Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 49

Unaweza Kufanya Nini Juu Familia Yako Ikuwe na Furaha?​—Sehemu ya 1

Unaweza Kufanya Nini Juu Familia Yako Ikuwe na Furaha?​—Sehemu ya 1

Watu wenye wametoka kuoana wanatumainiaka kama furaha yenye walikuwa nayo siku ya ndoa, itaendelea milele. Na inaweza kuendelea. Wakristo wenye wameoana kumepita miaka mingi na wenye wamejikaza sana kutumikisha mashauri ya Biblia, wanajua kama inawezekana.

1. Biblia inapatia bwana mashauri gani?

Yehova ameweka bwana kuwa kichwa cha familia, ni kusema yeye njo anapaswa kusimamia familia. (Soma Waefeso 5:23.) Yehova anapenda bwana akamate maamuzi yenye italetea familia faida. Biblia inashauria bwana hivi: “Muendelee kupenda bibi zenu.” (Waefeso 5:25) Namna gani bwana wanaweza kufanya vile? Bwana mwenye anapenda bibi yake, anamutendeaka muzuri ikuwe wakati wako wao wawili ao wakati wako na watu wengine. Anafanya yake yote juu bibi yake akuwe na furaha, anamulinda, na kumupatia vitu vyenye iko navyo lazima. (1 Timoteo 5:8) Na zaidi ya yote, anamusaidia akuwe na urafiki wa muzuri pamoja na Yehova. (Matayo 4:4) Kwa mufano, bwana anaweza kusali na kusoma Biblia pamoja na bibi yake. Wakati bwana anahangaikia bibi yake kwa upendo, ile inafanya ule bwana aendelee kuwa na urafiki muzuri pamoja na Yehova.​—Soma 1 Petro 3:7.

2. Biblia inapatia bibi mashauri gani?

Biblia inasema kama bibi “anapaswa kumuheshimia sana bwana yake.” (Waefeso 5:33) Anaweza kufanya vile namna gani? Anaweza kufikiria sifa za muzuri za bwana yake, na namna bwana yake iko najikaza juu ya kumuhangaikia yeye na watoto. Anaweza pia kuonyesha heshima kwa kuunga mukono maamuzi ya bwana yake, kwa kuzungumuza naye kwa heshima, na kusema mambo ya muzuri juu yake hata kama hamutumikie Yehova.

3. Bibi na bwana wanaweza kufanya nini juu ndoa yao ikuwe na furaha?

Biblia inasema kama wakati watu wawili wanaoana ‘wanakuwa mwili mumoja.’ (Matayo 19:5) Ni kusema wanapaswa kuepuka tabia ya kila mutu kuhangaikia mambo yake. Wanaonyesha kama wako mwili mumoja wakati wanajikaza kupitisha wakati pamoja na wakati kila mutu anajikaza kuambia mwenzake mawazo yake na namna anajisikia. Hawaache kitu ao mutu yeyote akuwe wa maana zaidi kuliko bibi ao bwana yao isipokuwa tu Yehova. Bibi ao bwana anajikaza sana juu asifanye urafiki wenye unapitisha mipaka na mutu mwingine mwenye haiko bibi ao bwana yake.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone namna kutumikisha kanuni za Biblia kunaweza kusaidia bibi na bwana wakuwe na furaha.

4. Bwana, upende na kuhangaikia bibi yako

Biblia inasema kama “bwana wanapaswa kupenda bibi zao kama miili yao wenyewe.” (Waefeso 5:28, 29) Ile inamaanisha nini? Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Bwana anaweza kufanya mambo gani juu ya kuonyesha kama anapenda na kuhangaikia bibi yake?

Musome Wakolosai 3:12, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Namna gani bwana anaweza kuonyesha zile sifa mu ndoa?

5. Bibi, upende na kuheshimia bwana yako

Biblia inashauria bibi aheshimie bwana yake, hata kama bwana yake hamutumikie Yehova. Musome 1 Petro 3:1, 2, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Kama bwana yako haiko Shahidi wa Yehova, ni wazi kama unapenda naye aanze kumutumikia Yehova. Nini njo inaweza kumusaidia sana, ni kukuwa namuhubiria-hubiria kila saa, ao kukuwa bibi muzuri na kumuheshimia? Juu ya nini unasema vile?

Bibi na bwana wanaweza kukamata maamuzi ya muzuri wakati wanazungumuza pamoja. Lakini, wakati fulani bibi anaweza kuwa na mawazo tofauti na ya bwana yake. Anaweza kueleza mawazo yake kwa upole na kwa heshima. Lakini, anapaswa kujua kama ni bwana njo Yehova amepatia daraka ya kukamata uamuzi wa mwisho mu familia. Njo maana, anapaswa kujikaza sana juu ya kuunga mukono maamuzi ya bwana yake. Kama anafanya vile, atasaidia familia yote ikuwe na furaha. Musome 1 Petro 3:3-5, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Yehova anajisikiaka namna gani wakati bibi anaheshimia bwana yake?

6. Munaweza kumaliza magumu mu ndoa yenu

Kila ndoa inakuwaka na magumu yake. Njo maana, bibi na bwana wanapaswa kusaidiana juu ya kupiganisha magumu yao. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, nini njo inaonyesha kama wale bibi na bwana hawakukuwa tena na furaha mu ndoa yao?

  • Walifanya nini juu ndoa yao ikuwe tena na furaha?

Musome 1 Wakorinto 10:24 na Wakolosai 3:13. Kisha kusoma kila andiko, muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini kutumikisha hii mashauri kunaweza kufanya ndoa ikuwe na furaha?

Biblia inasema kama tunapaswa kuheshimiana. Kuheshimia mutu, maana yake kumutendea muzuri na kwa adabu. Musome Waroma 12:10, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Bibi ao bwana anapaswa kungoya mwenzake njo akuwe wa kwanza kumuheshimia? Juu ya nini unasema vile?

WATU FULANI WANASEMAKA: “Mu ndoa yetu, hatukuwake tena marafiki sawa vile zamani.”

  • Unaweza kusema nini juu ya kuwafasiria kama Biblia inaweza kuwasaidia?

KWA KIFUPI

Bibi na bwana wanaweza kuwa na furaha kama wanapendana, wanaheshimiana, na kutumikisha kanuni za Biblia.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Bwana anaweza kufanya nini juu ndoa yake ikuwe na furaha?

  • Bibi anaweza kufanya nini juu ndoa yake ikuwe na furaha?

  • Kama ulishaoa ao kuolewa, ni kanuni gani ya Biblia inaweza kusaidia ndoa yenu ikuwe na furaha zaidi?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona mashauri yenye inaweza kusaidia familia yako ikuwe na furaha.

Familia Yenu Inaweza Kuwa na Furaha (broshua)

Angalia video ya muziki yenye inaonyesha faida ya kutumikisha mashauri ya Biblia mu ndoa yako.

Nakupenda Sana (4:26)

Ona namna mashauri ya Biblia inaweza kusaidia kabisa ndoa.

Biblia Iliokoa Ndoa Yetu (7:12)