Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 41

Biblia Inasema Nini Juu ya Ngono?

Biblia Inasema Nini Juu ya Ngono?

Watu wengi wanasikiaka haya ya kuzungumuzia ngono. Lakini, wakati Biblia inazungumuzia ngono, inaizungumuzia waziwazi na mu njia ya heshima. Mambo yenye Biblia inasema iko na faida. Ile haitushangaze juu Yehova njo alituumbaka. Anajua mambo yenye inaweza kutuletea faida. Anatuonyesha mambo yenye tunaweza kufanya juu tumufurahishe, na mambo yenye inaweza kutusaidia tufurahie maisha milele.

1. Yehova iko na mawazo gani juu ya ngono?

Ngono ni zawadi yenye Yehova amepatia wanadamu. Anapenda mwanamuke na mwanaume wenye wameoana njo waifurahie. Ngono inasaidia bibi na bwana wazale watoto na waonyeshane upendo mu njia ya asili na yenye kufurahisha. Njo maana Biblia inasema hivi: “Ufurahi pamoja na bibi wa ujana wako.” (Mezali 5:18, 19) Yehova anapenda bibi Mukristo akuwe muaminifu kwa bwana yake, na bwana Mukristo akuwe muaminifu kwa bibi yake. Hawapaswe hata kidogo kufanya uzinifu.​—Soma Waebrania 13:4.

2. Uasherati ni nini?

Biblia inasema kama “waasherati . . . hawatariti Ufalme wa Mungu.” (1 Wakorinto 6:9, 10) Wale wenye waliandikaka sehemu fulani za Biblia mu Kigiriki, walitumiaka neno por·neiʹa juu ya kuzungumuzia uasherati. Ile neno inamaanisha (1) ngono a kati ya watu wenye hawayaoana, (2) ngono kati ya wanaume na wanaume na wanamuke na wanamuke (3) na ngono kati ya watu na wanyama. Tunamufurahisha Yehova na tunapata faida wakati ‘tunajiepusha na uasherati.’​—1 Watesalonike 4:3.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone mambo yenye itakusaidia uepuke uasherati na faida yenye utapata kama unafanya vile.

3. Kimbia uasherati

Yosefu alikatala kabisa wakati mwanamuke fulani alipenda kufanya ngono naye. Musome Mwanzo 39:1-12, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Juu ya nini Yosefu alikimbia?​—Ona mustari wa 9.

  • Unawaza Yosefu alifanyaka muzuri kukimbia? Juu ya nini?

Namna gani vijana wa leo wanaweza kufuata mufano wa Yosefu na kukimbia uasherati? Muangalie VIDEO.

Yehova anapenda tuepuke kabisa uasherati. Musome 1 Wakorinto 6:18, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Ni hali gani zinaweza kufanya mutu afikie kufanya uasherati?

  • Unaweza kufanya nini juu ukimbie uasherati?

4. Unaweza kushinda jaribu

Kama unajaribiwa kufanya uasherati, nini njo inaweza kufanya ikuwe nguvu kushinda ile jaribu? Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Ule ndugu mwenye video inazungumuzia alifanya nini wakati aliona kama mawazo yake na matendo yake inaweza kufanya asikuwe muaminifu kwa bibi yake?

Wakati fulani, hata Wakristo waaminifu wanaweza kuwa na mawazo yenye haiko safi. Unaweza kufanya nini juu usiendelee kuwaza juu ya mambo ya uasherati? Musome Wafilipi 4:8, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Tunapaswa kuwaza juu ya mambo gani?

  • Namna gani kusoma Biblia na kufanya mambo mingi mu kazi ya Yehova kunaweza kutusaidia tusiangukie mu uasherati?

5. Kanuni za Yehova zinatuletea faida

Yehova anajua mambo yenye inaweza kutuletea faida. Anatuambia mambo yenye tunaweza kufanya juu tuepuke uasherati na faida yenye tutapata kama tunafanya vile. Musome Mezali 7:7-27 ao muangalie VIDEO, kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Namna gani ule kijana mwanaume alijiingiza mu jaribu?​—Ona Mezali 7:8, 9.

  • Sawa vile Mezali 7:23, 26 inaonyesha, kufanya uasherati kunaweza kuletea mutu magumu ya nguvu sana. Kama tunaepuka uasherati, hatutapata magumu gani?

  • Namna gani kuepuka uasherati kunaweza kutusaidia tufurahie maisha milele?

Watu fulani wanawaza kama Biblia haipendi watu wafurahie maisha juu inakataza ngono kati ya wanaume na wanaume na wanamuke na wanamuke. Lakini Yehova, Mungu mwenye upendo, anapenda watu wafurahie maisha milele. Na juu tufikie kufurahia maisha milele, tunapaswa kutii kanuni zake. Musome 1 Wakorinto 6:9-11, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Ni ngono kati ya wanaume na wanaume na wanamuke na wanamuke njo tu yenye Mungu anakataza?

Juu tumufurahishe Mungu, siye wote tunapaswa kufanya mabadiliko. Unawaza kuko kabisa faida ya kufanya vile? Musome Zaburi 19:8, 11, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Unawaza kanuni zenye Yehova anatupatia juu ya namna tunapaswa kujiendesha zinafaa? Juu ya nini unawaza vile?

Yehova amesaidia watu wengi kutii kanuni zake juu ya namna tunapaswa kujiendesha. Na weye, anaweza kukusaidia

WATU FULANI WANASEMAKA: “Haiko mubaya kufanya ngono, kama tu munapendana.”

  • Weye unawaza nini?

KWA KIFUPI

Ngono ni zawadi yenye Yehova amepatia bibi na bwana juu waifurahie.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Uasherati ni nini?

  • Tunaweza kufanya nini juu tusiangukie mu uasherati?

  • Tutapata faida gani kama tunafuata kanuni zenye Yehova anatupatia juu ya namna tunapaswa kujiendesha?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona juu ya nini Mungu anapenda mwanaume na mwanamuke waoane kwanza mbele waanze kuishi pamoja.

“Biblia Inasema Nini Juu ya Kuishi Pamoja Mbele ya Kufunga Ndoa?” (Inapatikana ku Enternete)

Mawazo ya Biblia juu ya ngono kati ya wanaume na wanaume na wanamuke na wanamuke haimaanishe kama tuchukie wenye kufanya vile.

“Ni Mubaya kwa Mwanaume Kufanya Ngono na Mwanaume na Mwanamuke Kufanya Ngono na Mwanamuke?” (Inapatikana ku Enternete)

Ona namna sheria za Mungu juu ya ngono zinatulinda.

“Ngono ya Kinywa, Nayo Ni Ngono?” (Inapatikana ku Enternete)

Mu habari yenye kichwa “Walinitendea kwa Heshima,” ona nini ilisaidia mwanaume fulani mwenye alikuwa nafanya ngono na wanaume wenzake, abadilishe maisha yake na aanze kumufurahisha Mungu.

“Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 4, 2011)

a Kati ya zile ngono zenye hazifae, tunaweza kutaya matendo mbalimbali sawa vile ngono kupitia viungo vya uzazi, ngono ya kinywa, ngono ya mukundu, na kugusa-gusa viungo vya uzazi vya mutu mwingine ili kulamusha tamaa yake ya ngono.