Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 40

Tunaweza Kufanya Nini Juu Tukuwe Safi mu Macho ya Mungu?

Tunaweza Kufanya Nini Juu Tukuwe Safi mu Macho ya Mungu?

Wazia mambo yenye mama mwenye upendo anafanyaka wakati iko natayarisha mutoto wake mbele aende ku masomo. Anamunawishaka na kumuvalisha manguo ya kutakata. Ile inafanyaka ule mutoto aendelee kuwa na afya ya muzuri, na inafanyaka wengine waone kama wazazi wake wako namuhangaikia muzuri. Vilevile, Yehova, Baba yetu mwenye upendo, anapenda tukuwe safi, ni kusema anapenda mwili yetu ikuwe safi, na pia mawazo yetu, maneno yetu, na matendo yetu. Wakati tuko safi, ile inatuletea faida na inamutukuza Yehova.

1. Tunaweza kufanya nini juu mwili yetu iendelee kuwa safi na pia vitu vyetu?

Yehova anatuambia hivi: “Munapaswa kuwa watakatifu.” (1 Petro 1:16) Juu tukuwe watakatifu, tunapaswa kujikaza juu mwili yetu, vitu vyetu, maneno yetu, matendo yetu, na mawazo yetu ikuwe safi. Tunapaswa kunawa kila siku na kujikaza juu nyumba yetu, manguo yetu, na gari yetu iendelee kuwa safi. Tunaweza pia kusaidia kusafisha Jumba ya Ufalme. Wakati tunajikaza juu mwili yetu na vitu vyetu viendelee kuwa safi, tunamutukuza Yehova.​—2 Wakorinto 6:3, 4.

2. Juu tukuwe safi, tunapaswa kuepuka tabia gani?

Biblia inatushauria “tujisafishe kila uchafu wa mwili na roho.” (2 Wakorinto 7:1) Ni kusema, tunapaswa kuepuka kila kitu yenye inaweza kuchafua mwili na akili yetu. Mawazo yetu inapaswa kumufurahisha Yehova, njo maana tunapaswa kuepuka mawazo machafu. (Zaburi 104:34) Tena tunapaswa kuepuka maneno machafu.​—Soma Wakolosai 3:8.

Ni mambo gani ingine yenye inaweza kufanya tusikuwe safi? Kuko vitu fulani vyenye vinaweza kuchafua mwili yetu. Tunapaswa kuepuka mambo sawa vile kuvuta tumbako ao bangi, na kutafuna miraa. Na hatupaswe kutumia dawa za kulewesha juu tu ya kujifurahisha. Kama tunaepuka ile mambo, tutakuwa na afya ya muzuri na tutaonyesha kama tunaheshimia uzima. Tunapaswa pia kuepuka tabia za mubaya sawa vile kugusa-gusa viungo vya uzazi juu ya kujitimizia tamaa ya ngono na kuangalia pornografia. (Zaburi 119:37; Waefeso 5:5) Inaweza kuwa nguvu kuachana na zile tabia, lakini Yehova anaweza kutusaidia.​—Soma Isaya 41:13.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone juu ya nini tunamutukuza Yehova wakati tuko safi, na namna tunaweza kuachana na tabia chafu.

3. Tunamutukuza Yehova wakati tuko safi

Sheria zenye Yehova alipatia Waisraeli, zinatusaidia kuona kama Yehova anapenda watu wake wakuwe safi. Musome Kutoka 19:10 na 30:17-19, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Ile maandiko inasema nini yenye inaonyesha kama Yehova anaona usafi kuwa wa maana?

  • Unapaswa kuzoea kufanya nini juu uendelee kuwa safi?

Inaomba wakati na kujikaza juu tuendelee kuwa safi. Ikuwe tuko matajiri, maskini, ao tunaishi wapi, tunaweza kuwa safi. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Juu ya nini watu wataheshimia zaidi kazi yetu ya kuhubiri kama vitu vyetu viko safi?

4. Achana na tabia za mubaya

Yehova anaweza kutusaidia tuachane na tabia ya mubaya, hata ikuwe tabia gani

Haikuwake mwepesi kuacha kuvuta tumbako ao kutumia dawa za kulewesha. Nini njo inaweza kusaidia? Kufikiria matokeo ya mubaya ya zile tabia. Musome Matayo 22:37-39, na kisha muzungumuzie namna kuvuta tumbako ao kutumia mubaya dawa za kulewesha kunaweza . . .

  • kuharibisha urafiki wa mutu pamoja na Yehova.

  • kuumiza watu wa familia na watu wengine.

Fikiria mambo yenye utafanya juu uachane na tabia ya mubaya. a Muangalie VIDEO.

Musome Wafilipi 4:13, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini kama mutu anazoea kusali, kujifunza Biblia, na kufika ku mikutano, anaweza kupata nguvu ya kuachana na tabia ya mubaya?

5. Ujikaze kuachana na mawazo, na matendo machafu

Musome Wakolosai 3:5, kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Nini njo inaonyesha kama kuangalia pornografia, kutumiana sexto, na kujigusa-gusa viungo vya uzazi juu ya kujitimizia tamaa ya ngono ni matendo machafu mu macho ya Yehova?

  • Unawaza Yehova iko na haki ya kutuomba tuepuke matendo machafu? Juu ya nini?

Tuone namna tunaweza kuachana na mawazo machafu. Muangalie VIDEO.

Yesu alitoa mufano juu ya kuonyesha kama tunapaswa kujikaza sana ili tuendelee kuwa safi. Musome Matayo 5:29, 30, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Yesu hakupenda kusema kama tunapaswa kujilumiza, lakini alipenda kuonyesha kama tunapaswa kufanya yetu yote juu ya kuachana na mawazo machafu. Mutu anaweza kufanya nini juu aachane kabisa na mawazo machafu? b

Yehova iko naona vile uko najikaza kuachana na mawazo machafu. Musome Zaburi 103:13, 14, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Kama uko najikaza kuachana na tabia fulani chafu, namna gani ile andiko inakutia moyo usichoke?

Kama unaanguka, simama!

Ni mwepesi kusema hivi: ‘Nimeshindwa, hata nipime tena, sitawezaka.’ Waza kidogo: Kama mukimbiaji anakwala na anaanguka, ile haimaanishe kama ameshindwa, na haimaanishe kama anapaswa kurudia nyuma na kuanza tena. Vilevile, kama unarudilia tabia fulani ya zamani yenye uko najikaza kuacha, ile haimaanishe kama umeshindwa na haimaanishe kama maendeleo yote yenye ulishafanya ni ya bure. Mutu anaangukaka, maisha ni vile. Lakini usichoke! Yehova atakusaidia uachane na tabia ya mubaya.

WATU FULANI WANASEMAKA: “Hii tabia ilishakaniingia mu damu. Sitaweza kuiacha.”

  • Unaweza kutumia andiko gani juu ya kusaidia mutu aone kama Yehova anaweza kumusaidia aachane na tabia ya mubaya?

KWA KIFUPI

Tunamufurahisha Yehova wakati tunajikaza juu mwili yetu, akili yetu, na mwenendo wetu uendelee kuwa safi.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Juu ya nini ni jambo ya maana sana tuendelee kuwa safi?

  • Unaweza kufanya nini juu mwili yako na vitu vyako viendelee kuwa safi?

  • Unaweza kufanya nini juu uendelee kuwa na mawazo na mwenendo safi?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Unaweza kufanya mambo gani juu uendelee kuwa safi hata kama uko maskini?

Afya na Usafi​—Kunawa Mikono (3:01)

Ona mambo yenye unaweza kufanya juu uache kuvuta tumbako.

“Mambo ya Kukusaidia Uache Kuvuta Tumbako” (Amuka!, Mwezi wa 5, 2010)

Ona mambo yenye ilisaidia mwanaume fulani aachane na tabia ya kuangalia pornografia.

“Nilifikia Kuweza Kisha Kushindwa Mara Nyingi” (Munara wa Mulinzi Na. 4 2016)

a Habari “Mambo ya Kukusaidia Uache Kuvuta Tumbako,” yenye kuwa mu sehemu Habari Zingine mu hii somo, inaonyesha mambo yenye mutu anaweza kufanya juu aachane na tumbako.

b Ili kujua mambo yenye inaweza kusaidia mutu aachane na tabia ya kugusa-gusa viungo vya uzazi juu ya kujitimizia tamaa ya ngono, ona habari yenye kichwa “Namna Gani Ninaweza Kuachana na Tabia ya Kugusa-gusa Viungo vya Uzazi Juu ya Kujitimizia Tamaa ya Ngono?” mu kitabu Maulizo Yenye Vijana Wanajiulizaka​—Majibu ya Kuwasaidia, Buku ya 1, sura ya 25.