Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 45

Kukatala Kuunga Mukono Upande Wowote, Maana Yake Nini?

Kukatala Kuunga Mukono Upande Wowote, Maana Yake Nini?

Yesu alifundisha wanafunzi wake kama hawapaswe kuwa “sehemu ya ulimwengu.” (Yohana 15:19) Mutu mwenye haiko sehemu ya ulimwengu anaepukaka mambo mbalimbali. Kwa mufano, anakatalaka kuunga mukono upande wowote, ni kusema anakatalaka kujiingiza mu mambo ya politike ao ya vita. Wakati fulani haikuwake mwepesi kukatala kuunga mukono upande wowote. Ile inaweza kufanya wengine watuchekelee. Unaweza kufanya nini juu usiunge mukono upande wowote na ubakie mushikamanifu kwa Yehova Mungu?

1. Wakristo wanaona namna gani guvernema za wanadamu?

Wakristo wanaheshimia guvernema za wanadamu. Tunatii Yesu kwa ‘kumulipa Kaisari vitu vya Kaisari,’ ni kusema, tunatii sheria za inchi, sawa vile sheria zenye zinatuomba kulipa kodi. (Marko 12:17) Biblia inaonyesha kama ikiwa guvernema za wanadamu ziko natawala, ni juu Yehova anaziruhusu zitawale. (Waroma 13:1) Njo maana, mamlaka ya guvernema za wanadamu iko na mipaka. Tunajua kama Mungu atatumia Ufalme wake juu ya kumaliza magumu yote ya wanadamu.

2. Unaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama hauunge mukono upande wowote?

Sawa Yesu, hatujiingizake mu mambo ya politike. Kisha kuona muujiza fulani wa Yesu, watu walipendaka kumufanya kuwa mufalme hapa ku dunia. Lakini Yesu alikatalaka. (Yohana 6:15) Juu ya nini? Yesu alionyeshaka sababu wakati alisemaka hivi: “Ufalme wangu hauko sehemu ya ulimwengu huu.” (Yohana 18:36) Juu tuko wanafunzi wa Yesu, tunaonyeshaka kama hatuunge mukono upande wowote kwa kuepuka mambo fulani. Kwa mufano, hatuendake ku vita. (Soma Mika 4:3.) Tunaheshimia alama za inchi, sawa vile bendera (drapeau), lakini hatuziabudu. (1 Yohana 5:21) Tena, hatuunge mukono ao kupinga chama fulani ya politike ao kiongozi fulani. Wakati tunafanya vile, tunaonyesha kama tuko washikamanifu kabisa kwa Ufalme wa Mungu.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone ni mu hali gani mbalimbali inaweza kuwa nguvu kukatala kuunga mukono upande wowote, na tuone mambo yenye itakusaidia ukamate maamuzi yenye itafurahisha Yehova.

3. Wakristo wa kweli hawaunge mukono upande wowote

Yesu na wanafunzi wake walituachia mufano. Musome Waroma 13:1, 5-7 na 1 Petro 2:13, 14. Kisha, muangalie VIDEO na muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Juu ya nini tunapaswa kuheshimia viongozi wenye guvernema inaweka?

  • Tunaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama tunawaheshimia?

Wakati wa vita, inchi fulani zinaweza kusema kama haziunge mukono upande wowote, lakini ziko nasaidia ngambo zote mbili. Kukatala kuunga mukono upande wowote, maana yake nini kabisa? Musome Yohana 17:16. Kisha, muangalie VIDEO na muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Kukatala kuunga mukono upande wowote maana yake nini?

Sasa, utafanya nini kama wakubwa wa inchi wanakuomba ufanye jambo fulani yenye sheria ya Mungu inakataza? Musome Matendo 5:28, 29. Kisha, muangalie VIDEO na muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Kama sheria ya wanadamu inapingana na sheria ya Mungu, tunapaswa kutii sheria ya nani?

  • Unawaza ni mu hali gani Wakristo hawapaswe kutii sheria zenye guvernema inaweka?

4. Usiunge mukono upande wowote, ikuwe mu mawazo ao mu matendo

Musome 1 Yohana 5:21. Kisha, muangalie VIDEO na muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, juu ya nini Ayenge aliamua kama hataunga mukono chama yoyote ya politike ao kujiingiza mu mambo ya kutukuza inchi, sawa vile kusalimia bendera?

  • Unawaza alikamata uamuzi muzuri?

Ni mu hali gani zingine njo inaweza kuwa nguvu kukatala kuunga mukono upande wowote? Muangalie VIDEO, na muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Namna gani tunaweza kuepuka kuunga mukono upande wowote wakati tuko naangalia michezo yenye iko nachezwa na watu wa inchi mbalimbali?

  • Namna gani tunaweza kuepuka kuunga mukono upande wowote wakati wakubwa wa inchi wanakamata maamuzi yenye inafanya maisha yetu ikuwe nguvu ao yenye inafanya maisha yetu ikuwe muzuri?

  • Namna gani habari zenye tunasikia ku televizyo ao ku radio ao kwa marafiki, zinaweza kutuchochea tuunge mukono upande fulani?

Ni mu hali gani Mukristo anapaswa kuepuka kuunga mukono upande wowote mu mawazo na mu matendo?

KAMA MUTU ANAULIZA: “Juu ya nini hausalimiake bendera ao kuimba wimbo wa taifa?”

  • Utamujibia nini?

KWA KIFUPI

Wakristo wanajikazaka sana juu wasiunge mukono upande wowote mu mambo ya politike, ikuwe mu mawazo, mu maneno, ao mu matendo.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Tunapaswa kupatia serikali za wanadamu nini?

  • Juu ya nini hatujiingizake mu mambo ya politike?

  • Ni mu hali gani inaweza kuwa nguvu kukatala kuunga mukono upande wowote?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Tunapaswa kujiima mambo gani juu tusiunge mukono upande wowote?

Hakuna Siku Yehova Ametuacha (3:14)

Familia zinaweza kufanya nini juu ya kujitayarisha kuhusu namna ya kutenda mu hali zenye zinaweza kufanya ikuwe nguvu kukatala kuunga mukono upande wowote?

Epuka Kuunga Mukono Upande Wowote Katika Kila Hali (4:25)

Juu ya nini mutu kutetea inchi yake haiko njo jambo ya maana sana?

“Kwa Mungu Mambo Yote Yanawezekana” (5:19)

Ona namna unaweza kuepuka kuwa sehemu ya ulimwengu wakati uko nachagula kazi yenye utafanya.

“Kila Mutu Atabeba Muzigo Wake Mwenyewe” (Munara wa Mulinzi, 15 Mwezi wa 3, 2006)