Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 35

Namna ya Kukamata Maamuzi ya Muzuri

Namna ya Kukamata Maamuzi ya Muzuri

Siye wote tunakamataka maamuzi. Maamuzi ya mingi yenye tunakamataka inaweza kutuletea faida ao kutuletea magumu. Tena, inaweza kufanya urafiki wetu pamoja na Yehova ukuwe muzuri ao uharibike. Kwa mufano, tunaweza kuamua tutaishi wapi, tutafanya kazi gani juu tupate makuta, ao kama tutaoa ao kuolewa, ao tutabakia bila kuoa ao kuoelewa. Wakati tunakamata maamuzi ya muzuri, tunakuwa na furaha mu maisha yetu na tunamufurahisha Yehova.

1. Namna gani Biblia inaweza kukusaidia kukamata maamuzi ya muzuri?

Mbele ya kukamata uamuzi, umuombe Yehova akusaidie na uchunguze Biblia ili uone mawazo yake juu ya uamuzi wenye unataka kamata. (Soma Mezali 2:3-6.) Wakati fulani, sheria ya Yehova inaonyeshaka waziwazi mambo ya kufanya. Kama ni vile, uamuzi wa muzuri ni kutii ile sheria.

Sasa, utafanya nini kama mu Biblia hamuna sheria yenye inaonyesha waziwazi mambo yenye unapaswa kufanya? Mu ile hali, Yehova atakuonyesha “njia yenye unapaswa kutembea ndani yake.” (Isaya 48:17) Atafanya vile namna gani? Mu Biblia muko kanuni zenye zinaweza kukuongoza. Kanuni ni kweli za musingi zenye zinatusaidia kujua mawazo ya Mungu na namna anajisikiaka. Mara mingi tunajuaka mawazo ya Mungu juu ya jambo fulani kisha kusoma habari fulani mu Biblia. Kisha kujua mawazo ya Yehova, tunaweza kukamata uamuzi wenye utamufurahisha.

2. Unapaswa kufikiria mambo gani mbele ya kukamata uamuzi?

Biblia inasema hivi: “Mwerevu anafikiria sana kila hatua.” (Mezali 14:15) Ni kusema, mbele ya kukamata uamuzi, tunapaswa kuwaza sana. Wakati uko nafikiria uamuzi wenye utakamata, ujiulize hivi: ‘Ni kanuni gani za Biblia zinaweza kunisaidia? Kama ninaamua hivi, nitakuwa na amani ya akili? Nitaletea wengine magumu ao hapana? Na ulizo ya maana sana ya kujiuliza ni hii: Kama ninaamua hivi, Yehova atafurahi?’​—Kumbukumbu la Torati 32:29.

Yehova iko na haki ya kutuambia mambo gani njo ya muzuri na mambo gani njo ya mubaya. Wakati tunaelewa muzuri sheria na kanuni za Yehova na tunajikaza kuzifuata, tunasaidia zamiri yetu ikuwe natumika muzuri. Zamiri, njo ile sauti ya ndani, yenye inatuambiaka ikiwa jambo fulani ni ya muzuri ao ni ya mubaya. (Waroma 2:14, 15) Zamiri yenye iko natumika muzuri itatusaidia tukamate maamuzi ya muzuri.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone namna kanuni za Biblia na zamiri yetu inatusaidiaka kukamata maamuzi ya muzuri.

3. Acha Biblia ikuongoze

Namna gani kanuni za Biblia zinaweza kutusaidia tukamate maamuzi ya muzuri? Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Uhuru wa kuchagula ni nini?

  • Juu ya nini Yehova alitupatia uhuru wa kuchagula?

  • Yehova ametupatia nini juu ya kutusaidia tutumie muzuri uhuru wetu wa kuchagula?

Juu ya kuona kanuni moja ya Biblia, musome Waefeso 5:15, 16. Kisha muzungumuzie namna unaweza “kutumia muzuri zaidi wakati wako” . . .

  • juu ya kusoma Biblia kila siku.

  • juu ya kuwa bibi ao bwana muzuri zaidi, muzazi muzuri zaidi, ao mutoto muzuri zaidi.

  • juu ya kuenda ku mikutano.

4. Zoeza zamiri yako juu ikusaidie kuamua muzuri

Wakati kuko sheria ya Biblia yenye kuwa wazi, ni mwepesi kuamua muzuri. Halafu kama hakuna sheria ya vile? Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, ule dada alifanya nini juu azoeze zamiri yake na akamate uamuzi wenye ungemufurahisha Yehova?

Juu ya nini hatupaswe kuomba wengine watukamatie maamuzi? Musome Waebrania 5:14, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Hata kama inaweza kuwa mwepesi kuomba wengine watukamatie maamuzi, siye peke tunapaswa kuwa na uwezo wa kufanya tofauti gani?

  • Tuko na mambo gani yenye inaweza kutusaidia tuzoeze zamiri yetu na tukamate maamuzi ya muzuri?

Sawa vile karte inatusaidiaka kujua njia, zamiri yetu inatusaidiaka kukamata maamuzi ya muzuri mu maisha

5. Heshimia zamiri ya wengine

Siye wote hatukamatake maamuzi ileile. Tunaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama tunaheshimia zamiri za wengine? Tuone hali mbili:

Hali ya 1: Dada mwenye anapendaka kujipodoa, anahamia mu kutaniko yenye dada wengi hawafurahiake wakati wanaona mutu mwenye alishajipodoa.

Musome Waroma 15:1 na 1 Wakorinto 10:23, 24, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Kwa kufikiria ile maandiko, ule dada anaweza kuamua kufanya nini? Utafanya nini kama uko na mutu mwenye zamiri yake inamukataza kufanya mambo yenye zamiri yako haikukataze?

Hali ya 2: Ndugu fulani anajua kama Biblia haikataze kukunywa pombe kwa kiasi, lakini yeye anaamua kama hatakuwa nakunywa pombe. Halafu wanamualika fasi fulani, na kule anaona ndugu na dada wako nakunywa pombe.

Musome Muhubiri 7:16 na Waroma 14:1, 10, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Kwa kufikiria ile maandiko, ule ndugu anaweza kuamua kufanya nini? Utafanya nini kama unaona mutu mwingine iko nafanya jambo fulani yenye zamiri yako inakukataza?

 Mambo ya kukusaidia ukamate maamuzi ya muzuri

1. Umuombe Yehova akusaidie ujue jambo ya kufanya.​—Yakobo 1:5.

2. Utafute mu Biblia na mu vichapo vyetu kanuni za kukusaidia. Unaweza pia kuomba mashauri Wakristo wenye wamemutumikia Yehova kwa miaka mingi.

3. Ujiulize ikiwa uamuzi wako utakusaidia ukuwe na zamiri ya muzuri ao hapana na ikiwa utakwaza wengine ao hapana.

WATU FULANI WANASEMAKA: “Mambo yenye ninaamua kufanya, haiangalie mutu. Niko na haki ya kufanya mambo yenye ninapenda.”

  • Juu ya nini tunapaswa kufikiria namna Yehova ataona uamuzi wetu na namna wengine wataona uamuzi wetu?

KWA KIFUPI

Juu tukamate maamuzi ya muzuri, tunapaswa kutafuta kujua mawazo ya Yehova juu ya uamuzi wenye tunataka kamata, na kutafuta kujua ikiwa matendo yetu itasaidia wengine ao itawaletea magumu.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Nini njo itakusaidia ukamate maamuzi yenye inamufurahisha Yehova?

  • Unaweza kufanya nini juu ya kuzoeza zamiri yako?

  • Namna gani unaweza kuonyesha kama unaheshimia zamiri ya wengine?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Namna gani unaweza kukamata maamuzi yenye itakusaidia ukuwe na urafiki wa sana pamoja na Mungu?

“Kamata Maamuzi Yenye Inamutukuza Yehova” (Munara wa Mulinzi, 15 Mwezi wa 4, 2011)

Ona namna Yehova anatupatiaka mashauri.

Yehova Anaongoza Watu Wake (9:50)

Ona mambo yenye ilisaidia mwanaume fulani akamate uamuzi wa nguvu.

Yehova Anatutakiaka Tu Mambo ya Muzuri (5:46)

Ona namna tunaweza kumufurahisha Yehova wakati hatuna sheria yenye inaonyesha waziwazi mambo ya kufanya.

“Uko na Lazima ya Amri ya Biblia mu Kila Hali?” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 12, 2003)