianza kutawala mu mwaka wa 1914?

  • Unaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama unaamini kama Ufalme wa Mungu uko natawala?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona mambo yenye watu wenye kujifunza historia na watu wengine wamesema juu ya mabadiliko yenye ilitokea mu dunia tangu mwaka wa 1914.

“Wakati Tabia za Watu Ziliharibika Kabisa” (Amuka!, Mwezi wa 4, 2007)

Ona namna unabii wenye kuwa mu Matayo 24:14 ulibadilisha maisha ya mwanaume fulani.

“Nilipenda Besiboli Kuliko Kitu Kingine!” (Munara wa Mulinzi Na. 3 2017)

 Nini njo inatusaidia kujua kama unabii wenye kuwa mu Danieli sura ya 4 unazungumuzia pia Ufalme wa Mungu?

“Ufalme wa Mungu Ulianza Kutawala Wakati Gani? (Sehemu ya 1)” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 10, 2014)

Nini njo inaonyesha kama “nyakati saba” zenye Danieli sura ya 4 inazungumuzia zilimalizika mu mwaka wa 1914?

“Ufalme wa Mungu Ulianza Kutawala Wakati Gani? (Sehemu ya 2)” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 11, 2014)

a Ona  habari mbili za mwisho-mwisho zenye kuwa mu sehemu Habari Zingine mu hii somo.