Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 42

Biblia Inasema Nini Juu ya Ndoa na Juu ya Kubakia Bila Kuoa ao Kuolewa?

Biblia Inasema Nini Juu ya Ndoa na Juu ya Kubakia Bila Kuoa ao Kuolewa?

Mu maeneo fulani, watu wanawazaka kama, juu mutu akuwe na furaha anapaswa tu kuoa ao kuolewa. Lakini haiko kila mutu mwenye alishaoa ao kuolewa njo anakuwaka na furaha, na haiko kila mutu mwenye anabakia bila kuoa ao kuolewa njo hakuwake na furaha. Biblia inasema kama kuko faida ya kubakia bila kuoa ao kuolewa na kuko pia faida ya kuoa ao kuolewa.

1. Mutu anaweza kupata faida gani kama anabakia bila kuoa ao kuolewa?

Biblia inasema hivi: “Mutu yeyote mwenye anaoa ao anaolewa anafanya muzuri, lakini mutu yeyote mwenye haoe ao haolewe atafanya muzuri zaidi.” (Soma 1 Wakorinto 7:32, 33, 38.) Ni mu maana gani mutu mwenye anabakia bila kuoa ao kuolewa ‘anafanya muzuri zaidi’? Wakristo wenye hawayaoa wala kuolewa, hawana bibi ao bwana wa kuhangaikia. Njo maana wanakuwaka na uhuru mingi. Kwa mufano, wanaweza kufanya mambo mingi mu kazi ya Yehova, sawa vile kuenda mu inchi ingine juu ya kuhubiri habari njema. Na zaidi ya yote, wanaweza kuwa na wakati mingi ya kumukaribia Yehova.

2. Mutu anaweza kupata faida gani kama anaandikisha ndoa yake ku serikali?

Ndoa nayo, iko na faida zake. Biblia inasema kama “wawili ni muzuri zaidi kuliko mumoja.” (Muhubiri 4:9) Ile ni kweli zaidi sana kama Wakristo wanatumikisha kanuni za Biblia mu ndoa yao. Wakati bibi na bwana wanaandikisha ndoa yao ku serikali, wanafanya naziri kama watapendana, wataheshimiana na watahangaikiana. Ile inafanya wajisikie kuwa salama zaidi mu ndoa yao kuliko wale wenye wanaishi tu pamoja bila kuandikisha ndoa, na watoto wao pia wanajisikiaka salama zaidi.

3. Yehova anaona ndoa namna gani?

Wakati Yehova alibariki ndoa ya kwanza, alisema hivi: “Mwanaume atamuacha baba yake na mama yake na atashikamana na bibi yake.” (Mwanzo 2:24) Yehova anapenda bibi na bwana wapendane na wabakie pamoja maisha yao yote. Anaruhusu kuvunja ndoa kama tu bibi ao bwana anafanya uzinifu. Hata mu ile hali, Yehova anaachia bibi ao bwana mwenye hana kosa, haki ya kuamua ikiwa atavunja ndoa ao hapana. a (Matayo 19:9) Yehova haruhusu bwana Mukristo akuwe na bibi zaidi ya mumoja na bibi Mukristo akuwe na bwana zaidi ya mumoja.​—1 Timoteo 3:2.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone mambo yenye unaweza kufanya juu ukuwe na furaha na juu umufurahishe Yehova, ikuwe hauyaoa ao kuolewa ao ikuwe ulishaoa ao kuolewa.

4. Kama hauyaoa ao kuolewa, utumikishe muzuri wakati yako

Yesu alisema kama kubakia bila kuoa ao kuolewa ni zawadi. (Matayo 19:11, 12) Musome Matayo 4:23, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu Yesu hakuoaka, alitumia wakati yake namna gani juu ya kutumikia Baba yake na kusaidia wengine?

Wakristo wenye hawayaoa ao kuolewa wanaweza kupata furaha kama wanafuata mufano wa Yesu. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Wakristo wenye hawayaoa ao kuolewa wanaweza kufanya mambo gani ya muzuri?

Unajua?

Biblia haiseme mutu anapaswa kuoa ao kuolewa na miaka ngapi. Lakini inasema kama ni muzuri kijana angoye mupaka akuwe “amepita mwanzo wa kipindi cha ujana.” Juu mu ile kipindi tamaa ya ngono inakuwaka nguvu sana na inaweza kumufanya asikamate maamuzi ya muzuri.​—1 Wakorinto 7:36.

5. Uchagule muzuri mutu wa kuoana naye

Kuchagula mutu wa kuoana naye ni kati ya maamuzi ya maana sana mu maisha. Musome Matayo 19:4-6, 9, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini Mukristo hapaswe kukimbilia kuoa ao kuolewa?

Biblia inatuambia sifa zenye tunapaswa kuangalia wakati tuko natafuta mutu wa kuoana naye. Zaidi ya yote, inatuambia tutafute mutu mwenye anamupenda Yehova. b Musome 1 Wakorinto 7:39 na 2 Wakorinto 6:14. Kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Juu ya nini tunapaswa kuoa ao kuolewa tu na Mukristo mwenzetu?

  • Unawaza Yehova anaweza kujisikia namna gani kama tunaoa ao kuolewa na mutu mwenye hamupendi?

Kama mutu anafungia nira ku shingo ya wanyama wawili wenye wako tofauti sana, wale wanyama watateseka. Vilevile, kama Mukristo anaoa ao kuolewa na mutu mwenye haiko Mukristo mwenzake, watakuwa na magumu mingi

6. Uone ndoa namna Yehova anaiona

Zamani, wanaume fulani wa Israeli walikuwa navunja ndoa na bibi zao juu ya sababu za burebure. Musome Malaki 2:13, 14, 16, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini Yehova anachukia wakati bibi ao bwana anavunja ndoa juu ya sababu za burebure?

Wakati mutu anafanya uzinifu na kuvunja ndoa, ile inaumizaka sana bibi ao bwana mwenye hana kosa na inaumizaka pia watoto

Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Kama uko na bibi ao bwana mwenye haiko Shahidi, unaweza kufanya nini juu ndoa yako ikuwe na furaha?

7. Tumikisha kanuni za Yehova mu ndoa yako

Wakati fulani inaombaka mutu ajikaze sana juu atumikishe kanuni za Yehova mu ndoa yake. c Lakini Yehova hakosake kubariki mutu mwenye anafanya vile. Muangalie VIDEO.

Musome Waebrania 13:4, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Unawaza kanuni za Yehova juu ya ndoa zinafaa? Juu ya nini unawaza vile?

Yehova anapenda Wakristo waandikishe ndoa zao ku serikali, na kama wanavunja ndoa, wafanye vile ku serikali. Juu mu inchi za mingi, serikali njo inasimamiaka ile mambo. Musome Tito 3:1, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Kama ulishaoa ao kuolewa, uko hakika kama ndoa yako imeandikishwa ku serikali?

KAMA MUTU ANAULIZA: “Juu ya nini tuoane? Si tunaweza kuishi tu pamoja?”

  • Utamujibia nini?

KWA KIFUPI

Kubakia bila kuoa ao kuolewa na kuoa ao kuolewa, yote iko na faida, na yote ni zawadi kutoka kwa Yehova. Yote inaleta furaha kama tu mutu anatumikisha kanuni za Yehova mu maisha yake.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Mutu mwenye hayaoa ao kuolewa, anaweza kufanya mambo gani ya muzuri?

  • Juu ya nini Biblia inasema kama Mukristo anapaswa tu kuoa ao kuolewa na Mukristo mwenzake?

  • Ni sababu gani moja tu yenye inaweza fanya mutu avunje ndoa?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Kuoa ao kuolewa “katika Bwana tu,” maana yake nini?

“Maulizo ya Wasomaji Wetu” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 7, 2004)

Ona video mbili zenye zinaweza kukusaidia ukamate maamuzi ya muzuri juu ya uchumba na ndoa.

Namna ya Kujitayarisha kwa Ajili ya Ndoa (11:53)

Ona juu ya nini ndugu fulani anaona kama mambo yote yenye Yehova amemupatia ni ya maana sana kupita mambo yote yenye aliachaka.

Nilikuwa Natumainia Kama Atajifunzaka Kweli (1:56)

Mutu anapaswa kufikiria mambo gani mbele ya kuamua kama atavunja ndoa ao ataachana na bibi ao bwana yake?

Heshimia “Kile Chenye Mungu Ameunganisha” (Munara wa Mulinzi, Mwezi wa 12, 2018)

a Ona Mafasirio Ingine ya 4 kuhusu kuachana wakati bibi ao bwana hakufanya uzinifu.

b Mu maeneo fulani, wazazi njo wanachaguliaka watoto wao mutu wa kuoana naye. Kama ni vile, haiko makuta njo wazazi wenye upendo wanapaswa kuangalia. Wanapaswa kwanza kuangalia kama ule mutu anamupenda Yehova ao hapana.

c Kama unaishi na mutu lakini hamuyaoana, weye peke njo utaamua ikiwa utaachana naye ao utaoana naye.