Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 48

Uchagule Marafiki Wazuri

Uchagule Marafiki Wazuri

Wakati ya furaha, marafiki wanafurahiaka pamoja na siye, na wakati ya magumu wanatusaidiaka. Lakini Biblia inaonyesha kama haiko kila mutu njo rafiki muzuri. Sasa, namna gani unaweza kuchagula marafiki wazuri? Tuzungumuzie maulizo yenye kufuata.

1. Marafiki wanaweza kukuchochea ufanye nini?

Mara mingi tunafananaka marafiki wetu. Wanaweza kutuchochea kufanya mambo ya muzuri ao ya mubaya. Njo vile mambo inakuwaka, ikuwe tuko napitisha nao wakati uso kwa uso, ao tuko nazungumuza nao kupitia Enternete. Biblia inasema hivi: “Mwenye anatembea na wenye hekima atakuwa na hekima, lakini mwenye kufanya urafiki na wajinga [wale wenye hawamupendi Yehova] ataumia.” (Mezali 13:20) Marafiki wenye wanamupenda na kumuabudu Yehova wanaweza kukusaidia uendelee kumupenda Yehova na ukamate maamuzi ya muzuri. Kama unakuwa rafiki wa sana wa watu wenye hawamupendi Yehova, wanaweza kukufanya umuache. Njo maana Biblia inatushauria tuchagule muzuri marafiki! Kama tunakuwa marafiki wa watu wenye wanamupenda Yehova, watatusaidia, na siye tutawasaidia. ‘Tutaendelea kutiana moyo na kujengana.’​—1 Watesalonike 5:11.

2. Yehova anaweza kujisikia namna gani wakati anaona marafiki wenye tunachagula?

Yehova hachagulake marafiki ovyo-ovyo. Biblia inasema kama Yehova “anafanya urafiki wa karibu pamoja na watu wanyoofu [ao waaminifu].” (Mezali 3:32) Sasa, anaweza kujisikia namna gani kama tunachagula marafiki wenye hawamupendi? Anaweza kuhuzunika sana! (Soma Yakobo 4:4.) Lakini, Yehova atafurahi sana na atatuchagula juu tukuwe marafiki wake kama tunaepuka marafiki wabaya na kama tunafanya urafiki pamoja naye, na wale wenye wanamupenda.​—Zaburi 15:1-4.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone juu ya nini ni jambo ya maana tuchagule marafiki wazuri, na namna unaweza kupata marafiki wenye watakusaidia kabisa.

3. Uepuke marafiki wabaya

Watu wenye hawamupendi Mungu na sheria zake hawako marafiki wazuri. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Namna gani tunaweza kuanza kufanya urafiki na watu wabaya bila hata kujua?

Musome 1 Wakorinto 15:33, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Ni mutu wa namna gani njo anaweza kuwa mashirika ao rafiki mubaya? Juu ya nini unasema vile?

Musome Zaburi 119:63, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Wakati uko nachagula rafiki, nini njo unapaswa kuangalia?

Tunda moja ya kuoza, inaweza kuozesha matunda ingine. Namna gani marafiki wabaya wanaweza kukuchochea ufanye mambo ya mubaya?

4. Watu wenye hawako sawasawa na siye, wanaweza pia kuwa marafiki wazuri

Biblia inazungumuzia Daudi na Yonatani, wanaume wawili wenye walikuwa naishi mu Israeli ya zamani. Hawakukuwa sawasawa juu Yonatani alikuwa mukubwa sana kupita Daudi, na alikuwa mutoto wa mufalme; hata vile, walikuwa marafiki wa sana. Musome 1 Samweli 18:1, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini haiko lazima tukuwe tu na marafiki wa miaka yetu, na wenye wako na maisha sawa yetu?

Musome Waroma 1:11, 12, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Namna gani marafiki wenye kumupenda Yehova wanaweza kutiana moyo?

Mu hii video, ona namna ndugu kijana alipata marafiki fasi zenye hakuwazia. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, juu ya nini wazazi wa Akil walikuwa na wasiwasi juu ya marafiki wake ku masomo?

  • Juu ya nini alikuwa napenda wale marafiki?

  • Alifanya nini juu asikuwe najisikia kama iko peke yake?

5. Namna ya kupata marafiki wazuri

Ona mambo yenye unaweza kufanya juu upate marafiki wazuri, na namna na weye unaweza kuwa rafiki muzuri. Muangalie VIDEO.

Musome Mezali 18:24 na 27:17, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Marafiki wazuri wanafanyaka nini juu ya kusaidiana?

  • Uko na marafiki wa vile? Kama hauna, unaweza kufanya nini juu ukuwe nao?

Musome Wafilipi 2:4, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ukuwe na marafiki wazuri, unapaswa kwanza kuwa rafiki muzuri. Unaweza kufanya nini juu ukuwe rafiki muzuri?

Juu mutu akuwe na marafiki wazuri, naye anapaswa kwanza kuwa rafiki muzuri

WATU FULANI WANASEMAKA: “Ni muzuri kuwa na rafiki hata akuwe wa namna gani, kuliko kubakia bila rafiki.”

  • Na weye unawaza nini?

KWA KIFUPI

Wakati tunachagula marafiki wazuri, tunamufurahisha Yehova na tunajiletea faida.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Juu ya nini Yehova anapenda tuchagule marafiki wazuri?

  • Tunapaswa kuepuka marafiki wa namna gani?

  • Unaweza kufanya nini juu upate marafiki wazuri?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Unapaswa kujua nini kuhusu kufanya urafiki na watu kupitia Enternete?

Tumia kwa Hekima Site za Enternete za Kupashana Habari (4:12)

Mu habari “Nilitamani Sana Kuwa na Baba,” ona mambo yenye ilifanya mwanaume fulani achunguze tena kama alikuwa na marafiki wazuri.

“Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 4, 2012)