Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 33

Ufalme wa Mungu Utafanya Nini?

Ufalme wa Mungu Utafanya Nini?

Ufalme wa Mungu ulishaanza kutawala. Mu siku zenye ziko nakuya, utabadilisha mambo ku dunia. Tuone mambo fulani ya muzuri yenye Ufalme wa Mungu utafanya.

1. Ufalme wa Mungu utafanya nini juu ya kurudisha amani na haki ku dunia?

Yesu, Mufalme wa Ufalme wa Mungu, ataharibu watu wabaya na guvernema zote za wanadamu ku vita ya Armagedoni. (Ufunuo 16:14, 16) Ile wakati, hii maneno ya Biblia itakuwa imetimia kabisa: “Kunabakia wakati kidogo tu, waovu hawatakuwa tena.” (Zaburi 37:10) Yesu atatumia Ufalme wa Mungu juu ya kurudisha amani na haki mu dunia yote.​—Soma Isaya 11:4.

2. Maisha itakuwa namna gani wakati mapenzi ya Mungu itafanyika ku dunia?

Wakati Ufalme wa Mungu utatawala dunia, “wenye haki watariti dunia, na wataishi milele juu yake.” (Zaburi 37:29) Wazia unaishi mu dunia yenye hamuna watu wabaya, lakini watu wote wanamupenda Yehova na wanapendana! Hakuna mutu mwenye atagonjwa, na kila mutu ataishi milele.

3. Ufalme wa Mungu utafanya nini kisha watu wabaya kuharibiwa?

Kisha watu wabaya kuharibiwa, Yesu atatawala kwa miaka 1 000. Mu ile miaka, yeye na watawala wenzake 144 000 watasaidia wanadamu wafikie kuwa wakamilifu. Ku mwisho wa ile miaka 1 000, dunia yote itakuwa paradiso ya muzuri. Na watu wote watakuwa na furaha juu watakuwa wanatii sheria za Yehova. Kisha, Yesu atarudishia Baba yake Ufalme. Jina ya Yehova ‘itatakaswa’ mu namna yenye haiyakuwaka. (Matayo 6:9, 10) Itakuwa imeonekana wazi kabisa kama Yehova ni Mutawala muzuri mwenye anahangaikia watu wake. Kisha Yehova ataharibu Shetani, pepo wake wachafu, na wengine wote wenye watakatala utawala wake. (Ufunuo 20:7-​10) Mambo ya muzuri yenye Ufalme wa Mungu utafanya itaendelea milele.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone juu ya nini tunaweza kuamini kama Mungu atatumia Ufalme wake juu ya kutimiza ahadi zake.

4. Ufalme wa Mungu utaharibu guvernema za wanadamu

“Mwanadamu anatawala mwanadamu mwenzake ili kumuumiza.” (Muhubiri 8:9) Yehova atatumia Ufalme wake juu ya kumaliza ukosefu wa haki ku dunia.

Musome Danieli 2:44 na 2 Watesalonike 1:6-8, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Yehova na Yesu, Mwana wake, watafanya nini guvernema za wanadamu na watu wenye kuziunga mukono?

  • Umejifunza mambo gani juu ya Yehova na Yesu yenye inakufanya ukuwe hakika kama watatendea watu kwa haki?

5. Yesu ni Mufalme muzuri sana

Yesu, Mufalme wa Ufalme wa Mungu, atafanya mambo mingi sana juu ya kusaidia watu ku dunia. Muangalie VIDEO juu ya kuona mambo yenye Yesu alishafanya yenye inaonyesha kama iko na nia ya kusaidia watu, na kama Mungu amemupatia nguvu ya kufanya vile.

Mambo yenye Yesu alifanya wakati alikuwa ku dunia, ilionyesha mambo yenye Ufalme wa Mungu utafanya. Hapa chini kuko baraka zenye Ufalme wa Mungu utaletea wanadamu. Ni baraka gani njo unangoya kwa hamu? Musome maandiko yenye inazungumuzia zile baraka.

WAKATI YESU ALIKUWA KU DUNIA . . .

NA IKO MBINGUNI, YESU . . .

  • atasaidia watu wote wakuwe na afya ya muzuri.​—Isaya 33:24.

6. Ufalme wa Mungu utafanya maisha ikuwe muzuri sana ku dunia

Ufalme wa Mungu utarudishia wanadamu maisha yenye Yehova alipendaka wakuwe nayo. Wataishi milele ku dunia paradiso. Muangalie VIDEO juu ya kuona namna Yehova atatumia Yesu, Mwana wake, juu ya kusaidia wanadamu wakuwe na maisha yenye alipendaka wakuwe nayo.

Musome Zaburi 145:16, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Yehova ‘atatimiza tamaa ya kila kitu chenye uzima.’ Kujua vile kunafanya ujisikie namna gani?

WATU FULANI WANASEMAKA: “Kama tunaungana mukono, tunaweza kumaliza magumu mu dunia.”

  • Ufalme wa Mungu utamaliza magumu gani yenye guvernema za wanadamu haziwezi kumaliza?

KWA KIFUPI

Ufalme wa Mungu utafanya mambo yenye Mungu anapenda. Utafanya dunia yote kuwa paradiso, na watu wote mu dunia watamuabudu Yehova milele.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Ufalme wa Mungu utafanya nini juu ya kutakasa jina ya Yehova?

  • Nini njo inatusaidia tuamini kama Ufalme wa Mungu utafanya mambo yote yenye Biblia inasema?

  • Kati ya mambo yote yenye Ufalme wa Mungu utafanya, ya wapi njo uko nangoya kwa hamu?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona mambo yenye itafanyika mu miaka 1000 na ku mwisho wa ile miaka 1000 ya utawala wa Kristo.

“Mambo Gani Njo Itafanyika mu Siku ya Hukumu?” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 9, 2012)

Ona namna watu wanaweza kufikiri pamoja mu familia juu ya baraka zenye Ufalme wa Mungu utaleta.

Ujiwazie mu Paradiso (1:50)

Mu habari “Maulizo Mingi Sana Ilikuwa Nanihangaisha,” ona namna mutu mwenye alikuwa napinga serikali alipata mambo yenye alikuwa natafuta.

“Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 1, 2012)