Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 43

Wakristo Wanapaswa Kuwa na Mawazo Gani Juu ya Pombe?

Wakristo Wanapaswa Kuwa na Mawazo Gani Juu ya Pombe?

Mu dunia yote, watu wako na mawazo tofauti-tofauti juu ya pombe. Wamoja wanafurahiaka kunywa wakati fulani pamoja na marafiki. Wengine hawakunywake hata kidogo. Na wengine wanakunywaka sana mupaka wanalewa. Sasa Biblia inasema nini juu ya pombe?

1. Ni mubaya kunywa pombe?

Biblia haiseme kama ni mubaya kunywa pombe. Inasema kama “divai yenye inafanya moyo wa mwanadamu ufurahi,” iko kati ya zawadi zenye Mungu ametupatia (Zaburi 104:14, 15) Wanaume na wanamuke fulani waaminifu, wenye Biblia inazungumuzia, walikuwaka nakunywa pombe.​—1 Timoteo 5:23.

2. Biblia inapatia watu wenye wanaamua kunywa pombe mashauri gani?

Yehova anakataza kunywa sana na kulewa. (Wagalatia 5:21) Neno yake Biblia inasema hivi: “Usikuwe kati ya wale wenye kunywa divai nyingi sana.” (Mezali 23:20) Njo maana, kama tunaamua kunywa pombe, hata wakati tuko siye peke, hatupaswe kunywa sana mupaka akili yetu inaacha kutumika muzuri, tunaanza kusema na kutenda ovyo-ovyo, ao mupaka tunaharibisha afya yetu. Kama hatutaweza kujizuia, ni muzuri tusikuwe nakunywa hata kidogo.

3. Unaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama unaheshimia maamuzi ya wengine juu ya pombe?

Kila mutu iko na haki ya kuamua kama atakunywa pombe ao hapana. Hatupaswe kuhukumu mutu mwenye anaamua kunywa pombe kwa kiasi, na hatupaswe kukaza mutu akunywe pombe kama hapendi. (Waroma 14:10) Ni muzuri tusikunywe kama tunaweza kukwaza wengine. (Soma Waroma 14:21.) Tunapaswa kutafuta ‘hapana faida yetu wenyewe, lakini faida ya ule mutu mwingine.’​—Soma 1 Wakorinto 10:23, 24.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone kanuni za Biblia zenye zinaweza kukusaidia uamue kama utakuwa nakunywa pombe ao hapana, na kama unaamua kunywa, utakunywa kiasi gani. Na tuone mambo yenye unaweza kufanya kama uko na tatizo ya kunywa sana.

4. Amua kama utakunywa pombe ao hapana

Yesu alikuwa na mawazo gani juu ya pombe? Juu ya kupata jibu, ona muujiza wa kwanza wenye alifanyaka. Musome Yohana 2:1-11, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Wakati tunachunguza ile muujiza, tunaona Yesu iko na mawazo gani juu ya pombe na juu ya wale wenye wanakunywaka pombe?

  • Juu Yesu hakukatazaka kunywa pombe, Mukristo anapaswa kuona namna gani mutu mwenye anaamua kunywa pombe?

Ni kweli kama Mukristo iko huru kunywa pombe, lakini wakati fulani, haikuwake muzuri kufanya vile. Musome Mezali 22:3, na kisha muone ikiwa ni jambo ya hekima kunywa pombe mu hali zenye kufuata:

  • Utatembeza gari ao utatumikisha mashini fulani.

  • Uko na mimba.

  • Munganga amekushauria usikuwe nakunywa pombe.

  • Hauwezake kujizuia kama uko mbele ya pombe.

  • Sheria ya serikali inakukataza kunywa pombe.

  • Uko na mutu mwenye ameamua kama hatakunywaka pombe juu zamani hakukuwaka naweza kujizuia.

Utapatia watu pombe ku karamu ya ndoa ao wakati ingine ya kujifurahisha? Juu ya kuona mambo yenye inaweza kukusaidia kuamua, muangalie VIDEO.

Musome Waroma 13:13 na 1 Wakorinto 10:31, 32. Kisha kusoma kila andiko, muzungumuzie hii ulizo:

  • Namna gani kutumikisha kanuni za Biblia kunaweza kukusaidia ukamate uamuzi wa muzuri wenye utafurahisha Yehova?

Kila Mukristo anapaswa kujiamulia kama atakunywa pombe ao hapana. Hata kama anakunywaka wakati fulani, wakati ingine anaweza kuamua kama haiko muzuri kunywa

5. Amua utakunywa kiasi gani ya pombe

Ikiwa unaamua kunywa pombe, ukumbuke kama Yehova hakataze kunywa pombe, lakini anakataza kunywa sana. Juu ya nini? Musome Hosea 4:11, 18, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Mambo inaweza kuwa namna gani kama mutu anakunywa sana?

Tunaweza kufanya nini juu tuepuke kunywa sana? Tunapaswa kuwa na kiasi ao kujua mipaka yetu. Musome Mezali 11:2, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini ni muzuri kuamua ni kiasi gani ya pombe utakuwa nakunywa?

6. Nini njo inaweza kusaidia mutu aachane na tabia ya kunywa sana?

Ona mambo yenye ilisaidia mwanaume fulani aache kunywa sana. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, pombe ilikuwa nafanya Dmitry ajiendeshe namna gani?

  • Ilikuwaka mwepesi kwake kuachana na pombe?

  • Alifanya nini juu aweze kuachana na tabia ya kunywa sana?

Musome 1 Wakorinto 6:10, 11, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Juu ya nini ulevi ni kosa kubwa sana?

  • Nini njo inaonyesha kama mulevi anaweza kubadilika?

Musome Matayo 5:30, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Kukata mukono maana yake kuwa tayari kuachana na kitu fulani yenye tunapendaka sana juu tu tumufurahishe Yehova. Unaweza kufanya nini kama unakunywaka sana? a

Musome 1 Wakorinto 15:33, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Mambo inaweza kuwa namna gani kama uko na marafiki wenye wanakunywaka sana?

KAMA MUTU ANAULIZA: “Ni mubaya kunywa pombe?”

  • Utamujibia nini?

KWA KIFUPI

Pombe ni zawadi yenye Yehova ametupatia juu tuifurahie, lakini anakataza kunywa sana na kulewa.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Biblia inasema nini juu ya pombe?

  • Kunywa sana kunaweza kuletea mutu magumu gani?

  • Tunaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama tunaheshimia maamuzi ya wengine juu ya pombe?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Nini njo inaweza kusaidia vijana wakamate maamuzi ya muzuri kuhusu pombe?

Ufikirie Matokeo Mbele ya Kunywa (2:31)

Ona mambo yenye unaweza kufanya juu uachane na tabia ya kunywa sana.

“Acha Pombe Fasi Yake” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 1, 2010)

Wakristo wanapaswa kugonganisha virauli mbele ya kunywa?

“Maulizo ya Wasomaji Wetu” (Munara wa Mulinzi, 15 Mwezi wa 2, 2007)

Mu habari “Nilikuwaka Nakunywa Sana,” ona namna mwanaume fulani aliachaka tabia ya kunywa sana.

“Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 5, 2012)

a Watu wenye walishakuwa watumwa wa pombe wanaweza kuwa na lazima ya kuonana na wanganga. Wanganga wengi wanasema kama wale wenye walikuwaka na tatizo ya kunywa sana zamani, hawapaswe kunywa hata kidogo.