Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 46

Juu ya Nini Unapaswa Kujitoa kwa Mungu na Kubatizwa?

Juu ya Nini Unapaswa Kujitoa kwa Mungu na Kubatizwa?

Unajitoa kwa Yehova wakati unamuambia mu sala kama yeye tu njo utaabudu na utamutia pa nafasi ya kwanza mu maisha yako. (Zaburi 40:8) Kisha pale, njo unaweza kubatizwa. Wakati unabatizwa, unaonyesha wengine kama umejitoa kwa Mungu. Kujitoa kwa Yehova njo uamuzi wa maana sana mu maisha. Nini njo inaweza kukuchochea ukamate ule uamuzi wenye utabadilisha maisha yako?

1. Nini njo inachocheaka mutu ajitoe kwa Mungu?

Tunajitoaka kwa Mungu juu tunamupenda. (1 Yohana 4:10, 19) Biblia inatuambia hivi: ‘Umupende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.’ (Marko 12:30) Tunaonyesha kama tunamupenda Yehova kupitia maneno yetu na matendo yetu. Upendo njo unachocheaka mwanaume na mwanamuke waoane. Vilevile, kumupenda Yehova njo kunachocheaka mutu ajitoe kwake na kubatizwa.

2. Yehova anapatiaka Mashahidi wake wenye kubatizwa baraka gani?

Wakati unabatizwa, unaingia mu familia ya Yehova yenye furaha. Mu ile familia, utaona mambo mingi yenye kuonyesha kama Yehova anakupenda na utakuwa rafiki yake sana kuliko hata leo. (Soma Malaki 3:16-18.) Yehova atakuwa Baba yako, na utakuwa na familia ya ndugu na dada wa mu dunia yote wenye wanamupenda na wenye wanakupenda pia. (Soma Marko 10:29, 30.) Lakini, kuko mambo fulani yenye unapaswa kufanya mbele ubatizwe. Unapaswa kujifunza juu ya Yehova, kumupenda, na kuamini Mwana wake. Na ku mwisho, unapaswa kutoa maisha yako kwa Yehova. Kama unafanya ile mambo na kisha unabatizwa, utakuwa na tumaini ya kufurahia maisha milele. Biblia inasema hivi: “Ubatizo . . . unawaokoa ninyi sasa pia.”​—1 Petro 3:21.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone juu ya nini ni jambo ya maana ujitoe kwa Yehova na kubatizwa.

3. Siye wote tunapaswa kuchagula nani njo tutatumikia

Mu Israeli ya zamani, watu fulani waliwaza kama wanaweza kumuabudu Yehova na wako naabudu pia Baali, mungu wa uongo. Lakini, Yehova alituma nabii wake Eliya juu awaonyeshe kama ni makosa kuwaza vile. Musome 1 Wafalme 18:21, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Waisraeli walipaswa kukamata uamuzi gani?

Kama Waisraeli, na siye tunapaswa kuchagula nani njo tutatumikia. Musome Luka 16:13, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Juu ya nini hatuwezi kumuabudu Yehova na tuko pia naabudu mutu mwingine ao kitu ingine?

  • Tunaweza kufanya nini juu ya kuonyesha Yehova kama yeye njo tunachagula kuabudu?

4. Fikiria mambo yenye inaonyesha kama Yehova anakupenda

Yehova ametupatia mambo mingi sana ya muzuri. Na siye tunaweza kumupatia nini? Muangalie VIDEO.

Yehova amefanya mambo gani juu ya kuonyesha kama anakupenda? Musome Zaburi 104:14, 15 na 1 Yohana 4:9, 10, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Kati ya ile mambo yenye Yehova ametupatia, ya wapi njo unafurahiaka sana?

  • Wakati unafikiria ile mambo, unaona Yehova namna gani?

Wakati mutu anatupatia zawadi yenye tunafurahia kabisa, tunapendaka kumushukuru. Musome Kumbukumbu la Torati 16:17, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Wakati unafikiria mambo yote yenye Yehova alishakufanyia, unawaza na weye unaweza kumupatia nini?

5. Utapata baraka mingi kama unajitoa kwa Mungu

Watu wengi wanawazaka kama kujulikana sana, kuwa na kazi ya muzuri, ao makuta njo itawaletea furaha. Ile ni kweli? Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Hata kama ule mutu mwenye video inazungumuzia alipenda sana kucheza kabumbu, juu ya nini aliacha?

  • Aliamua kujitoa kwa Yehova, hapana kwa kabumbu. Unawaza aliamua muzuri? Juu ya nini?

Mbele mutume Paulo akuwe Mukristo, alikuwaka nafuatia kazi yenye ingemufanya ajulikane sana. Alifundishwa sheria ya Wayahudi na mwalimu mwenye kujulikana sana. Lakini, aliacha ile mambo yote juu akuwe Mukristo. Kuko siku alihuzunikaka juu ya uamuzi wenye alikamataka? Musome Wafilipi 3:8, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Juu ya nini Paulo alisema kama mambo yenye alikuwaka nafanya mbele akuwe Mukristo ilikuwa “takataka nyingi,” ao uchafu?

  • Lakini alipata baraka gani?

  • Kama unalinganisha kumutumikia Yehova na kufanya mambo ingine, unaona namna gani?

Wakati Paulo alikubali kuwa Mukristo, alipata baraka mingi sana kupita mambo yenye aliacha

WATU FULANI WANASEMAKA: “Kutoa maisha yako kwa Mungu ni kujitia kamba ku shingo.”

  • Juu ya nini unawaza kama ni muzuri kujitoa kwa Yehova?

KWA KIFUPI

Kumupenda Yehova njo kunatuchochea tujitoe kwake na kubatizwa.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Juu ya nini Yehova tu njo tunapaswa kupenda na kuabudu kwa moyo wote?

  • Yehova anapatiaka Mashahidi wake wenye kubatizwa baraka gani?

  • Na weye unapenda kujitoa kwa Yehova?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona juu ya nini muimbaji fulani na muchezaji fulani waliamua kujitoa kwa Yehova.

Vijana Wanauliza​—Nitatumia Namna Gani Maisha Yangu?​—Wanakumbuka (6:54)

Ona sababu zingine zenye zinapaswa kukuchochea ujitoe kwa Yehova.

“Juu ya Nini Ujitoe kwa Yehova?” (Munara wa Mulinzi, 15 Mwezi wa 1, 2010)

Mu hii video ya muziki, ona furaha yenye wale wenye kujitoa kwa Yehova wanapataka.

Ninatoa Maisha Yangu Kwako (4:30)

Ona mambo yenye ilichochea mwanamuke fulani atafute kujua nini njo ilikuwa ya maana zaidi mu maisha yake, mu habari yenye kichwa “Kwa Miaka Mingi Nilijiuliza, ‘Sababu Gani Tunaishi?’”.

“Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 11, 2012)