Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 50

Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha​​—Sehemu ya 2

Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha​​—Sehemu ya 2

Watoto ni zawadi kutoka kwa Yehova. Anataka wazazi waitunze zawadi hiyo. Yehova ameandaa ushauri wenye hekima unaoweza kuwasaidia wazazi kuwalea watoto. Pia, ameandaa ushauri unaoweza kuwasaidia watoto kuchangia furaha katika familia.

1. Yehova amewapatia wazazi ushauri gani?

Yehova anataka wazazi wawapende watoto wao na watumie muda mwingi iwezekanavyo pamoja nao. Pia, Yehova anataka wazazi wawalinde watoto wao wasipate madhara na watumie kanuni za Biblia kama msingi wa kuwazoeza watoto wao. (Methali 1:8) Anawaambia hivi akina baba: “Endeleeni kuwalea [watoto wenu] katika . . . maagizo ya Yehova.” (Soma Waefeso 6:4.) Yehova anafurahi wazazi wanapofuata mwongozo wake wanapowalea watoto wao, na pia wanapoepuka kumpa mtu mwingine jukumu hilo.

2. Yehova anawapa watoto ushauri gani?

Yehova anawaagiza hivi watoto: “Watiini wazazi wenu.” (Soma Wakolosai 3:20.) Watoto wanapowaheshimu na kuwatii wazazi wao, wanamfurahisha Yehova na wazazi wao pia. (Methali 23:22-25) Yesu aliweka mfano mzuri alipokuwa mtoto. Ingawa alikuwa mkamilifu, aliwatii na kuwaheshimu wazazi wake.​—Luka 2:51, 52.

3. Mnawezaje kumkaribia Mungu zaidi mkiwa familia?

Ikiwa wewe ni mzazi, bila shaka unataka watoto wako wampende Yehova kama wewe unavyompenda. Unawezaje kufanikiwa kufanya hivyo? Kwa kufuata ushauri huu wa Biblia: “Nawe lazima uyakazie [maneno ya Yehova] kwa wanao na kuongea kuyahusu unapoketi nyumbani mwako na unapotembea barabarani.” (Kumbukumbu la Torati 6:7) ‘Kukazia’ kunamaanisha kufundisha jambo kwa kulirudia. Huenda unajua kwamba ili watoto wakumbuke jambo unalowafundisha unahitaji kulirudia tena na tena. Andiko hili linamaanisha kwamba unapaswa kuwa na muda wa kuzungumza na watoto wako kwa ukawaida kumhusu Yehova. Ni vizuri kutenga wakati kila juma ili kumwabudu Yehova mkiwa familia. Ikiwa huna watoto, bado unaweza kunufaika ikiwa utatenga wakati kila juma ili kujifunza Neno la Mungu.

CHIMBA ZAIDI

Chunguza mapendekezo yanayoweza kuchangia furaha na usalama katika familia.

4. Wafundishe watoto wako kwa upendo

Kumfundisha mtoto kunaweza kutokeza changamoto. Biblia inawezaje kukusaidia? Soma Yakobo 1:19, 20, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Wazazi wanaweza kuonyeshaje upendo wanapozungumza na watoto wao?

  • Kwa nini mzazi hapaswi kamwe kuwatia watoto wake nidhamu akiwa amekasirika? a

5. Walinde watoto wako

Ili uwalinde watoto wako wasitendewe vibaya kingono, ni muhimu sana uzungumze waziwazi na kila mtoto kuhusu ngono. Huenda isiwe rahisi kufanya hivyo. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.

  • Kwa nini ni vigumu kwa baadhi ya wazazi kuzungumza na watoto wao kuhusu ngono?

  • Wazazi fulani wametumia njia gani kuwaeleza watoto wao kuhusu ngono?

Kama ilivyotabiriwa, uovu unazidi kuongezeka katika ulimwengu wa Shetani. Soma 2 Timotheo 3:1, 13, kisha mzungumzie swali hili:

  • Baadhi ya watu waovu waliotajwa kwenye mstari wa 13 wanawatendea watoto vibaya kingono. Basi, kwa nini ni muhimu kwa wazazi kuzungumza waziwazi na watoto wao kuhusu ngono na kuwaeleza jinsi wanavyoweza kujilinda dhidi ya watu wanaoweza kuwatendea vibaya?

Je, wajua?

Mashahidi wa Yehova wameandaa habari nyingi zinazoweza kuwasaidia wazazi kuwaeleza watoto wao kuhusu ngono, na jinsi ya kuwalinda wasitendewe vibaya kingono. Kwa mfano, tazama:

6. Waheshimu wazazi wako

Watoto na vijana wanaweza kuwaonyesha wazazi wao heshima kupitia jinsi wanavyozungumza nao. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.

  • Kwa nini ni muhimu kijana azungumze kwa heshima na wazazi wake?

  • Kijana anawezaje kuzungumza na wazazi wake kwa heshima?

Soma Methali 1:8, kisha mzungumzie swali hili:

  • Kijana anapaswa kutendaje anapopata mwongozo kutoka kwa wazazi wake?

7. Jinsi ya kumwabudu Yehova mkiwa familia

Familia za Mashahidi wa Yehova hutenga muda hususa kila juma ili kumwabudu Yehova pamoja. Ibada hiyo ya familia inahusisha mambo gani? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.

  • Familia inawezaje kupanga ratiba ya kufanya Ibada ya Familia kwa ukawaida?

  • Wazazi wanawezaje kufanya ibada ya familia iwe yenye kunufaisha na kufurahisha?​—Ona picha mwanzoni mwa somo hili.

  • Ni nini kinachoweza kufanya iwe vigumu kwa familia yenu kujifunza pamoja?

Katika taifa la kale la Israeli, Yehova alitaka familia zizungumze kwa ukawaida kuhusu Maandiko. Soma Kumbukumbu la Torati 6:6, 7, kisha mzungumzie swali hili:

  • Unawezaje kutumia kanuni hii?

Mambo mnayoweza kufanya katika ibada ya familia:

  • Kutayarisha mikutano ya kutaniko.

  • Kusoma na kuzungumzia simulizi la Biblia ambalo familia yenu itafurahia.

  • Ikiwa mna watoto, pakua au uchapishe mojawapo ya makala ya watoto iliyo kwenye jw.org/sw.

  • Ikiwa mna vijana, zungumzieni mojawapo ya makala kuhusu vijana kwenye jw.org/sw.

  • Igizeni simulizi la Biblia pamoja na watoto wenu.

  • Tazameni na mzungumzie mojawapo ya video kwenye jw.org/sw.

WATU FULANI HUSEMA: “Watoto hawawezi kuielewa Biblia.”

  • Wewe una maoni gani?

MUHTASARI

Yehova anataka wazazi wawapende, wawafundishe, na kuwalinda watoto wao, pia, anataka watoto wawaheshimu na kuwatii wazazi wao, na anataka familia zimwabudu pamoja.

Ungejibuje?

  • Wazazi wanawezaje kuwafundisha na kuwalinda watoto wao?

  • Watoto wanawezaje kuwaheshimu wazazi wao?

  • Kuna manufaa gani ya kutenga wakati kila juma ili kumwabudu Yehova mkiwa familia?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Mtoto anapaswa kujifunza masomo gani yatakayomsaidia atakapokuwa mtu mzima?

“Masomo Sita Muhimu ya Kuwafundisha Watoto” (Amkeni! Na. 2 2019)

Jifunze ushauri ambao Biblia inawapa wale wanaowatunza wazazi waliozeeka.

“Biblia Inasema Nini Kuhusu Kutunza Wazazi Waliozeeka?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

Ona mwanamume ambaye hakujua jinsi ya kuwalea watoto alivyofanikiwa kuwa baba mzuri.

Yehova Alitufundisha Kuwalea Watoto Wetu (5:58)

Jifunze jinsi akina baba wanavyoweza kuimarisha uhusiano wao na watoto wao wa kiume.

“Akina Baba Wanawezaje Kuwa na Uhusiano wa Karibu na Wana Wao?” (Mnara wa Mlinzi, Novemba 1, 2011)

a Katika Biblia, “nidhamu” inatia ndani kufundisha, kuongoza, na kurekebisha. Lakini haihusishi kamwe kumtendea mtoto vibaya au kwa ukatili.​—Methali 4:1.