SOMO LA 41

Biblia Inasema Nini Kuhusu Ngono?

Biblia Inasema Nini Kuhusu Ngono?

Watu wengi hawapendi kuzungumza kuhusu ngono. Hata hivyo, Biblia inazungumza kuhusu ngono kwa njia iliyo wazi na ya heshima. Tunanufaika na mambo ambayo Biblia inasema, na tunatarajia iwe hivyo kwa sababu Yehova ndiye Muumba wetu. Basi anajua mambo yanayotufaa kabisa. Anatuambia mambo tunayopaswa kufanya ili kumfurahisha, na mambo yatakayotusaidia kufurahia maisha milele.

1. Yehova ana maoni gani kuhusu ngono?

Ngono ni zawadi kutoka kwa Yehova. Anataka mwanamume na mwanamke waliofunga ndoa wafurahie zawadi hiyo. Zawadi hiyo inasaidia mume na mke kupata watoto, na pia kuonyeshana upendo mwororo kwa njia ya asili na yenye kufurahisha. Ndiyo sababu Neno la Mungu linasema hivi: “Na ushangilie pamoja na mke wa ujana wako.” (Methali 5:18, 19) Yehova anatarajia Mkristo aliyefunga ndoa awe mshikamanifu kwa mwenzi wake wa ndoa. Hivyo, wenzi wa ndoa hawapaswi kamwe kufanya uzinzi.​—Soma Waebrania 13:4.

2. Uasherati ni nini?

Biblia inatuambia kwamba “waasherati . . . hawataurithi Ufalme wa Mungu.” (1 Wakorintho 6:9, 10) Waandikaji wa Biblia walioandika kwa lugha ya Kigiriki, walitumia neno por·neiʹa kumaanisha uasherati. Neno hilo linatia ndani (1) kufanya ngono a na mtu ambaye si mume au mke wako, (2) ngono kati ya watu wa jinsia moja, na (3) kufanya ngono na mnyama. ‘Tunapojiepusha na uasherati,’ tunanufaika na pia tunamfurahisha Yehova.​—1 Wathesalonike 4:3.

CHIMBA ZAIDI

Chunguza jinsi unavyoweza kuepuka uasherati na jinsi utakavyonufaika kwa kudumisha maadili safi.

3. Ukimbieni uasherati

Mwanamume mwaminifu Yosefu alikataa kufanya uasherati aliposhawishiwa kufanya ngono na mke wa mtu mwingine. Soma Mwanzo 39:1-12, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Ni sababu gani iliyofanya Yosefu akimbie?​—Ona mstari wa 9.

  • Je, unafikiri Yosefu alifanya uamuzi unaofaa? Kwa nini?

Leo, vijana wanawezaje kumwiga Yosefu na kukimbia uasherati? Onyesha VIDEO.

Yehova anataka sisi sote tujiepushe na uasherati. Soma 1 Wakorintho 6:18, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Ni hali gani ambazo zinaweza kufanya mtu ashawishike kufanya uasherati?

  • Unawezaje kuukimbia uasherati?

4. Unaweza kupinga vishawishi

Ni nini kinachoweza kufanya iwe vigumu kupinga kishawishi cha kufanya uasherati? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

  • Ndugu katika video hiyo alifanya nini alipotambua kwamba mawazo na matendo yake yangefanya akose kuwa mwaminifu kwa mke wake?

Wakati mwingine, hata Wakristo waaminifu hupambana ili kudumisha mawazo safi. Unawezaje kuacha kufikiria mawazo machafu? Soma Wafilipi 4:8, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Tunapaswa kufikiria mambo gani?

  • Kusoma Biblia na kuwa na shughuli nyingi katika utumishi wa Yehova, kunawezaje kutusaidia kupinga vishawishi vya kutenda dhambi?

5. Viwango vya Yehova hutunufaisha

Yehova anajua mambo yanayotufaa kabisa. Anatufundisha jinsi ya kudumisha maadili safi na manufaa ya kufanya hivyo. Soma Methali 7:7-27 au onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.

  • Kijana huyo aliingiaje katika kishawishi?​—Ona Methali 7:8, 9.

  • Kulingana na Methali 7:23, 26, uasherati unaweza kuwa na matokeo mabaya sana. Tukidumisha maadili safi tutaepuka matatizo gani?

  • Kuwa na maadili safi kunawezaje kutusaidia kufurahia maisha milele?

Baadhi ya watu wanafikiri kwamba mambo ambayo Biblia inafundisha kuhusu ngono kati ya watu wa jinsia moja, si jambo la upendo kuwaelekea watu hao. Lakini Yehova ni Mungu mwenye upendo na anataka watu wote wafurahie maisha milele. Ili tustahili kuishi milele, lazima tufuate viwango vyake vya maadili. Soma 1 Wakorintho 6:9-11, kisha mzungumzie swali hili:

  • Je, Mungu anachukizwa tu na ngono kati ya watu wa jinsia moja au kuna mambo mengine yanayomchukiza?

Ili tumfurahishe Mungu, sisi sote tunahitaji kufanya mabadiliko. Je, tunanufaika tunapofanya mabadiliko hayo? Soma Zaburi 19:8, 11, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Je, unafikiri viwango vya Yehova kuhusu maadili vinafaa? Kwa nini?

Yehova amewasaidia watu wengi watii viwango vyake vya maadili. Anaweza kukusaidia pia

WATU FULANI HUSEMA: “Ni sawa kwa watu wawili kufanya ngono ikiwa wanapendana.”

  • Wewe una maoni gani?

MUHTASARI

Ngono ni zawadi ambayo Yehova amempa mume na mke ili waifurahie.

Ungejibuje?

  • Uasherati unatia ndani mambo gani?

  • Ni nini ambacho kitatusaidia kuepuka uasherati?

  • Tunanufaikaje tunapofuata viwango vya maadili vya Yehova?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Jifunze kwa nini Mungu anataka mwanamume na mwanamke wafunge ndoa kabla ya kuishi pamoja.

“Biblia Inasema Nini Kuhusu Kuishi Pamoja Bila Kufunga Ndoa?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

Jifunze kwa nini viwango vya Biblia kuhusu ngono kati ya watu wa jinsia moja havichochei chuki.

“Je, Ni Kosa Kufanya Ngono Kati ya Watu wa Jinsia Moja?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

Jifunze jinsi sheria za Mungu zinavyotulinda inapohusu matendo yote ya ngono.

“Je, Ngono ya Mdomo Ni Ngono?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

Katika simulizi “Walinionyesha Heshima,” ona jambo lililomchochea mtu aliyekuwa na zoea la kufanya ngono na watu wa jinsia yake abadili maisha yake ili amfurahishe Mungu.

“Biblia Inabadili Maisha” (Mnara wa Mlinzi, Aprili 1, 2011)

a Vitendo hivyo vya ngono visivyo halali vinatia ndani mambo mbalimbali kama vile kufanya ngono kwa mdomo, ngono ya mkundu, kupapasa viungo vya uzazi vya mtu mwingine ili kuamsha hamu ya ngono, na ngono kati ya mwanamume na mwanamke ambao hawajafunga ndoa.