Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 46

Kwa Nini Unapaswa Kujiweka Wakfu na Kubatizwa?

Kwa Nini Unapaswa Kujiweka Wakfu na Kubatizwa?

Tunajiweka wakfu kwa Yehova tunapomwahidi katika sala kwamba tutamwabudu yeye peke yake na kutanguliza mapenzi yake maishani. (Zaburi 40:8) Hatua inayofuata ni kubatizwa. Unapobatizwa, unaowaonyesha wengine kwamba umejiweka wakfu. Uamuzi wa kujiweka wakfu kwa Yehova ndio uamuzi muhimu zaidi maishani. Ni nini ambacho kitakuchochea ufanye uamuzi huo muhimu sana na utakaobadili maisha yako?

1. Ni nini ambacho humchochea mtu ajiweke wakfu?

Tunachochewa na upendo kujiweka wakfu kwa Yehova. (1 Yohana 4:10, 19) Biblia inatuhimiza hivi: “[Mpende] Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.” (Marko 12:30) Tunaonyesha kwamba tunampenda Mungu si kwa maneno tu, bali pia kwa matendo yetu. Kama vile mwanamume na mwanamke wanaopendana sana wanavyoamua kufunga ndoa, vivyo hivyo kumpenda Yehova hutuchochea kujiweka wakfu kwake na kubatizwa.

2. Yehova anawapa baraka gani Mashahidi wake waliobatizwa?

Unapobatizwa, unajiunga na familia ya Yehova yenye furaha. Kisha utajionea upendo wake kwa njia nyingi sana na utazidi kumkaribia hata zaidi. (Soma Malaki 3:16-18.) Yehova atakuwa kama Baba kwako, isitoshe utakuwa na familia ya kiroho ya akina ndugu na dada ulimwenguni pote wanaompenda Yehova na wanaokupenda pia. (Soma Marko 10:29, 30.) Bila shaka, lazima uchukue hatua fulani kabla ya kubatizwa. Unapaswa kujifunza kumhusu Yehova, kumpenda, na kuwa na imani katika Mwana wake. Mwishowe, lazima ujiweke wakfu kwa Yehova. Ukichukua hatua hizo kisha ubatizwe, utakuwa umeanza kutembea katika barabara inayoongoza kwenye uzima wa milele. Neno la Mungu linasema hivi: “Ubatizo . . . unawaokoa ninyi sasa pia.”​—1 Petro 3:21.

CHIMBA ZAIDI

Jifunze kwa nini ni muhimu kwako kujiweka wakfu kwa Yehova na kubatizwa.

3. Sisi sote tunapaswa kuchagua yule tutakayemtumikia

Katika taifa la kale la Israeli, baadhi ya watu walifikiri kwamba wangemwabudu Yehova na pia mungu wa uwongo Baali. Lakini Yehova alimtuma nabii wake Eliya arekebishe maoni hayo yasiyo sahihi. Soma 1 Wafalme 18:21, kisha mzungumzie swali hili:

  • Waisraeli walipaswa kufanya uamuzi gani?

Kama Waisraeli, sisi pia tunapaswa kuchagua yule tutakayemtumikia. Soma Luka 16:13, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Kwa nini hatupaswi kumwabudu Yehova na wakati huohuo kuabudu mtu au kitu kingine?

  • Tunamwonyeshaje Yehova kwamba tumechagua kumwabudu yeye?

4. Tafakari upendo ambao Yehova amekuonyesha

Yehova ametupatia zawadi nyingi zenye thamani. Tunaweza kumpatia nini? Onyesha VIDEO.

Yehova amekuonyesha kwa njia gani kwamba anakupenda? Soma Zaburi 104:14, 15 na 1 Yohana 4:9, 10, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Ni zawadi gani kutoka kwa Yehova ambazo hasa zinakuchochea kumshukuru?

  • Zawadi hizo zinafanya uhisije kumhusu Yehova?

Tunapopokea zawadi ambayo tunaipenda, tunachochewa kumwonyesha shukrani yule aliyetupatia zawadi hiyo. Soma Kumbukumbu la Torati 16:17, kisha mzungumzie swali hili:

  • Unapofikiria mambo yote ambayo Yehova amekufanyia, unachochewa kufanya nini?

5. Kujiweka wakfu huleta baraka nyingi

Watu wengi wanaamini kwamba umaarufu, kazi nzuri, au pesa zitawafanya wawe na furaha. Je, hilo ni kweli? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.

  • Ingawa mwanamichezo katika video hiyo alipenda kucheza mpira, kwa nini aliacha kucheza mpira?

  • Aliamua kujiweka wakfu kwa Yehova bali si kucheza mpira. Je, unafikiri alifanya uamuzi sahihi? Kwa nini?

Kabla mtume Paulo hajawa Mkristo, alikuwa na kazi nzuri sana. Alikuwa amesomea sheria ya Wayahudi na mwalimu wake alikuwa mashuhuri. Lakini aliacha hayo yote ili awe Mkristo. Je, Paulo alijuta? Soma Wafilipi 3:8, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Kwa nini Paulo alisema kwamba mambo aliyofanya kabla ya kuwa Mkristo yalikuwa “takataka nyingi”?

  • Uamuzi wake ulimletea baraka gani?

  • Unafikiri ni nini ambacho kitafanya uwe na maisha bora, je, ni kumtumikia Yehova au ni kufuatia malengo mengine maishani?

Baada ya kuwa Mkristo, Paulo alipata faida nyingi kuliko mambo aliyoacha

WATU FULANI HUSEMA: “Si lazima umtumikie Mungu, furahia maisha.”

  • Kwa nini unafikiri ni muhimu kujiweka wakfu kwa Yehova?

MUHTASARI

Kumpenda Yehova hutuchochea kujiweka wakfu kwake na kubatizwa.

Ungejibuje?

  • Kwa nini tunapaswa kumpenda Yehova kwa moyo wetu wote na kumwabudu yeye peke yake?

  • Yehova huwapa baraka gani Mashahidi wake waliobatizwa?

  • Je, ungependa kujiweka wakfu kwa Yehova?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Ona sababu iliyofanya mwanamuziki na mwanamichezo waamue kujiweka wakfu kwa Yehova.

Vijana Huuliza​—Nitayatumiaje Maisha Yangu?​—Kukumbuka Yaliyopita (6:52)

Katika video hii ya muziki, ona shangwe ambayo wale wanaojiweka wakfu kwa Yehova wanapata.

Ninajitoa Kwako (4:30)

Katika simulizi “Kwa Miaka Mingi Nilijiuliza, ‘Kwa Nini Tuko Hai?’” ona jambo lililomchochea mwanamke fulani achunguze mambo aliyotanguliza maishani.

“Biblia Inabadili Maisha” (Mnara wa Mlinzi, Novemba 1, 2012)